Monday, June 20, 2016

Kijana mwenzangu kabla hujaanza kusumbuka kutafuta pesa kila mahala kwaajili ya biashara. 
Kwanza Fanya maamuzi ni biashara gani unayohitaji kufanya, hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Kwanini ufanye uwamuzi kwanza? Ili kukupa Nidhamu ya pesa.

Pesa pia inahitaji Nidhamu kubwa, hivyo bila nidhamu pesa yako itapotea bure. Utakuta baada ya kupata pesa unaanza kuwaza sijui nifungue hoteli au niuze mbao au nichome Mahindi au niuze kitimoto n.k lakini ukishatambua biashara gani utafanya ukishapata pesa yako, utakuwa na nidhamu Mara baada ya kuipata pesa hiyo.
Jambo la pili:

 baada ya kufahamu ni biashara gani utafanya baada ya kupata fedha. Ni vyema pia ufanye uchunguzi juu ya uendeshwaji wa hyo biashara... Kama ikiwezekana nenda hata mtaa wa pili au wilaya nyingine na kutafuta Mtu ambaye anafanya biashara hyo na umuulize yeye  jinsi  alivyoweza kufanikiwa... Kumbuka kuwa na mazungumzo yenye hekima siyo kukurupuka tu kama mtu aliyeng'atwa na nyoka halafu akatupiwa Jani shingoni. Acha Aibu, uliza waliokutangulia na ninaona vyema iwe ni mtu ambaye Yuko mbali na mahali hapo ulipo ili asipate ugumu wa kukupa siri ya mafanikio.


Jambo la Tatu,
Weka Juhudi katika biashara uliyoamua kuifanya... Kwa moyo wako wote...uipende biashara yako. Focus.
F-Follow
O-One
C-Course
U-Until
S-Successful

Hakikisha unatumia kila mbinu kuifikisha biashara yako katika hatua kubwa. Siyo Leo unashona nguo, kesho unauza viazi na kesho kutwa umefungua kibanda cha chips. Wekeza faida katika biashara yako ili iwe kubwa. Jiulize: unadhani Barhesa hana pesa ya kuanza kutengeneza nguo na kuuza? Anazo pesa nyingi tu lakini ameamua kuFOCUS... Kufanya kile ulichonacho kuwa uhai wako. Fanya hiyo baishara kwa ustadi mkubwa na utafanikiwa tu. Love what you do and you will be successful.
“Success is not the Key to Happiness. Happiness is the key to Success. If you love what you are doing, you will be successful” –Albert Schweitzer.

Ahsante sana. Karibu kwa maswali na Mchango wako

WhatsApp: 0764793105 [Lackson Tungaraza]
Facebook: www.facebook.com/ltungaraza
Instagram: LACKSONTUNGARAZA



Related Posts:

  • KUWA STARRING WA MAISHA YAKO. ~Nilipokuwa mtoto nilipendelea sana kutazama muvi za ngumi ( action movies), katika kuangalia kwangu nilishangaa kuona ya kwamba muhusika mkuu wa Muvi ambaye ndiye anaitwa STARRING alikuwa hafi hata kama amekutana na maj… Read More
  • PATA MAARIFA KWA KUWA MKIMYA ~ Wanadamu hata siku moja haitawahi kutokea tukawa sawa kimtazamo, kimienendo..never. Unaweza ukajiulza mbona Mimi ninajiheshima, mpole, mvumilivu lakini huyu ndugu yangu ni mkorofi sana, mlevi, mbeya, mzinzi n.k. Hyo … Read More
  • JIFUNZE JINSI YA KUTUMIA KINYWA CHAKO VIZURI NGUVU YA MANENO YATOKAYO KATIKA VINYWA VYETU Walisema manabii na mitume, “Atakaye kupenda maisha na kuona siku njema auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isinene hila” (1 Petro 3:10). Wengine wakaongezea”Mtu a… Read More
  • MAMBO MATATU MUHIMU ILI MTU AWEZE KUFANIKIWA. By Lackson Tungaraza 0764793105 whatsapp Hapo ulipo sahivi unaangaika kwasababu unataka Mafanikio, jiulize kwanza Mafanikio yana maana gani kwa upande wako!! Kila mmoja wetu anahitaji mafanikio katika mambo anayoyafany… Read More
  • SIRI INAYOVUTA MAFANIKIO SIRI INAYOVUTA MAFANIKIO  Nitakuwa muongo sana kama nikisema ya kwamba hamna mtu anayependa Mafanikio, hata wewe umechukua muda wako kusoma makala hii kwa sababu unapenda kufanikiwa kupitia hii Siri Inayovuta Mafa… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI