Saturday, August 6, 2016



KUJIAMINI Ni uwezo wa kuwa na uthubutu juu ya mambo pasipo kuwa na hofu wala uwoga, wala kutegemea msukumo kutoka kwa ndugu, jamaa au rafiki.

Kujiamini kunaweza kujengeka ndani ya mtu kwa:

Uwamuzi Binafsi. Nadhani wewe hapo ulipo hujawahi kulazimishwa kuvuta hewa... Unavuta kwasababu umeamua kufanya hvyo na hata akitokea mtu akakwambia acha kuvuta hewa, utamshangaa sana na uhenda ukamhisi ni mchawi. Vivyo hivyo KUJIAMINI Ni Uwamuzi ambao mtu binafsi anapaswa kuamua kuishi.. Katika kila eneo la Maisha yako, amua Kujiamini. Fanya Uwamuzi binafsi kuanzia sasa.


Utendaji.

INORDER TO BE EXPERIENCED YOU HAVE TO TRY MANY THINGS AS MUCH AS YOU CAN, MEET CHALLENGES AND LEARN FROM THEN.
KUJIAMINI hujengwa kwa Kufanya jambo tena na tena, kutana na changamoto na Kujifunza kupitia hizo Changamoto.

Mtu aliyefanya mitihani mingi ya shuleni, huwa anakuwa na hali ya Kujiamini ndani yake kuliko ambaye kafanya michache au ambaye hajafanya kabisa wakiwa wanaenda kufanya Mtihani wa Taifa.
Mfano unafanya shughuli za kuuza Viatu, mwanzoni unaweza ukawa na wasiwasi Au hofu lakini kwa kadri ya muda utakavyozidi kwenda utaanza Kujiamini na hata ikitokea unahojiwa sehemu, utakuwa hauna mashaka yoyote. HUWEZI JIFUNZA KUENDESHA BAISKELI KWA KUSOMA KITABU AU KWA KUANGALIA IGOLIZO; BALI KWA KUTENDA. Anza kutenda, Kujiamini kutajengeka ndani Yako.


Jitambue:

Ukijua unakokwenda, utaweza kuchagua aina nzuri ya Usafiri wa Kutumia
... Kama ni Usafiri wa baiskeli, gari, train au ndege. Nitashangaa kukuona uko stendi ya basi unasubiria usafiri na hujui unakokwenda.
Jitaambue; unatĂ ka kufanya jambo gani kwenye Maisha.. Kwa kufanya hvyo utaumba KUJIAMINI ndani Yako.
0764793105 whatsApp
www.lacksontungaraza.blogspot.com


Mwonekano- Your Grooming.

Unaweza ukawahujaelewa hii pointi na hata kuanza kushangaa, ni kwa namna gani Mwonekano ukajenga Kujiamini ndani ya mtu… Kuwa mpole, tuwe pamoja ndugu. Mwonekano wa mtu huanzia katika Mavazi aliyovaa… ndani ya sekunde kumi za mwanzoni unapokutana na mtu kwa mara ya kwanza, aina ya Mavazi utakayokuwa umevaa ndiyo yataashiria akupokeeje.

Chukulia mfano uko sehemu umepumzika halafu anakuja mtu amevaa haya mavazi ya sahivi ya kimwendokasi… shati na suruali kama dekio, halafu anakuomba simu yako mara moja awasiliane na nduguye maana yeye ni mgeni eneo hilo na hanasimu… sidhani kama utamuamini. Licha ya kwamba Mavazi hujenga Kujiamini, humpatia pia mtu Kibali/Kukubalika machoni pa wengine.
MWONEKANO HUJENGA KUJIAMINI.[Lackson Tungaraza]

MAVAZI HULETA KIBALI MACHONI PA WATU.[Lackson Tungaraza]


Asilimia kubwa, huwezi kuvaa mavazi ambayo hayaendani na tabia yako ya sirini… ukiona mdada anavaa nguo za kumuonesha mapaja au maungo yake, basi fahamu hiyo ndiyo hali yake ya ndani moyoni na hivyo pia jamii itamtafsiri kwa mwonekano wake, wanaume watakaomchumbia watakuwa na aina yake hiyo hiyo. Sasa Mavazi yanajengaje Kujiamini!! Hii ndiyo pointi ya msingi hapa.

 Unapokuwa umevaa vizuri kiimaadili, siyo kuvaa tu ilimradi umekutana na nguo kabatini kwako… Unakuwa na uhuru wa kutembea njiani kwa Kujiamini, kusimama mbele ya watu pasipokuwa na wasiwasi…. Ndiyo maana vyuoni wakati wa ‘presentation’ wanafunzi wanaaswa kujitahidi kuvaa vizuri kimaadili, kwanini? Kujenga Kujiamini katika hatua ya kwanza. Ukivaa vinguo vimekubana makalio, hata ukiwa njiani unajishitukia kama utapigiwa mluzi na wanaume na hata kukaa kwenye kiti unajikunja kama paka aliyenyeshewa mvua na wakati vazi ni lako. Mimi binafsi [Lackson Tungaraza] huwa nahisi Kujiamini sana pale ninapovaa vyema kimaadili zaidi. Capture that!!



Ambatana na watu sahihi.

Kunamsemo usemao, ndege ambaye hanambawa akiwa katika kundi la ndege wenye mbawa, naye hujiona kuwa na uwezo wa kuruka au kupaa na hivyo humpelekea kujaribu kuruka kama wenzake. Why!! Birds of the same feathers flock together. Therefore, [associate yourself with confident people and you’ll develop a sense of confidence in yourself, and eventually you’ll begin to practice that sense of confidence to the outside world]-said Lackson Tungaraza.

Amua leo Kuifuata Ndoto yako bila kujali watu watasemaje..Inawezekana.



Lastly but not least, Neno La MUNGU

YES, Neno la MUNGU. GOD is the beginning and the end, the source and the destination.
*tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru- Yoh 8:32* Kwahiyo Neno la Mungu ambaye ndiye Mungu anakujulisha maarifa ambayo umepungukiwa ndani yako ili kujenga Kujiamini.. aliyekuumba, anafahamu udhaifu wako na nguvu yako. Kweli hiyo ni ipi sasa!!

*Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu, na ya upendo na ya moyo wa kiasi- 2Tim 1:7* Huu ndiyo ukweli wa Neno lake, uwoga hautoki kwa Mungu bali kwa shetani. Ndiyo maana YESU KRISTO anawaambia wanafunzi wake [Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum- Mathayo 10:28]… Anawajengea Kujiamini ndani yao, wasiwaogope wanadamu bali wamuogope Mungu.

Kujua kama kweli Mungu hakutuumbia roho ya Uwoga, soma hapa… “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili” –Ufunuo 21:8. Waoga hapo inamaanisha wenye roho ya uoga, hivyo Mungu hawezi akakuumbia roho ya uwoga halafu tena akuangamize… ni roho itokayo kwa shetani. Dawa yake? Mwamini YESU KRISTO na ukubariki akuongoze katika maisha yako yote na yale uyafanyayo… Mwambie ulikosea mwanzoni lakini sasa umetambua na unarudi kundini mwake. WORD OF GOD IS THE BREATHE OF LIFE

Tembelea: www.jesusisalive2016.wordpress.com kumjua MUNGU zaidi


©Lackson Tungaraza
0764793105 whatsApp
www.lacksontungaraza.blogspot.com
www.facebook.com/ltungaraza on facebook[Follow me]

Hizo ni baadhi ya njia za Kuweza KUJIAMINI. Fanyia kazi.... Kuwa Ni Kutenda. Actions speak Louder than Words.
WE ARE THE CHOSEN GENERATION [N.T.I MOVEMENT].


1 comment:

  1. Ebu tushirikishe njia nyingine ambayo huwa unatumia kujenga hali ya KUJIAMINI ndani yako .... karibu sana, tunasubiria wazo lako

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI