Sunday, December 27, 2015

  CHAGUA LEO UNAPENDA KUWA KAMA   NANI MAISHANI






Kama wewe ni Mzazi, ni rahisi sana mtoto wako kutamani kuwa kama wewe kitabia au kimafanikio. Utamsikia mtoto akisema maneno kama, “nataka nije kuwa daktari kama baba au mama, nataka niwe nashika majambazi kama baba ” n.k. Vivyo hivyo kupitia waalimu wanaomfundisha shuleni, anaweza kupenda jinsi mwalimu wake alivyo na jinsi anavyofundisha na kutamani siku moja kuwa hivyo.

Nakumbuka nilianza kupata hamasa ya kutafuta njia za kupata mafanikio kwa kutumia ujuzi na kipawa ambacho Mungu ameweka ndani yangu kupitia mafunzo ya Bwana Robert Kiyosaki, ambaye ni Mwandishi mkubwa wa vitabu mbalimbali vya Uwekezaji, Kujitambua, Elimu ya biashara n.k. Moja ya kitabu kilichompa umaarufu hadi sasa ni kitabu cha “RICH DAD POOR DAD”. Lakini pia kuna kitabu cha Wajasiriamali waliofanikiwa kiitwacho “MIDAS TOUCH” kumfundisha Mjasiriamali mambo matano ambayo anapaswa kuwa nayo ili kufanikiwa, na vitabu vingine vingi kama “Unfair Advantage” na “Second Chance”. Kwa jinsi ambavyo ameelezea safari yake ya mafanikio kutoka katika mazingira magumu hadi kuwa Milionea ilinipa nguvu sana na hamasa na tangu kipindi hicho niliweza kujitambua na kuamini ipo siku na mimi nitapiga hatua fulani kimaisha. Hata wewe pia unaweza, tambua hazina iliyoko ndani yako kupitia somo hili na kwenye vitabu mbalimbali. Vivyo nikaanza kutamani kuwa kama huyu jamaa kimafanikio, japokuwa safari bado ni ndefu lakini naamini nitafika tu kwa neema ya Mwenyezi Mungu atupae yote.
Lackson Tungaraza


Hicho ndicho nilichotaka kukizungumzia leo. Ukweli ni kwamba watu wengi sana ambao unawaona wana mafanikio makubwa sana, wana watu wao ambao waliwaweka mbele. Kwa mfano, wewe unafanya biashara, je ni mfanya biashara gani mkubwa ambaye ungependa uwe kama yeye? Je, umedhamiria kweli kufikia mafanikio aliyo nayo huyo “Role Model” wako?

Kama wewe ni Mwanafunzi , ungetamani siku moja uwe kama msomi gani mashuhuri nchini? Kama unacheza mpira, ni mchezaji gani maarufu ambaye siku moja utafurahi ukiwa katika kiwango chake na kufikia mafanikio yake? Hilo ni jambo la msingi sana la kulifanyia kazi ili uweze kuongeza jitihada katika fani unayotarajia ikufikishe kwenye ulimwengu wa mafanikio.
Ukiwa mafanyabiashara na ukatamani uwe na mafanikio makubwa kama aliyonayo Saidi Bakhresa, lazima utakuwa na nidhamu katika fedha zako na utatumia mbinu sahihi za kibiashara ambazo mfanyabiashara huyo ametumia.


Uzuri ni kwamba, watu wengi wenye mafanikio, historia zao zinapatikana. Baadhi maisha yao yapo kwenye vitabu, wengine kwenye vitabu, wengine kwenye mitandao, hivyo ni rahisi sana kujifunza nini walikifanya mpaka kufikia walipo, changamoto walizopitia na jinsi walivyokabiliana nazo. Mfano hai wa hapa nchini ni Bwn. Erick Shigongo ambaye alikuwa amemtanguliza mbele mfanyabiashara mkubwa sana, Reginald Mengi kama “role model” wake. Je, wewe ungependa kuwa kama nani? Je ,kuna mtu ambaye unafuata nyayo zake? Kama unataka kuwa kama Shigongo, je unajua alikopitia mpaka alipo sasa? Wewe pia amini siku moja unaweza kuwa kama Fulani ambaye ana mafanikio makubwa kama tu utakuwa na dhamira ya kweli. Hebu changia mawazo yako  hapa kwa jinsi ulivyojifunza kupitia hii mada.

Related Posts:

  • HATUA ZA MAFANIKIO "MAFANIKIO hayaji kwa Ukubwa au Udogo wa kile Ulichonacho, bali kwa namna Unavyotumia kile Ulichonacho" ~Lamax Kila siku nikikumbuka Hatua nilizopitia Kufika hapa nilipo Leo Kimaisha, ninapata hamasa ya Kumshukuru Mungu k… Read More
  • FIND_SOMETHING_TO_DIE_FOR_THAN_TO_LIVE_FOR FANYA JAMBO la Kumfanya MUNGU azidi Kuona  Umuhimu wa Kukuacha Uendelee kuwa HAI hapa duniani. JAMBO la Kumfanya MUNGU aone KUNA PENGO wakati  wa Kuugua Kwako (Kupatwa na Magonjwa) ili AKUPONYE HARAKA URUDI… Read More
  • BADO UNAENDELEA KUVUNJA LAANA ZA UMASKINI? Tangu Uanze kuvunja Laana za UMASKINI, huu ni Mwaka wa ngapi, na Je Umeshaanza kuwa TAJIRI? Kabla ya Kuanza au Kuendelea tena na Uvunjaji Wako wa Laana za UMASKINI, Tathimini Kwanza ni kwa Jinsi Umejitoa Kulipa Gharama … Read More
  • UNAMALIZAJE HUU MWAKA WA 2017?? Kati ya maeneo ambayo huwa yanawatia watu Joto Kubwa ni eneo la Umalizaji. Umalizaji huu huenda mbali zaidi katika mchezo wa Mpira, katika Utumishi, kwenye Chumba cha Mitihani, kwenye Ndoa, Uchaguzi Mkuu n.k... Eneo hili hu… Read More
  • NJIA MPYA YA KUTENGENEZA KIPATO CHA ZIADAHaijalishi una Kazi ama hauna Kazi, kikubwa ni UTAYARI wako pamoja na Kiasi kidogo cha #PESA kuanzia Tsh.4000/= Sasa Unaweza Kutengeneza Kipato cha Ziada (PESA) kupitia Kitabu changu "SITARUDI NYUMA TENA" - Sitaki KUFANIKI… Read More

1 comment:

  1. ukiwa na role model mzuri, hutojutia hiyo safari yako..
    nini maoni yako juu ya hili?

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI