Saturday, March 16, 2019

Watu Wengi huwa Wananunua Vifurushi vya Intaneti Ili Waelimike Mtandaoni, Lakini huwa hawafikii hayo Malengo Yao.

- Unakuta Mtu anaingia YouTube ili apate Elimu ya kumsaidia Kukua Kiroho au Kiuchumi, lakini anaishia kuangalia Comedy  (Vichekesho), Mieleka ya WWE, Video za Ngono  (Pornography), Udaku, Series, Taarifa ya Habari, N.k.



- KIFURUSHI KINAPOISHA, au kinapokaribia kuisha, ndipo Wanakumbuka walichokuwa wanataka Kujifunza. Na tabia hiyo hujirudia tena na tena baada ya Kununua Vifurushi vingine vya Intaneti. Nami Lackson Tungaraza nilikuwa Vivyo hivyo hapo Awali.


UNAJUA SHIDA NI NINI??

- SHIDA ni kwamba hawajui kwa Kina wanachotaka Kujifunza, kwa nini wanataka Kujifunza hicho wanachotaka Kujifunza  (Nia na Sababu ya kujifunza), na kutokuwa na Nidhamu binafsi (Self-Discipline) ya Kujiongoza.

Inawezekana kabisa nawe unayesoma huu ujumbe ni Muhanga  (Victim) wa hilo, Usihofu Ikiwa utaamua Kubadilika kuanzia Sasa. Sasa FANYA YAFUATAYO KABLA YA KUINGIA FACEBOOK, INSTAGRAM, YOUTUBE, N.K;

(I) Fahamu Unataka Kujifunza nini na kwa Nani (Mtu anayefundisha Unachokitaka, au Kama ni Page au Channel ya YouTube).

(II) Fahamu ni KWA NINI Unataka Kujifunza  (Nia na Sababu Yako ya Kujifunza).

(III) ANDIKA Mahali Yale Yote Unayotaka Kujifunza YouTube. Mfano!
- Jinsi ya Kutengeneza Sabini ya Unga.
- Faida za Nyama tamu ya Sungura. N.k.

(IV) Ingia Mtandaoni na kuanza kutekeleza hatua hiyo ya (III) hapo Juu. Ikiwa na maana ya kwamba UWE NA NIDHAMU BINAFSI YA KUJISIMAMIA, KUJIZUIA USIANGALIE au USIFANYE AMBAYO HUKUPANGA, na Kuweza KUJIONGOZA  (Leading Yourself).
Kumbuka kutumia "SEARCH BUTTON" (Kitufe cha Kutafutia unachokitaka) Kupata Yale uliyopanga Kujifunza YouTube.

(V) Ondoka Mtandaoni UKAFANYIE KAZI ULICHOJIFUNZA au ULICHOPAKUA MTANDAONI  (What you Downloaded from the Internet).


KWA KUFANYA HIVYO;

(I) Utakuwa unaokoa muda wako mwingi (Time saving).

(II)  Utakuwa unatumia vyema Vifurushi vya Intaneti kama ulivyokusudia. Na Pia

(III) Utakuwa Mbali na mambo yasiyokuhusu ambayo yangekupotezea Muda Wako na Kuharibu Tabia Yako njema - kwa Sababu Mazungumzo mabaya na Marafiki Wabaya huaribu tabia Njema.


Naamini Utakuwa umejifunza Jambo la Kukusaidia unapokuwa Mtandaoni. Usisahau kutendea kazi na Kushea hili Somo Zuri sana kwa Rafiki zako waliyopo Facebook, Messenger, Instagram, WhatsApp, Twitter, n.k. Uwe na Siku njema sana. Ni Mimi Rafiki Yako Lackson Tungaraza  (Lamax).

AMUA LEO KUWA WA TOFAUTI.
@LACKSONTUNGARAZA
0764793105 - WhatsApp

Related Posts:

  • BADO UNAENDELEA KUVUNJA LAANA ZA UMASKINI? Tangu Uanze kuvunja Laana za UMASKINI, huu ni Mwaka wa ngapi, na Je Umeshaanza kuwa TAJIRI? Kabla ya Kuanza au Kuendelea tena na Uvunjaji Wako wa Laana za UMASKINI, Tathimini Kwanza ni kwa Jinsi Umejitoa Kulipa Gharama … Read More
  • LIVING FOR MANY ONLINE SEMINAR - SEMINA BOMBA YA KIUCHUMIMwenye hekima mmoja alisema ya kwamba,  “sababu ya msingi inayowafanya watu wafeli kwenye maisha ni kutoweka Mipango mipya ya kuwaondoa kwenye Mipango ile ya awali iliyowakwamisha.” Naamini kuna mipango kadhaa uliyop… Read More
  • HATUA ZA MAFANIKIO "MAFANIKIO hayaji kwa Ukubwa au Udogo wa kile Ulichonacho, bali kwa namna Unavyotumia kile Ulichonacho" ~Lamax Kila siku nikikumbuka Hatua nilizopitia Kufika hapa nilipo Leo Kimaisha, ninapata hamasa ya Kumshukuru Mungu k… Read More
  • WAKE UP NOW, TOMORROW IS NOT YOURS!! Ndugu zangu maisha ni kusonga mbele, usikubali kusimama kwa lolote!.. Anza kutambaa, tembea, kimbia na ikiwezekana paa lakini usikubali kusimama..moja ya usafiri wako ni kutumia fursa zinazopita mbele yako.Ni Mara ngapi… Read More
  • FIND_SOMETHING_TO_DIE_FOR_THAN_TO_LIVE_FOR FANYA JAMBO la Kumfanya MUNGU azidi Kuona  Umuhimu wa Kukuacha Uendelee kuwa HAI hapa duniani. JAMBO la Kumfanya MUNGU aone KUNA PENGO wakati  wa Kuugua Kwako (Kupatwa na Magonjwa) ili AKUPONYE HARAKA URUDI… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI