Monday, March 4, 2019


Mwalimu Emmanuel Makwaya aliwahi kusema ya kwamba, "HUNUNUI KITABU CHANGU KUNIPA MIMI FAIDA, BALI KUUPA UFAHAMU WAKO FAIDA"

Kuna Watanzania Wengi Leo ambao hudhani Kununua Vitabu ni Kuwatajirisha Waandishi wa Vitabu. Utawasikia wakisema, NGOJA TUKUUNGE KWENYE KITABU CHAKO HIKI!

Laiti kama Waandishi wa Vitabu wangekuwa wanaandika kwa Lengo la biashara, wasingekuwa Wanaviuza kwa Gharama ndogo za Tsh. 5000/= au Tsh. 10,000/=


-Waandishi wengi wa Vitabu Wanatoa HUDUMA kwenye Jamii, Sio kufanya BIASHARA.
Ingekuwa ni kwa Lengo la biashara; Vitabu vingekuwa vinauzwa hadi laki nane au Milioni Nne. Kwa Sababu wangekuwa wanakokotoa kwanza FAIDA ambazo Wasomaji wanaenda kuzalisha kupitia hivyo Vitabu - Results produced by the Book Content.

Fikiria! Kuna Waandishi ambao Wameandika VITABU vya Kukuza Biashara, Ufugaji wa Samaki au Sungura... Na kuviuza kwa Gharama ndogo ya Tsh. 10,000/= halafu Wewe Unaenda kuzalisha zaidi ya Milioni kupitia hivyo Vitabu.

Kwa maisha ya Sasa, Tsh. 5000/= au Tsh. 10,000/= inaweza Kununua Nguo Moja au Mbili za ndani kulingana na Jinsia au Mwuzaji, na baada ya Mwezi mmoja Huchakaa sana na kutupwa. Lakini KITABU cha Gharama hiyo hiyo ni HAZINA YA KUDUMU Kwako, kwa Wajukuu na kwa Uzao wako Wote KUTEGEMEANA NA UTUNZAJI WAKO.

□ Kwa hiyo, kuanzia Leo Usinunue Kitabu cha Lackson Tungaraza, Joel Nanauka, Pastor Raphael Lyela, Shemeji Melayeki, na Wengine Wengi kwa dhana ya KUWAUNGA- KUWASAIDIA WAO.


....KUNUNUA KITABU NI KUJISAIDIA WEWE MWENYEWE KABLA YA KUMSAIDIA MWANDISHI HUSIKA.

.... KUNUNUA KITABU NI KUJITAJIRISHA WEWE KWANZA, na Sio KUMTAJIRISHA MWANDISHI.

Acha Fikra Potofu, "Nikinunua Kitabu cha Lackson Tungaraza Nitamtajirisha, na Mimi nitabaki kuwa Maskini."

- Fikra Potofu Ndio Umaskini Wako wa Kwanza, Ukifuatiwa na Hofu ya Mabadiliko na Uthubutu.

TANZANIA BILA FIKRA POTOFU INAWEZEKANA!


Related Posts:

  • MY HAPPY BIRTHDAY MESSAGE TO YOUUsisubiri hadi Uzeeke, ndipo uanze kupata hamasa ya kutimiza ndoto... Rasilimali kubwa uliyonayo sasa ni Kwamba wewe ni kijana, unanguvu nyingi, afya njema. Usitumie nguvu zako vibaya katika kufanya mapenzi kiholela... Kadri … Read More
  • FIND_SOMETHING_TO_DIE_FOR_THAN_TO_LIVE_FOR FANYA JAMBO la Kumfanya MUNGU azidi Kuona  Umuhimu wa Kukuacha Uendelee kuwa HAI hapa duniani. JAMBO la Kumfanya MUNGU aone KUNA PENGO wakati  wa Kuugua Kwako (Kupatwa na Magonjwa) ili AKUPONYE HARAKA URUDI… Read More
  • NJIA MPYA YA KUTENGENEZA KIPATO CHA ZIADAHaijalishi una Kazi ama hauna Kazi, kikubwa ni UTAYARI wako pamoja na Kiasi kidogo cha #PESA kuanzia Tsh.4000/= Sasa Unaweza Kutengeneza Kipato cha Ziada (PESA) kupitia Kitabu changu "SITARUDI NYUMA TENA" - Sitaki KUFANIKI… Read More
  • NAMNA AMBAVYO WATU WENGI NI WAFUNGWAWatu wengi hawataki kuwa huru kabisa.  Watu wengi hawataki kuachana na UTUMWA. Wakiambiwa, hawaamini, na Kudhani ya kwamba wanafatiliwa maisha yao. Kati ya mambo yaliyomtia hamasa Mwalimu  Nyerere kuacha Ualim… Read More
  • KWAKO KIPENZI CHANGUNinayaandika haya nikiwa na majuto makubwa sana ndani yangu, kiasi cha Kuona ya kwamba dunia nzima inafahamu historia yangu. Sikutaka kuyaandika haya, ila sipendi uendelee kuteseka kwa sababu yangu. Licha ya kwamba kwa sas… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI