Monday, June 20, 2016

Kijana mwenzangu kabla hujaanza kusumbuka kutafuta pesa kila mahala kwaajili ya biashara. 
Kwanza Fanya maamuzi ni biashara gani unayohitaji kufanya, hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Kwanini ufanye uwamuzi kwanza? Ili kukupa Nidhamu ya pesa.

Pesa pia inahitaji Nidhamu kubwa, hivyo bila nidhamu pesa yako itapotea bure. Utakuta baada ya kupata pesa unaanza kuwaza sijui nifungue hoteli au niuze mbao au nichome Mahindi au niuze kitimoto n.k lakini ukishatambua biashara gani utafanya ukishapata pesa yako, utakuwa na nidhamu Mara baada ya kuipata pesa hiyo.
Jambo la pili:

 baada ya kufahamu ni biashara gani utafanya baada ya kupata fedha. Ni vyema pia ufanye uchunguzi juu ya uendeshwaji wa hyo biashara... Kama ikiwezekana nenda hata mtaa wa pili au wilaya nyingine na kutafuta Mtu ambaye anafanya biashara hyo na umuulize yeye  jinsi  alivyoweza kufanikiwa... Kumbuka kuwa na mazungumzo yenye hekima siyo kukurupuka tu kama mtu aliyeng'atwa na nyoka halafu akatupiwa Jani shingoni. Acha Aibu, uliza waliokutangulia na ninaona vyema iwe ni mtu ambaye Yuko mbali na mahali hapo ulipo ili asipate ugumu wa kukupa siri ya mafanikio.


Jambo la Tatu,
Weka Juhudi katika biashara uliyoamua kuifanya... Kwa moyo wako wote...uipende biashara yako. Focus.
F-Follow
O-One
C-Course
U-Until
S-Successful

Hakikisha unatumia kila mbinu kuifikisha biashara yako katika hatua kubwa. Siyo Leo unashona nguo, kesho unauza viazi na kesho kutwa umefungua kibanda cha chips. Wekeza faida katika biashara yako ili iwe kubwa. Jiulize: unadhani Barhesa hana pesa ya kuanza kutengeneza nguo na kuuza? Anazo pesa nyingi tu lakini ameamua kuFOCUS... Kufanya kile ulichonacho kuwa uhai wako. Fanya hiyo baishara kwa ustadi mkubwa na utafanikiwa tu. Love what you do and you will be successful.
“Success is not the Key to Happiness. Happiness is the key to Success. If you love what you are doing, you will be successful” –Albert Schweitzer.

Ahsante sana. Karibu kwa maswali na Mchango wako

WhatsApp: 0764793105 [Lackson Tungaraza]
Facebook: www.facebook.com/ltungaraza
Instagram: LACKSONTUNGARAZA



Related Posts:

  • MTAJI KWA KIJANA NI UPI...! Proudly Sponsored by N.Y.I MOVEMENT *Join and Be part of the Change*. Kuna mambo mbali mbali ambayo wewe kama Kijana mwenzangu unaweza fanya pasipokuwa na pesa kubwa Bali hiyo hiyo uliyonayo hapo .... Akili, maarifa… Read More
  • FACEBOOK VS BLOG KIPI NI BORA KWA BIASHARA YAKO? Kumekuwa na sitofahamu juu ya namna ya kutumia mitandao hii katika kukuza biashara. Ndiyo maana nimekuuliza; Kati ya Facebook na Blog, ni kipi bora kwa Biashara yako? Jibu lako litaash… Read More
  • SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA  “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA”  Tunashindwa kuongeza vipato vyetu kwa sababu biashara zetu hazina mvuto. Tunapoendelea kufungua vyanzo vingine vya vipato kwa kut… Read More
  • MAMBO MATATU MUHIMU YA KUFANYA KIJANA KABLA YA KUANZA KUTAFUTA PESA YA KUFANYA BIASHARA Kijana mwenzangu kabla hujaanza kusumbuka kutafuta pesa kila mahala kwaajili ya biashara.  Kwanza Fanya maamuzi ni biashara gani unayohitaji kufanya, hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Kwanini ufanye uwamuzi kwanza? Ili k… Read More
  • UJASIRIAMALI NI NINI? Kuna tafsiri mbali mbali katika vichwa vya watu na katika mitandao ya kijamii juu ya dhana ya UJASIRIAMALI. Wengi wamepata tafsiri zilizowapa presha na kuamua kuacha kuwa WAJASIRIAMALI, na baadhi hawatambua ni kwa namna gan… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI