Saturday, March 16, 2019


Hodi Hodi Uwanjani, Lamax Naingia,
Nimetoka Darasani, Mkononi na wangu Dia,
Nyumbani kwetu Msasani, Mbagala pa Kuzugia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Watoto sikilizeni, Vijana nanyi pia,
Shuleni sio Ukweni, Useme Mke Utampitia,
Shuleni sio Ufukweni, Vimini Kutuvalia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia..

Notes zisomeni, Review na Google pia,
Uzembe Uacheni, Jengeni yenu Tabia,
Dunia Imesheheni, Vitabu na nyingi Bia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Ushauri Nawapeni, Bure bila Kulipia,
Shuleni sio Baani, Mapenzi Kuyazamia,
Maisha hayana Utani, Kufeli Kutawajia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Vijiweni Ondokeni, Hukumu Imekaribia,
Rudini Ibadani, Mungu Atawakumbatia,
Shetani yuko Njiani, Viburi Kuwapatia,
Mapenzi Yaacheni, Tamaa ni Dhambi pia,
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

Waalimu wako Darasani, Mazuri kukupatia,
Njoo na Yako Wani, Zawadi Kujitwalia
Ngoswe sio Diwani, Useme Kura Kazikimbia.

SHAIRI hili la ‘NGOSWE SIO DIWANI’ limeletwa kwenu na LACKSON TUNGARAZA kwa Udhamini wa LAMAX QUOTES na Kitabu cha ‘SITARUDI NYUMA TENA’

@LACKSONTUNGARAZA


Related Posts:

  • WHY ONLINE SEMINARS? UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tel… Read More
  • ANDIKA JINA LAKO VIZURI Heri Kuchagua Jina jema kuliko Mali nyingi [smart phones, kompyuta, iPhone, iPad, gari, nyumba, nguo, shamba, ng'ombe]; Na Neema kuliko fedha na dhahabu.. Mith 22:1 Watu wengi sana hawajali juu ya majina wanayojiita au … Read More
  • JICHUNGUZE, JITATHMINI, JITAMBUE. Karibu sana rafiki yangu mpendwa katika mfululizo wa masomo yangu kwa njia ya mtandao. Wakati uliyopita, nilifundisha juu ya MTAJI KWA KIJANA NI UPI!! Maana neno MTAJI limekuwa maarufu sana kwetu vijana hasa katika karne h… Read More
  • MAMBO MATATU MUHIMU YA KUFANYA KIJANA KABLA YA KUANZA KUTAFUTA PESA YA KUFANYA BIASHARA Kijana mwenzangu kabla hujaanza kusumbuka kutafuta pesa kila mahala kwaajili ya biashara.  Kwanza Fanya maamuzi ni biashara gani unayohitaji kufanya, hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Kwanini ufanye uwamuzi kwanza? Ili k… Read More
  • WHAT DO YOU WANT TO BE REMEMBERED FOR?  Kwa kawaida kila mtu huwa anatamani na anapenda ya kwamba akitenda jambo, baadae Akumbukwe kwalo. Ikiwezekana hata watu kadhaa watoe shuhuda za jambo hilo. This a human character. Unataka kukumbukwa kwa lipi… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI