Monday, January 25, 2016

       MADHARA YA KUKATA TAMAA

Habari yako rafiki yangu mpendwa?
Nakupa pongezi kwa kuendelea kutafuta maarifa mbali mbali ya kuweza kubadili maisha yako katika mtazamo uliochanya, ni wengi wanatamani lakini hawachukui hatua wanabaki kulalamika kila siku. Kwahiyo mshukuru Mungu wako.

Baada ya kujifunza mambo mengi kwa habari ya namna ya  kuweka Malengo na jinsi ya kuyafanikisha na masomo mengine mengi juu ya Mafanikio katika Maisha yetu ya kila siku. Leo napenda tuangalie hili suala la kukata tamaa. Watu wengi, wanamuziki, waalimu, wanasheria, wanafunzi, mawaziri, wafanyabiashara, wanandoa, wachumba, wachungaji wameingia katika ramani ya maisha ambayo hawakuwa nayo awali kwa sababu ya kukata tamaa. Kukata tamaa ni adui namba moja aliyewapeleka wengi makaburini kabla ya wakati wao, aliyewafanya wengi waonekane ni wazee wakati bado ni vijana, aliyewafanya wengi waone kama maisha hayana maana yoyote kwao. KUKATA TAMAA NI NINI?

Kukata tamaa ni hali ya kupoteza matumaini. Hali hii hutokea pale ambapo mtu anapoteza imani juu ya matarajio yake ya sasa na ya baadae ya kupata kitu fulani alichojipangia. Kuna wanaofahamu kuwa wamekata tamaa na wengine hawafahamu kama wamekata tamaa. Kama una dalili zifuatazo, basi gundua ya kuwa umeshakata tamaa;

       i.            Kukosa msukumo wa ndani. Ili mtu yeyote yule aweze kufanikiwa anahitajika kuwa na msukumo wa ndani (burning desire), huu msukumo haupo ndani ya aliyekata tamaa.

     ii.            Kufanya Maamuzi ya haraka

  iii.            Kupoteza hamu  juu ya jambo Fulani. Inawezekana kuna jambo ulikuwa unalifanya kwa furaha na uzuri lakini ghafla unaanza kupoteza hamu juu ya jambo hilo.

  iv.            Kupoteza Ujasiri. Mwanzoni ulikuwa unatenda jambo kwa ujasiri lakini sasa ujasiri huo umepotea ghafla.

     v.            Kujihisi hufai kabisa. Unajichukulia kama mtu usiye na thamani yoyote ile hapa duniani.

  vi.            Mabadiliko ya Tabia. Kutoka tabia nzuri hadi mbaya

vii.            Kupungua kwa juhudi katika jambo ulitendalo. Mwanzoni ulikuwa unafanya kazi kwa bidii lakini sasa unajifariji ya kwamba unapumzika kidogo au utafanya baadae.

viii.            Maneno na vitendo vinavyoashiria kukata tamaa kama matumizi ya madawa ya kulevya, Ukahaba, Sidhani kama nitaweza, kujitenga n.k
          
Nadhani sasa utakuwa umejitambua kama ulikuwa umekata tamaa au la. Madhara ya kukata tamaa ni makubwa japokuwa watu wanajifariji, kama;

                          I.  Kupoteza Dira ya Maisha. Ili mwanadamu aweze kufanikiwa hapa duniani, anatakiwa kuwa na dira (maono). Lakini mtu anapokata tamaa, dira hii hupotea ghafla na hivyo kujikuta akitenda mambo ya ajabu hata kama mwanzoni alikuwa mtu mwema na mwadilifu
          
     I           II. Kutokufikia Malengo yako ndani ya Wakati. Katika video iliyopita nilielezea juu ya sifa mojawapo ya Malengo, lazima yawe na muda maalumu; kama ni wiki, mwezi, mwaka au zaidi ya hapo. Hivyo mtu anapokata tamaa, Malengo hayo huwekwa pembeni kwanza na kusababisha upotevu wa muda uliopangwa
         
              III.   Kufanya Maamuzi ya Haraka. Kama mtu alikuwa mtumishi wa Mungu, basi anajiingiza katika masuala ya Uzinzi, matumizi ya madawa ya kulevya. Mwanafunzi aliyefeli kujiua, Wanandoa kupeana taraka, Wanawake kutoa Mimba n.k pasipo kufikiria kwanza.

              IV. Jamii na Taifa kukoswa Maendeleo. Waziri, Mzazi anapokata tamaa, basi hawezi kuleta maendeleo yoyote kwa sababu ameshajiona yeye siyo wa thamani na hata hatokuwepo, kwa nia ya kujiua .


         KUMBUKA MAMBO YAFUATAYO IKIWA UNATAKA KUKATA TAMAA;



HAMNA MWENYE UWEZO WA KUZUIA NDOTO YAKO IKIWA HUJAWAPA NAFASI YA KUITAWALA, SONGA MBELE SIKU ZOTE, 
USIKATE TAMAA, 
MAMBO MAZURI ZAIDI YANAKUJA MBELENI.


Nakushukuru sana kwa muda uliyotoa kusoma Makala hii ya leo, Unaweza changia lolote lile ambalo unaona kwa upande wako litasaidia jamii yetu kusonga mbele. Pia kumbuka kuSHARE ili kuwafikia ndugu na rafiki zetu wengi. Ubarikiwe na Bwana.

Ni Mimi Rafiki Yako Mpendwa,
Lakson Tungaraza.

0764793105 (whatsapp/piga simu)




1 comment:

  1. Ukizijua principles za maisha, hutopata shida...usikate tamaa.
    Toa maoni yako hapa

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI