Saturday, March 5, 2016


 By Lackson Tungaraza
0764793105 whatsapp.

Habari yako rafiki yangu mpendwa?
Baada ya kuwa tumejifunza mada mbalimbali za ukombozi wa fikra na mafanikio ya kiuchumi. Napenda kukushukuru kwa ufuatiliaji wako katika masomo yangu na pia kwa kuhudhuria semina zangu za Ujasiriamali kwa njia ya Email na Whatsapp. Pia ni matumaini yangu ya kwamba utakuwa umepiga hatua kiMaisha. Leo tutajifunza jinsi ya kuweka Malengo na Njia za kufanikisha Malengo yako;

                      1.  NAMNA YA KUWEKA MALENGO YANAYOFIKIKA;

Malengo ni Mipango ya muda mfupi; yaweza kuwa ni siku, wiki, mwezi au mwaka. Moja ya sifa kubwa ya Malengo ni lazima yawe SMART;
S-Specific (Malengo yako yawe wazi)
M-Measurable (Yenye Uwezo wa kupimika kujua ni nguvu na jitihada kiasi                 vinahitajika ili kuyafikia)
A-Attainable (Yenye kufikika, usipange ambayo huwezi kutimiza)
R-Realistic (Yaweze kuakisi Uhalisia)
T- Timed (Yenye kutimia ndani ya muda fulani).

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine huwa anajiwekea malengo ambayo anatamani baada ya muda fulani yawe yametimia, yaweza kuwa ni malengo ya kiroho au kimwili. Utofauti unakuja kwenye namna ya kuweka hayo malengo, kuna wanaotumia nguvu nyingi na wengine nguvu kidogo. Nitakupa njia fupi hii leo;

Ili kuyafikia Malengo yako kwa urahisi, ni vyema ukatumia SHORTEST PLAN ili usiwahi kuchoka njiani. Weka Malengo yako katika Vipengele vidogo vidogo. Inawezekana unataka kuwa Mwandishi mkubwa wa vitabu, ni vyema ukaliweka hilo lengo lako katika Vipengele. Anza kuandika kila siku hata  hadithi moja au Insha yoyote ile ili kuweka ufahamu wako sawa. Kwa kufanya hivyo utapiga hatua fulani kila siku kwa urahisi zaidi, utajikuta baada ya miezi kadhaa unahadithi nyingi na Insha na unaweza kuwa na kitabu chako. 
  
Mimi binafsi Lackson Tungaraza, njia hii imenisaidia sana kuyafikia Malengo yangu na bado ninaitumia kila siku. Sitaki kutenda yale yale kila siku, kila siku ninajipangia jambo jipya la kufanya; Yaweza kuwa ni kuweka Blog yangu vizuri na kuweka Makala, kuongeza ujuzi wa kutumia mitandao kibiashara, kusoma vitabu mbali mbali n.k. Hii yote ili baadae niwe Gwiji na Sumaku katika Masoko ya biashara.

Don’t think about what can happen in a month or a year, focus on the 24 hours ahead of you and do what you can to get closer to where you want to be

                     2.  NAMNA YA KUFANIKISHA MALENGO YAKO;

Baada ya kujifunza namna ya kuweka Malengo yanayofikika kwa urahisi, naamini ya kwamba umeanza kuweka elimu hii katika matendo. Kumbuka kuyaandika Malengo na vipengele vyake katika daftari la kumbukumbu (notebook) au kwenye simu, kompyuta na kuweka mahali ambapo panafikika. Yaani mahali ambapo ni rahisi kwako kuyaona na kujikumbusha kila mara ili kuamsha nguvu mpya ndani yako; Yaweza kuwa ni chumbani, sebuleni, kwenye gari, dressing table n.k.
Tutajifunza namna ya kufanikisha Malengo yako ambayo umekwisha kuyaweka katika vipengele na kuhifadhi mahali ambapo ni rahisi kufikika. Fuata hatua hizi chache tu;

                i.   Uwe na Nidhamu~ Have Discipline
Nidhamu/discipline ni neno pana sana kwa sababu linatumika kila mahali kwa wakati wake. Shuleni ili mwanafunzi afaulu vizuri inabidi awe na nidhamu nzuri, vivyo hivyo Maofisini na Serikalini. Kumbe Nidhamu ni jambo la muhimu sana!! Tia bidii katika kutimiza malengo yako, usiwe mtu wa visingizio na kughairi kila wakati, kumbuka umri unaenda na muda haukusubiri. Huyo mzee unayemwona hapo, kuna wakati naye alikuwa ni kijana kama wewe.

Rafiki yangu mpendwa, unatakiwa kuwa na nidhamu ili Malengo yako yapate kutimia ndani ya muda ulioweka. Nidhamu ya kujali muda wako, nidhamu ya kuthamini mwili wako na pia watu unaochangamana nao. Ikiwa lengo lako ni la mwezi mmoja, basi hakikisha unalitimiza ndani ya mwezi huo.

               ii.  Jiamini~ Have Confidence in yourself
Kijana mmoja mdogo Daudi alimwua Goliathi, bonge la mtu lenye miraba mine kwa sababu ya kujiamini. Unapojiamini, ule uwezo uliyoko ndani yako unapata nafasi ya kujidhihirisha wazi wazi. Jiamini ya kwamba unaweza kuyatimiza Malengo yako ndani ya muda uliyojipangia. Usitolewe katika mstari wa mafanikio na watu wasiojua mbele wala nyuma, wapo wapo tu, kumbuka kuwa mtendaji siyo msomaji tu wa post na kukaa kimya

         iii. Kuwa na Shauku/Msukumo wa kuyatimiza Malengo yako~ Burning desire.

Chukulia mfano wa mtu ambaye amezidiwa na maji ziwani, yanamzamisha na kutaka kumwua, jinsi mtu huyo anavyotapa tapa huku na kule ilia pate hewa ya Oxygen na pia ili asife. Hiyo ndiyo “burning desire.”  Ukiwa na Msukumo ndani yako, rafiki yangu mpendwa hakuna jambo litakalokukatisha tamaa kusonga mbele. Utakuwa kama bondia unakwepa, unakinga na kutupia ngumi (Rolling with punches) unakuwa ‘Unstoppable’. Hata zije ngurumo, radi, kiangazi ama masika, wewe bado utasonga tu mbele. Kwa hiyo natamani sana uwe na shauku/msukumo ndani yako kwanza ndipo uanze kuona mafanikio katika yale yote utakayoyapanga.

Ahsante sana kwa muda wako uliotumia kusoma hii post, ubarikiwe na Bwana.
Kwa lolote, usisite kunijulisha kwa nambari 0764793105 ambayo pia ipo Whatsapp.







0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI