Monday, May 6, 2019


Leo ukimwuliza Mtoto wa Darasa la Kwanza 1-5 (Moja kutoa Tano) ni Sawa sawa na ngapi, atakwambia haiwezekani, ni Lazima pawepo mahali pa kukopa. Lakini ukimwuliza hilo hilo Swali aliye Darasa la Tano atakwambia ni Sawa sawa na -4 (hasi Nne). Wanafunzi ni wale wale lakini Majibu tofauti. Na Kila Mmoja yuko Sahihi kulingana na kiwango cha Maarifa alichonacho kwa wakati huo.

Ni jambo gani ninalotaka ujifunze kupitia huo mfamo wa hapo Juu? Sikiliza, kwenye maisha yako Yote ya hapa Duniani, usitegemee ya kwamba kuna Siku Watu wote watakuwa na Mtazamo kama wako, Akili kama zako, wala kiwango cha Maarifa kama ulichonacho. Never. Unaweza Ukaandika, ukasema,  au ukatenda Jambo ambalo ni Sahihi lakini Ukapingwa sana kana kwamba hauko Sahihi, na waliokupinga ndiyo wako Sahihi. Hiyo isikutishe sana. Inawezekana Wameamua kupinga kwa Sababu ndiyo kazi inayowaweka Mjini (Siku zote wapo kwenye kambi ya Upinzani kwa Kila Jambo), au hawajui walitendalo kwa Sababu ya Kiwango cha Maarifa na aina ya Usahihi walionao, au hawataki Ukweli ujulikane  (wanataka Watu Wengi waendelee kutembea gizani katika upofu, na wao wanufaike zaidi).

Kumbuka ya kwamba, kupingwa kwa Jambo Sahihi hakuondoi Usahihi wa hilo Jambo hata kama waliyolipinga watashinda.

Aiseeeh! Songa mbele, wasikutishie nyau. Unajua hata waliyokuwa wanapinga ujio wa Simu Janja  (Smartphone) kwa kusema ya kwamba ni za Freemason na zinanyonya Damu za Watu za Mikononi, ndiyo WANAOONGOZA Leo kwa kutumia hizo Simu. Kupingwa Sio kuzuiliwa. Yesu alipingwa ya kwamba Sio Mwana Pekee wa Mungu Ingawa Ishara zote zilionesha ndiye. Hata hivyo kupinga Kwao hakukuondoa Ukweli kwamba Yeye ndiye Mwana wa Mungu aliye hai. John Magufuli alipingwa sana wakati wa kampeni za Uchaguzi mwaka 2015 wakisema ya kwamba hawezi kuwa Rais wa Nchi kwa Sababu alifanya Makosa ABC alipokuwa Waziri. Kwani kupinga kwao kulimfanya asiwe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Hahahaha, Jibu unalo.

"Ukishindwa kusonga Mbele kwa Sababu ya kupingwa, basi Ujue ya kwamba Ulikuwa Hujui ulitendalo hata kabla ya kuanza kulitenda ulitendalo Leo." - LAMAX.


AMUA LEO KUWA WA TOFAUTI. Kuwa Yule unayetakiwa kuwa. Usiwe Yule anayetakiwa Kuwa kwa Sababu ya matakwa ya Watu fulani fulani.

Tukutane baadae.
By Lackson Tungaraza (Mwandishi wa Vitabu Kadhaa ambavyo Unaweza ukavipata Leo na ukaweza kunoa Uwezo uliyomo ndani Yako).

@LACKSONTUNGARAZA
#0764793105 WhatsApp.
https://lacksontungaraza.blogspot.com
#LamaxQuotes #LIVING4MANY #LamaxLibrary

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI