Saturday, March 16, 2019


Hodi Hodi Uwanjani, Lamax Naingia,
Nimetoka Darasani, Mkononi na wangu Dia,
Nyumbani kwetu Msasani, Mbagala pa Kuzugia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Watoto sikilizeni, Vijana nanyi pia,
Shuleni sio Ukweni, Useme Mke Utampitia,
Shuleni sio Ufukweni, Vimini Kutuvalia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia..

Notes zisomeni, Review na Google pia,
Uzembe Uacheni, Jengeni yenu Tabia,
Dunia Imesheheni, Vitabu na nyingi Bia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Ushauri Nawapeni, Bure bila Kulipia,
Shuleni sio Baani, Mapenzi Kuyazamia,
Maisha hayana Utani, Kufeli Kutawajia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Vijiweni Ondokeni, Hukumu Imekaribia,
Rudini Ibadani, Mungu Atawakumbatia,
Shetani yuko Njiani, Viburi Kuwapatia,
Mapenzi Yaacheni, Tamaa ni Dhambi pia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Waalimu wako Darasani, Mazuri kukupatia,
Njoo na Yako Wani, Zawadi Kujitwalia
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

SHAIRI hili la ‘NGOSWE SIO DIWANI’ limeletwa kwenu na LACKSON TUNGARAZA kwa Udhamini wa LAMAX QUOTES na Kitabu cha ‘SITARUDI NYUMA TENA’

@LACKSONTUNGARAZA


Related Posts:

  • HATA WANADAMU WAKIKUSAHAU, MUNGU BADO ANAKUKUMBUKA Daudi kuwa porini na kuchunga kondoo kwa muda mrefu SI KWAMBA MUNGU ALIMWACHA AU ALIMSAHAU, maana ndugu zake hawakumhesabia thamani, mzee Yese alimtoa mawazoni mwake, hata anapo ambiwa alete watoto wake mbele ya nabii SAM… Read More
  • JE UNAOGOPA KUPINGWA? Leo ukimwuliza Mtoto wa Darasa la Kwanza 1-5 (Moja kutoa Tano) ni Sawa sawa na ngapi, atakwambia haiwezekani, ni Lazima pawepo mahali pa kukopa. Lakini ukimwuliza hilo hilo Swali aliye Darasa la Tano atakwambia ni Sawa sawa… Read More
  • NGOSWE SIO DIWANI, USEME KURA KAZIKIMBIA. Hodi Hodi Uwanjani, Lamax Naingia, Nimetoka Darasani, Mkononi na wangu Dia, Nyumbani kwetu Msasani, Mbagala pa Kuzugia, Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia. Watoto sikilizeni, Vijana nanyi pia, Shuleni sio Ukwen… Read More
  • KWAKO KIPENZI CHANGUNinayaandika haya nikiwa na majuto makubwa sana ndani yangu, kiasi cha Kuona ya kwamba dunia nzima inafahamu historia yangu. Sikutaka kuyaandika haya, ila sipendi uendelee kuteseka kwa sababu yangu. Licha ya kwamba kwa sas… Read More
  • NAMNA AMBAVYO WATU WENGI NI WAFUNGWAWatu wengi hawataki kuwa huru kabisa.  Watu wengi hawataki kuachana na UTUMWA. Wakiambiwa, hawaamini, na Kudhani ya kwamba wanafatiliwa maisha yao. Kati ya mambo yaliyomtia hamasa Mwalimu  Nyerere kuacha Ualim… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI