Thursday, June 23, 2016

LACKSON TUNGARAZA KATIKA HARAKATI ZAKE ZA KUTOA HUDUMA YA VIATU

Tunashindwa kuongeza vipato vyetu kwa sababu  biashara zetu hazina mvuto

Tunapoendelea kufungua vyanzo vingine vya vipato kwa kutumia mbinu zile zile, tunaendelea kufeli zaidi na hata kukata tamaa kwa sababu ya kukosa wateja kwa kile tunachokifanya


Hivyo badala ya kukimbilia mikopo kwa ajili ya kuanzisha biashara nyingine, ni bora tukajifunza mbinu za kuifanya biashara yako kuwa ya tofauti na Mvuto Mkubwa kwa Wateja

Biashara inapokuwa na Mvuto na Utofauti ni rahisi sana kupata Wateja na pato lako kuongezeka


Zifuatazo ni mbinu utakazotumia ili uwe na Biashara yenye Mvuto na Utofauti Mkubwa dhidi ya Biashara zingine;


     Mbinu Ya Kwanza

      Bei Ya Bidhaa/Huduma Yako Imvutie Mteja

Biashara huanzishwa kwa lengo la kutatua changamoto zilizopo katika jamii, zinaweza zikawa ni ukosefu wa bidhaa au huduma Fulani

Endapo atatokea mtu wa kutatua changamoto hizo, basi Wateja wapo tayari kumpa fedha zao kupata hizo Huduma au Bidhaa

Tatizo linakuja kwenye upangaji wa bei ya Huduma au Bidhaa, na usipolizingatia hili litaangamiza biashara yako kwa kufukuza Wateja

Bei yako isiwe ya ghali ili uweze kuwashawishi watu kuinunua, Usitake faida kubwa au Mafanikio ya mara moja. Wengine husema, “Kulala masikini na Kuamka Tajiri”
Inawezekana Huduma Yako Ikahitajika mahali Fulani, lakini kwa sababu umetanguliza pesa mbele zaidi kuliko Utu au Huduma yako, Utakuwa umekatisha watu tamaa ya kuwa Wateja wako na hutofanikiwa


             Mbinu Ya Pili

             Ubora Wa Huduma/Bidhaa Yako

Wahenga walisema, “Kizuri Chajiuza Na Kibaya Chajitembeza”. Ubora wa Bidhaa/Huduma yako ni jambo la muhimu sana ili kuvutia Wateja

Wateja wanapenda Bidhaa/Huduma ambazo zitawatatulia matatizo yako moja kwa moja bila kuathiri hali zao za kiafya


Bidhaa zako zikiwa na Ubora, zitawavutia watu wengi kwako na utashangaa kuona mauzo yako yakipanda

Ukifanya tofauti na hapo, itabaki historia ya kwamba ulikuwa na Wateja Fulani. Hivyo usiwauzie watu bidhaa feki au zilizopoteza Ubora wake (zilizo expire)

Usijaze bidhaa ambazo sio bora, ni afadhali uwe nazo chache lakini ni bora zaidi.


       Mbinu Ya Tatu

       Muoneshe Mteja au Mpenzi Wa Huduma Yako Kuwa Unamjali

Wanataaluma wengi hupenda kusema, “Kama hauna tabasamu usoni mwako ni vyema usifungue biashara”.

Mtu yeyote Yule anapenda kuonekana wa muhimu na wa thamani zaidi, wengine wanatafuta nafasi hiyo kupitia vyombo vya habari kama TV, redio, Magazeti n.k.


Hii tabia ipo pia ndani ya Wateja, wanapenda kupokelewa kwa tabasamu na uchangamfu mkubwa wanapofika sehemu ya uhitaji wa bidhaa/huduma

Ukifanya hivyo atatamani kuja kwako kila mara, maana wengine huko wanakotoka hawana faraja wala furaha

Zingatia mbinu hii na utaona Wateja wakimiminika kwako zaidi kuliko kwa jirani yako.


           Mbinu Ya Nne

       Usijali Muda Wako Tu, Jali Na Kuthamini Muda Wa Mtu Mwingine Pia

Wazungu wanasema ya kwamba, “Time Is Money”. Kwetu sisi Wabongo, tunaona muda kama ni kitu cha kawaida sana kana kwamba hakiwezi kuleta athari zozote katika maisha yetu na ya wale wanaotuzunguka

Unakuta Mteja anafika dukani kwa mtu, anabisha hodi hadi anachoka, au anamtajia mahitaji yake mwenye duka lakini yeye anakomaa tu na kuchati au kupiga soga


Mteja endapo utamwona bado anakuja kwako, ni kwa sababu hajapata tu sehemu nyingine ya kwenda kupata hiyo huduma/bidhaa. Ikitokea mtu mwingine akaja mwenye kukidhi haja ya moyo wake na kujali muda wake kwa kumsikiliza kwa umakini, huyo Mteja hatorudi tena kwako

Tumia vizuri kwa umakini nafasi ambayo Mteja amekupatia ili apate huduma/bidhaa kutoka kwako.

Mbinu Ya Tano

Tangaza Huduma/Bidhaa Yako

Hamna mwenye alama kichwani ambaye akikutana tu na watu, wanatambua yeye anafanya biashara gani na yuko sehemu gani. Labda tu kama amebeba bango au bidhaa Fulani ambayo ndiyo itakayo mtambulisha

Biashara ni Matangazo na Matangazo ni Biashara.


Matangazo ni gharama lakini tunatumia shilingi kupata shilingi. Lakini usitangaze Huduma ambayo huwezi kuitoa kwa kiwango hicho ulichoahidi, utapoteza Wateja wengi

Tumia njia mbalimbali katika kutangaza bidhaa au huduma yako, unaweza tumia Redio, TV, Magazeti, Mabango,Vipeperushi, Mitandao ya kijamii kama Facebook ambayo inawatumiaji wengi sana duniani na wanazidi kuongezeka kila leo, Twitter, Instagram n.k.


        Fanya Zoezi Hili Fupi

Nakushukuru kwa kusoma Mbinu hizi za kuifanya biashara yako iwe ya tofauti na Yenye Mvuto mkubwa mpaka hatua hii, Ninaamini kabisa una lengo la kubadilisha biashara yako kwenda hatua nyingine. Malizia kwa kufanya zoezi hili fupi;

# Chunguza kwa Umakini kama bidhaa ulizonazo zina ubora sahihi wa kumvutia Mteja. Pia chunguza kwa umakini bidhaa unazonunua kwenye maduka ya jumla, zingine ni feki au zimeshapitiliza muda wa matumizi

# Chunguza kama Bei zako zinaendana na Uchumi wa Wateja wako waliopo katika hilo eneo. Lakini zingatia ya kwamba Ubora wa bidhaa huendana na bei, zenye Ubora mkubwa zina bei kubwa pia


# Je, unamjali Mteja wako na kuthamini muda wake pia?

# Je, unafanya Matangazo ya kutosha kwa bidhaa au huduma ulizonazo?

Kwa Ushauri na Mafunzo yanayohusu kufanya biashara yako kuwa ya tofauti na Mvuto mkubwa, Wasiliana na Ndugu Lackson Tungaraza, +255764793105 au tembelea Website ya lacksontungaraza.blogspot.com

Pia unaweza kupata Nakala ya Kitabu Cha “MBINU ZA KUONGEZA MAUZO KWENYE BIASHARA YAKO,” Kikiwa ni Mwendelezo wa somo hili kama Sehemu Ya Pili Kwa Gharama Nafuu Kabisa. Bila Kusoma Kitabu Hiki Cha Mwendelezo, Biashara Yako bado itakuwa yenye Kuingiza Kipato Kidogo na Cha Kawaida.. Kipo katika softcopy kukuwezesha kukisoma katika simu yako au kompyuta mahali popote pale ulipo   bila kusumbuka kubeba kitabu mkononi mwako.

     07647931059(sms/wasap) [Lackson Tungaraza

PATA KITABU HIKI KWA GHARAMA NAFUU: 5000/- TU.
PUNGUZO HILI LA BEI NI LA MUDA MFUPI TU, HIVYO WAHI MAPEMA.



1 comment:

  1. Wahi sasa, muda wa punguzo la bei umekaribia kufika mwisho.
    0764793105 [Lackson Tungaraza].

    Nini maoni yako juu ya masomo ninayofundisha hapa?

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI