Friday, June 3, 2016


Maisha ya Mwanadamu yana mwanzo na mwisho, ikiwa na maana ya kwamba kuna kuzaliwa na kufariki. Lakini katikati ya kuzaliwa na kufariki kuna mambo ambayo Mwanadamu anatakiwa afanye ili aweze kustahimili hali ya kimwili na kiroho pia.
.
Dira ndiyo inayomwongoza Rubani kuifikisha Ndege mahala salama, pasipokuwa na Dira Rubani anaweza kwenda mahala pasipo sahihi na hata wakati mwingine kupata ajali. Kama wanadamu tunaoishi duniani, pasipokuwa na Dira inayotuongoza ni rahisi sana kupoteza muda mwingi katika kufanya mambo ambayo hatutakiwi kufanya, hatimaye kuangamia katika Uharibifu

Ulishawahi kuona  siku nzima inapita katika maisha yako na huoni jambo la muhimu ulilofanya, au ulifanya ambayo hukutakiwa kufanya? That’s lack of Direction/Daily Schedule

Nimejifanyia utafiti binafsi [Lackson Tungaraza], kati ya kuishi maisha ya Ratiba na yasiyo na ratiba. Ndugu yangu unayesoma taarifa hii, Maisha yasiyo na Ratiba ni sawa na Samaki pasipokuwa na maji. Nilikuwa namaliza siku nzima wakati mwingine pasipokufanya jambo lolote ambalo linaendana na Malengo yangu ya muda fulani.
Ukitaka siku yako iwe yenye thamani na hata ukatamani ijirudie tena, uwe na Dira inayokuongoza kila siku kwasababu siku huzaa wiki na wiki huzaa mwezi na miezi huzaa miaka na miaka huzaa urefu wa maisha ya mtu.

Anza kidogo kidogo, haba na haba hujaza kibaba. Kila siku jioni andika mambo hata matatu/matano ambayo kwa siku inayofuata utayafanya kwa Ufasaha na kuyamaliza ndani ya siku husika.
MFANO WA UPANGAJI WA RATIBA KWA SIKU INAYOFUATA. WEWE NDIYE RUBANI WA MAISHA YAKO.... KUWA MPYA KILA SIKU.


Kumbuka; Hayo mambo ambayo unayapanga kufanya, yawe yanaendana na Ndoto uliyonayo juu ya maisha yako ya baadae. Kama hayaendani na kule unakotaka kufika, yaache hata kama ni yenye kufurahisha kwa wakati huo

Mfano.. Una ndoto ya kuwa Mfanyabiashara mkubwa baadae ambaye utakuwa ukiwashauri watu jinsi ya kutumia fedha vyema halafu Rafiki zako wanakuambia muende kwenye kumbi za starehe kutafuta mwanawake wa kulala nao, acha kabisa kwasababu utapoteza Nidhamu ya Pesa na pia Afya yako kuwa katika hali ya hatari kupata Magonjwa hatarishi. Na ukishakuwa na Afya mbovu, hutofurahia mafanikio ambayo utapata katika maisha yako… Afya Bora ni Msingi Imara wa kukufikisha kule unakohitaji kwenda… huwezi kufanya kazi kwa muda mrefu ikiwa Afya yako siyo Imara… Ishi kwa tahadhari… Kinga ni bora kuliko Tiba.

Ahsante sana kwa muda uliyoutumia kusoma makala haya, naamini ya kwamba kuanzia sasa utakuwa na maisha yenye furaha na thamani kila siku kwasababu utakuwa na Dira ya kukuongoza… shea na rafiki zako ujumbe huu na kutoa maoni yako…
0764793105 WhatsApp/call/sms.



1 comment:

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI