Saturday, September 2, 2017

Jina lake kamili ni Maza Sinare Mchome. 
 
Alipokuwa anaongea katika Kipindi cha Ndoano ndani ya Wanawake live tv ya JOYCE KIRIA, alisema ya kwamba alipokuwa Mdogo alikuwa anaweka 2000 juu ya meza na kuisemeza ya kwamba hataitumia hadi iwe 4000. 

Pengine ilichangiwa na aina ya wazazi aliokuwa nao, maana walikuwa ni wachapakazi sana. Mamake alikuwa Fashion designer na Fundi Cherehani mzuri, na babaye alikuwa Daktari wa Mifugo.


MAZNAT alisoma sana na kupata vyeti kadhaa vya kiheshima, lakini MWISHO wa siku aliamua kuweka Vyeti pembeni na Kuanza KUJIAJIRI. 


Nilijifunza mambo kadhaa kutoka kwake kama ifuatavyo;


1. MTAZAMO

MAZNAT alikulia maisha ya kuwa na Mtazamo Chanya katika Kila jambo alilokuwa akikutana nalo. Mtazamo huo ulimwezesha Kupiga hatua sana Kimaisha, na Mtazamo huo ulichangiwa pia na aina ya watu waliokuwa wakimzunguka kwanzia kwenye familia yao na kwingine. 

Hivyo ni muhimu sana kuwa na MTAZAMO CHANYA. Haijalishi Aina ya FURSA unayopata, pesa unazoingiza, nafasi yako katika Jamii. JAMBO kubwa ni Mtazamo, una Mtazamo gani??


2. DHARAU
Dharau ya jambo lolote ni mbaya. MAZNAT alishawahi kuuza Vocha, Ubuju, Maji, Big G, mitumbe, house Girl n.k. 

#Chochote ambacho hakimkosei Mungu ni vyema kukifanya pasipo kukidharau. Hata kama kinakuingizia Fedha ndogo au kubwa, kiheshimu kabisa. Acha kudharau hicho kidogo unachofanya leo. Wajasiriamali wakubwa unaowaona, nao walikuwa wadogo hapo awali.

Kumbuka MAZNAT alikuwa akiheshimu hata biashara ya Big G, kusaga Unga wa Watoto n.k.


3. UTHAMINI.

MAZNAT alikuwa msomi, lakini hakujali hilo, akaanza kufanya biashara ndogo ndogo kwa kuzithamini sana. MWISHO wa siku zikamtoa Kimaisha.

Hivyo ni vyema kuthamini biashara au kazi ufanyayo hata kama hailingani na vyeti vyako au haiendani na Mtazamo wa watu kwako. Kuna walioanza kuuza Vitumbua na sasa ni wamiliki wa Hoteli kubwa, walianza kucheza mpira wa mchangani na sasa wanacheza Ligi kuu TANZANIA bara na wengine wako Ulaya. Kila kitu ni hatua. Nyumba ya ghorofa 30 huanza kwa Tofali moja. Wazungu husema, "ROME WASN'T BUILT IN A SINGLE DAY." Kwahyo THAMINI unachofanya sasa, uwe na UVUMILIVU na IMANI juu ya mambo YATARAJIWAYO bayana na Yale Yasiyoonekana kwa sasa.

KWA upande mwingine, MAZNAT alikulia maisha ya kubanwa sana na WAZAZI wake. Alikuwa hapati MUDA WA kukaa KIHASARA HASARA wakati wa Likizo. Alikuwa anapewa pesa baada ya KUFANYA KAZI KWANZA. Siku moja alifanya kazi vizuri sana na KUPEWA Tsh. 10,000. Akaichukua hiyo Fedha na kuanzisha Home English Tuition Center, akapata wanafunzi kadhaa aliokuwa akiwafundisha Kiingereza hapo kwao. Kwa sasa ni Mfanyabiashara Mkubwa anayemiliki MAZNAT BRIDAL CARE nk

Hivyo WAZAZI nao wana NAFASI kubwa sana ya Kuwafanya watoto wao kuwa Wachapakazi na wajasiriamali wakubwa. Waswahili husema,"Mtoto Umleavyo ndivyo Akuavyo, SAMAKI MKUNJE ANGALI MBICHI" na Wazungu husema, "CHARITY BEGINS AT HOME"

KWA yote hayo niliyoandika hapa, MAZNAT ni mfano mzuri sana wa wanawake wa kuigwa katika Jamii. Ni mfano mzuri kwa MABINTI na wamama ambao wanajiona Hawafai au Hawawezi kufanya mambo makubwa katika Jamii zao. Pia ni mfano kwa VIJANA ambao walidhani ya kwamba Wanawake wote ni Wadhaifu kikazi nk.

Aliyeandika haya ni Lackson Tungaraza
Facebook! fb.com/ltungaraza
WhatsApp!0764793105

NI WAKATI WA KUACHA LAWAMA NA KUPIGA KAZI. HUU NI MSIMU WA 'HAPA KAZI TU'
Watumie na wenzako Wajifunze pia.

Related Posts:

  • JE UNATAKA KUKINYWEA KIKOMBE CHAKE?Asomae na asome kwa Umakini na Kuelewa Lengo la Makala hii. Kabla ya Hadithi kuanza kusimuliwa, huanza Hadithi! Hadithi! Hapo zamani za Kale… Nami katika Kutafakari jambo hili, nikakumbuka hapo zamani za kale za Mama yao Wa… Read More
  • FIKIRIA NJE YA BOX All the so-called 'Secrets of Success' will not work unless you do--Unknown. Siri za mafanikio ni nyingi sana na utaendelea kuzisikia na kuzisoma sehemu mbali mbali.. Mtandaoni, magazetini, vitabuni nk..... Sidhani kama k… Read More
  • ROLE MODEL WETU WA LEO 16/1/2016 WILLIAM H GATES III    WILLIAM H GATES III William H Gates III , anajulikana kama Bill Gates. Alizaliwa tarehe 28 Oktoba 1955 na kulelewa katika kijiji cha Seattle pamoja na dada zake wawili. Baba yake ni At… Read More
  • "JIFUNZE KWA MWANAMKE MCHAPAKAZI MAZNAT"Jina lake kamili ni Maza Sinare Mchome.    Alipokuwa anaongea katika Kipindi cha Ndoano ndani ya Wanawake live tv ya JOYCE KIRIA, alisema ya kwamba alipokuwa Mdogo alikuwa anaweka 2000 juu ya meza na kuisemeza ya… Read More
  • HAKIKA, ANASTAHILI KUPEWA SIFA.Haikuwa jambo jepesi kuacha shughuli zake, Umaarufu wake, Ulinzi, Utajiri na kuja kututembelea huku kwetu. Sidhani kama wewe msomaji ungeweza kufanya hivyo. Yeye aliweza, pasipo manung'uniko wala hamu ya kutamani kurudi huk… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI