Sunday, December 27, 2015

  CHAGUA LEO UNAPENDA KUWA KAMA   NANI MAISHANI






Kama wewe ni Mzazi, ni rahisi sana mtoto wako kutamani kuwa kama wewe kitabia au kimafanikio. Utamsikia mtoto akisema maneno kama, “nataka nije kuwa daktari kama baba au mama, nataka niwe nashika majambazi kama baba ” n.k. Vivyo hivyo kupitia waalimu wanaomfundisha shuleni, anaweza kupenda jinsi mwalimu wake alivyo na jinsi anavyofundisha na kutamani siku moja kuwa hivyo.

Nakumbuka nilianza kupata hamasa ya kutafuta njia za kupata mafanikio kwa kutumia ujuzi na kipawa ambacho Mungu ameweka ndani yangu kupitia mafunzo ya Bwana Robert Kiyosaki, ambaye ni Mwandishi mkubwa wa vitabu mbalimbali vya Uwekezaji, Kujitambua, Elimu ya biashara n.k. Moja ya kitabu kilichompa umaarufu hadi sasa ni kitabu cha “RICH DAD POOR DAD”. Lakini pia kuna kitabu cha Wajasiriamali waliofanikiwa kiitwacho “MIDAS TOUCH” kumfundisha Mjasiriamali mambo matano ambayo anapaswa kuwa nayo ili kufanikiwa, na vitabu vingine vingi kama “Unfair Advantage” na “Second Chance”. Kwa jinsi ambavyo ameelezea safari yake ya mafanikio kutoka katika mazingira magumu hadi kuwa Milionea ilinipa nguvu sana na hamasa na tangu kipindi hicho niliweza kujitambua na kuamini ipo siku na mimi nitapiga hatua fulani kimaisha. Hata wewe pia unaweza, tambua hazina iliyoko ndani yako kupitia somo hili na kwenye vitabu mbalimbali. Vivyo nikaanza kutamani kuwa kama huyu jamaa kimafanikio, japokuwa safari bado ni ndefu lakini naamini nitafika tu kwa neema ya Mwenyezi Mungu atupae yote.
Lackson Tungaraza


Hicho ndicho nilichotaka kukizungumzia leo. Ukweli ni kwamba watu wengi sana ambao unawaona wana mafanikio makubwa sana, wana watu wao ambao waliwaweka mbele. Kwa mfano, wewe unafanya biashara, je ni mfanya biashara gani mkubwa ambaye ungependa uwe kama yeye? Je, umedhamiria kweli kufikia mafanikio aliyo nayo huyo “Role Model” wako?

Kama wewe ni Mwanafunzi , ungetamani siku moja uwe kama msomi gani mashuhuri nchini? Kama unacheza mpira, ni mchezaji gani maarufu ambaye siku moja utafurahi ukiwa katika kiwango chake na kufikia mafanikio yake? Hilo ni jambo la msingi sana la kulifanyia kazi ili uweze kuongeza jitihada katika fani unayotarajia ikufikishe kwenye ulimwengu wa mafanikio.
Ukiwa mafanyabiashara na ukatamani uwe na mafanikio makubwa kama aliyonayo Saidi Bakhresa, lazima utakuwa na nidhamu katika fedha zako na utatumia mbinu sahihi za kibiashara ambazo mfanyabiashara huyo ametumia.


Uzuri ni kwamba, watu wengi wenye mafanikio, historia zao zinapatikana. Baadhi maisha yao yapo kwenye vitabu, wengine kwenye vitabu, wengine kwenye mitandao, hivyo ni rahisi sana kujifunza nini walikifanya mpaka kufikia walipo, changamoto walizopitia na jinsi walivyokabiliana nazo. Mfano hai wa hapa nchini ni Bwn. Erick Shigongo ambaye alikuwa amemtanguliza mbele mfanyabiashara mkubwa sana, Reginald Mengi kama “role model” wake. Je, wewe ungependa kuwa kama nani? Je ,kuna mtu ambaye unafuata nyayo zake? Kama unataka kuwa kama Shigongo, je unajua alikopitia mpaka alipo sasa? Wewe pia amini siku moja unaweza kuwa kama Fulani ambaye ana mafanikio makubwa kama tu utakuwa na dhamira ya kweli. Hebu changia mawazo yako  hapa kwa jinsi ulivyojifunza kupitia hii mada.

Related Posts:

  • LACKSON TUNGARAZA NI NANI HASWA? I- Mjasiriamali (Entrepreneur) kwa kuwa sehemu ya kuleta Suluhu ya Matatizo Yaliyopo kwenye Jamii. (SOCIAL ENTREPRENEUR). II- Mwamasishaji (Motivator) kwa Kuwasaidia Waliovunjika mioyo, waliyokata tamaa ya kusonga mb… Read More
  • KUWA MC (Master Of Ceremony) "UKITAKA KUWA MC (Master Of Ceremony) UNAYEPENDWA ZAIDI MJINI, Unapaswa Kuwa na SIFA Mbili Kuu; (I) Uwezo wa Kuwafurahisha Watu, Hata kama ni kwa Mambo ya Kijinga na Yasiyokuwa na maana. (II) Uwezo wa Kuwafanya Watu W… Read More
  • SUALA LA KUFANIKIWA au KUTOKUFANIKIWA LIKO MIKONONI MWETU Yesu alizaliwa kwenye familia ya kawaida kabisa, akawa mwana wa Seremala aitwaye Yusufu. Mazingira aliyokulia hayakuwa na Intaneti, mitandao ya Simu, mitandao ya Kijamii kama Facebook, Twitter, Youtube, na Instagram. Wala h… Read More
  • USIPOTEZE TENA MUDA WAKO NA VIFURUSHI VYAKO VYA INTANETI MTANDAONIWatu Wengi huwa Wananunua Vifurushi vya Intaneti Ili Waelimike Mtandaoni, Lakini huwa hawafikii hayo Malengo Yao. - Unakuta Mtu anaingia YouTube ili apate Elimu ya kumsaidia Kukua Kiroho au Kiuchumi, lakini anaishia kuanga… Read More
  • JIPATIE VITABU_BORA_2019. Kitabu cha Kwanza: "MBINU 16 ZA KUONGEZA MAUZO KWENYE BIASHARA YAKO.". - Ndani ya Kitabu hiki Utapata Mbinu 16 za uhakika za Kukusaidia katika Kuongeza Mauzo (SALES) kwenye Biashara Yako yo yote Ile uifanyayo Mtan… Read More

1 comment:

  1. ukiwa na role model mzuri, hutojutia hiyo safari yako..
    nini maoni yako juu ya hili?

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI