Monday, May 6, 2019


Hivi hicho Unachokifanya Sasa Ukiwa peke Yako au ukiwa na mtu mwingine, kama Kesho utakikuta kwenye magazeti Yote ya Mitaani na Mitandaoni, JE UTAKIFURAHIA? JE NDUGU ZAKO WATAENDELEA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUWA DAMU MOJA NAWE? JE WAZAZI WAKO WATAKUWA TAYARI KUJISIFIWA YA KWAMBA WEWE NI MTOTO WAO? JE JAMII ITAKUWEKA KWENYE KUMBU KUMBU ZA WATU WALIYOISAIDIA KUSONGA MBELE KIMAENDELEO? JE WATOTO WAKO WATAKIFURAHIA NA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUWA NA MAMA au BABA KAMA WEWE? JE LITAMFURAHISHA MUNGU WA MBINGUNI?

Ikiwa unachokifanya Unaona kitakuaibisha kikiwekwa kwenye Magazeti ya kesho au kwenye Vyombo vyote vya Habari Nchini, basi ACHA KABISA KUKIFANYA. ANZA KUFANYA MAMBO MEMA HATA UKIWA MAHALI AMBAPO HAKUNA ANAYEKUONA au ANAYEKUJUA. Haijalishi Uko Gesti, Hotelini, Hosteli za Chuoni, Geto, Kichakani, Porini, Shambani, Sokoni, au pengine pale - SIKU ZOTE JIULIZE HAYA MAMBO KABLA YA KUTENDA JAMBO LO LOTE LILE.

Haya yote yanawezekana, hakuna lisilowezekana. Uwezekano unaanzia kwenye Nia, na Uzuri ni kwamba "Penye NIA pana NJIA."

AMUA LEO KUWA WA TOFAUTI.
#LD-LAMAX DESIGNS tunakutakia Mabadiliko Chanya kwenye Maisha Yako Yote.

"HISTORIA YAKO INAANDIKWA NA WEWE MWENYEWE. WENGINE WATAKUJA TU KUISOMA HADHARANI."

#Mawasiliano: +255 (0) 764 793 105
#Email: lamaxdesigs@gmail.com
#Sponsor: @LACKSONTUNGARAZA

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI