Monday, May 6, 2019


Leo ukimwuliza Mtoto wa Darasa la Kwanza 1-5 (Moja kutoa Tano) ni Sawa sawa na ngapi, atakwambia haiwezekani, ni Lazima pawepo mahali pa kukopa. Lakini ukimwuliza hilo hilo Swali aliye Darasa la Tano atakwambia ni Sawa sawa na -4 (hasi Nne). Wanafunzi ni wale wale lakini Majibu tofauti. Na Kila Mmoja yuko Sahihi kulingana na kiwango cha Maarifa alichonacho kwa wakati huo.

Ni jambo gani ninalotaka ujifunze kupitia huo mfamo wa hapo Juu? Sikiliza, kwenye maisha yako Yote ya hapa Duniani, usitegemee ya kwamba kuna Siku Watu wote watakuwa na Mtazamo kama wako, Akili kama zako, wala kiwango cha Maarifa kama ulichonacho. Never. Unaweza Ukaandika, ukasema,  au ukatenda Jambo ambalo ni Sahihi lakini Ukapingwa sana kana kwamba hauko Sahihi, na waliokupinga ndiyo wako Sahihi. Hiyo isikutishe sana. Inawezekana Wameamua kupinga kwa Sababu ndiyo kazi inayowaweka Mjini (Siku zote wapo kwenye kambi ya Upinzani kwa Kila Jambo), au hawajui walitendalo kwa Sababu ya Kiwango cha Maarifa na aina ya Usahihi walionao, au hawataki Ukweli ujulikane  (wanataka Watu Wengi waendelee kutembea gizani katika upofu, na wao wanufaike zaidi).

Kumbuka ya kwamba, kupingwa kwa Jambo Sahihi hakuondoi Usahihi wa hilo Jambo hata kama waliyolipinga watashinda.

Aiseeeh! Songa mbele, wasikutishie nyau. Unajua hata waliyokuwa wanapinga ujio wa Simu Janja  (Smartphone) kwa kusema ya kwamba ni za Freemason na zinanyonya Damu za Watu za Mikononi, ndiyo WANAOONGOZA Leo kwa kutumia hizo Simu. Kupingwa Sio kuzuiliwa. Yesu alipingwa ya kwamba Sio Mwana Pekee wa Mungu Ingawa Ishara zote zilionesha ndiye. Hata hivyo kupinga Kwao hakukuondoa Ukweli kwamba Yeye ndiye Mwana wa Mungu aliye hai. John Magufuli alipingwa sana wakati wa kampeni za Uchaguzi mwaka 2015 wakisema ya kwamba hawezi kuwa Rais wa Nchi kwa Sababu alifanya Makosa ABC alipokuwa Waziri. Kwani kupinga kwao kulimfanya asiwe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Hahahaha, Jibu unalo.

"Ukishindwa kusonga Mbele kwa Sababu ya kupingwa, basi Ujue ya kwamba Ulikuwa Hujui ulitendalo hata kabla ya kuanza kulitenda ulitendalo Leo." - LAMAX.


AMUA LEO KUWA WA TOFAUTI. Kuwa Yule unayetakiwa kuwa. Usiwe Yule anayetakiwa Kuwa kwa Sababu ya matakwa ya Watu fulani fulani.

Tukutane baadae.
By Lackson Tungaraza (Mwandishi wa Vitabu Kadhaa ambavyo Unaweza ukavipata Leo na ukaweza kunoa Uwezo uliyomo ndani Yako).

@LACKSONTUNGARAZA
#0764793105 WhatsApp.
https://lacksontungaraza.blogspot.com
#LamaxQuotes #LIVING4MANY #LamaxLibrary

Related Posts:

  • NAMNA AMBAVYO WATU WENGI NI WAFUNGWAWatu wengi hawataki kuwa huru kabisa.  Watu wengi hawataki kuachana na UTUMWA. Wakiambiwa, hawaamini, na Kudhani ya kwamba wanafatiliwa maisha yao. Kati ya mambo yaliyomtia hamasa Mwalimu  Nyerere kuacha Ualim… Read More
  • KWAKO KIPENZI CHANGUNinayaandika haya nikiwa na majuto makubwa sana ndani yangu, kiasi cha Kuona ya kwamba dunia nzima inafahamu historia yangu. Sikutaka kuyaandika haya, ila sipendi uendelee kuteseka kwa sababu yangu. Licha ya kwamba kwa sas… Read More
  • JE UNAOGOPA KUPINGWA? Leo ukimwuliza Mtoto wa Darasa la Kwanza 1-5 (Moja kutoa Tano) ni Sawa sawa na ngapi, atakwambia haiwezekani, ni Lazima pawepo mahali pa kukopa. Lakini ukimwuliza hilo hilo Swali aliye Darasa la Tano atakwambia ni Sawa sawa… Read More
  • NGOSWE SIO DIWANI, USEME KURA KAZIKIMBIA. Hodi Hodi Uwanjani, Lamax Naingia, Nimetoka Darasani, Mkononi na wangu Dia, Nyumbani kwetu Msasani, Mbagala pa Kuzugia, Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia. Watoto sikilizeni, Vijana nanyi pia, Shuleni sio Ukwen… Read More
  • HATA WANADAMU WAKIKUSAHAU, MUNGU BADO ANAKUKUMBUKA Daudi kuwa porini na kuchunga kondoo kwa muda mrefu SI KWAMBA MUNGU ALIMWACHA AU ALIMSAHAU, maana ndugu zake hawakumhesabia thamani, mzee Yese alimtoa mawazoni mwake, hata anapo ambiwa alete watoto wake mbele ya nabii SAM… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI