Thursday, September 14, 2017

Kati ya maeneo ambayo huwa yanawatia watu Joto Kubwa ni eneo la Umalizaji. Umalizaji huu huenda mbali zaidi katika mchezo wa Mpira, katika Utumishi, kwenye Chumba cha Mitihani, kwenye Ndoa, Uchaguzi Mkuu n.k... Eneo hili huwafanya wengine kupata Heshima na wengine Kudharauliwa.


Kuna Wachezaji ambao huwa wanapiga sana Chenga katikati ya Uwanja na kisha kushindwa Kuwa na Umaliziaji mzuri (Kufunga Goli), kisha kuanza Kusemwa vibaya na Washangiliaji. Vivyo hivyo kwa Wanafunzi ambao huwa wanafaulu sana Mitihani ya ndani ya shule na kushindwa Kumaliza vyema (kufaulu mitihani ya nje).

Pointi yangu kubwa ipo katika UMALIZAJI. UNAMALIZAJE HUU MWAKA WA 2017??

Naamini kabisa ya kwamba MAJIRA kama haya mwaka Jana, kuna mambo ambayo Ulighairi kuyafanya na kusema ya kwamba utayafanyia kazi ndani ya mwaka huu wa 2017. Lakini pia Uliupokea Mwaka huu kwa Shangwe na Ndelemo za "HAPPY NEW YEAR (HERI YA MWAKA MPYA)" huku Ukiwa na MALENGO na Mipango mingi kwenye 'Diary' zako kubwa. Ulikuwa Moto sana, hukuacha Kuhudhuria Semina mbali mbali na Kusoma Vitabu vingi.

Nakuuliza tena "UNAMALIZAJE HUU MWAKA WA 2017??"

Mwaka huu Unapokwisha, ni JAMBO gani Umelifanya au Utalifanya na kuweka Kumbukumbu Chanya kwenye Maisha yako?

Inawezekana ulikuwa na MALENGO na Mipango mingi sana na hujafanya kama Ulivyokuwa umepanga mwanzoni mwa mwaka huu. Usife MOYO na Kughairi tena kwa kusema ya kwamba Utafanya Mwakani. MUDA bado upo. Ni wewe tu Kubadili namna unavyoona, kufikiri na kuamini Nafsini mwako. Huwezi ukafanikiwa zaidi ya Yale yanayofanyika Nafsini mwako.

Amua Leo kuchagua JAMBO moja na kuliwekea NGUVU kubwa hadi lifanikiwe (Focus). JAMBO ambalo litakuachia Kumbukumbu Chanya ndani ya maisha yako utakapokuwa ukiukumbuka huu mwaka wa 2017. Wazungu husema ya kwamba "half a Loaf is better than nothing" na "Better Late than Never"
Ni BORA Uchelewe na Kufika kuliko Kukata tamaa na kuwa Sanamu.

Mungu anakuwazia MAWAZO Mema, Usimwangushe kabisa. Atakapokuja kuchukua hesabu ya Yale uliyoyafanya mwaka huu, basi jitahidi akute hata jambo moja ambalo Umelifanya kwa Ukamilifu na kwa Uaminifu. USIWE NA VIPORO VINGI, ZINGATIA UBORA.


Kwa Upande wangu, Nilikuwa pia na Mipango na MALENGO, baadhi yamefika mbali na mengine bado. Lakini moja kubwa lilikuwa ni Kumiliki KITABU changu KIPYA katika mfumo wa hardcopy. Na sasa limefanikiwa kwa 90%. Nikiamini ya kwamba NITAONGEA NA WATU WENGI SANA KUPITIA HICHO KITABU KIPYA kuliko ambavyo Ningefanya kwa njia ya KUONGEA Ana kwa Ana na mtu mmoja mmoja huko Shuleni, kanisani au Mitaani.

Dhamiria kufanya JAMBO ambalo litapandisha Thamani yako. Dhamiria pia kupata hicho KITABU changu KIPYA katika mfumo wa hardcopy. Ndani yake Utapata mambo ya kukusaidia Kumaliza huu mwaka vyema na kuanza mwaka mpya Ukiwa na kiapo cha "SITARUDI NYUMA TENA"
Tafakari: UNAMALIZAJE HUU MWAKA WA 2017!! Vizuri au Vibaya!! Amua sasa.


Ninayomengi sana ya Kuandika lakini hutabadilika Usipofanyia kazi hata hayo machache. Mengine utayakuta Kitabuni.
0764793105
Lackson Tungaraza


Naitwa Lackson Tungaraza.
Fb.com/ltungaraza
Description: https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v9/f5e/1/16/1f51b.png0764793105 (#WhatsApp)
Description: https://static.xx.fbcdn.net/images/emoji.php/v9/f66/1/16/1f493.pngSHARING IS CARING.


Related Posts:

  • FACEBOOK VS BLOG KIPI NI BORA KWA BIASHARA YAKO? Kumekuwa na sitofahamu juu ya namna ya kutumia mitandao hii katika kukuza biashara. Ndiyo maana nimekuuliza; Kati ya Facebook na Blog, ni kipi bora kwa Biashara yako? Jibu lako litaash… Read More
  • WHAT DO YOU WANT TO BE REMEMBERED FOR?  Kwa kawaida kila mtu huwa anatamani na anapenda ya kwamba akitenda jambo, baadae Akumbukwe kwalo. Ikiwezekana hata watu kadhaa watoe shuhuda za jambo hilo. This a human character. Unataka kukumbukwa kwa lipi… Read More
  • JE UNAJIKUBALI...! #KUJIKUBALI NI HATUA KUBWA SANA NA YA KWANZA KATIKA MAISHA ILI MTU AWEZE KUFURAHIA UUMBAJI WA MUNGU. #Hivi unamkubali kwa asilimia ngapi huyo unayemwona kwenye Kioo unapojiangalia? #Kuna waliojikatia tamaa kabisa, hawata… Read More
  • BE A SILENT KILLER*Mwuaji wa Kimya Kimya* Hahahaa... Nakumbuka wakati nilipokuwa nikitazama Movie za Kivietnam. Komando mmoja anatumwa kwenda kuokoa watu zaidi ya Kumi waliochukuliwa mateka huko Vietnam. ⚜Katika harakati zake za kuingia ka… Read More
  • DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO.Ukubali, Ukatae.. Ukweli unabaki pale pale ya kwamba DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO. Karibu tupeane Maarifa kidogo hapa, Kujifunza Kitu Kipya Kila Mara ni sifa kubwa ya watu wenye Mafanikio Makubwa maishani. -Binafsi napen… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI