Thursday, September 8, 2016


Heri Kuchagua Jina jema kuliko Mali nyingi [smart phones, kompyuta, iPhone, iPad, gari, nyumba, nguo, shamba, ng'ombe]; Na Neema kuliko fedha na dhahabu.. Mith 22:1

Watu wengi sana hawajali juu ya majina wanayojiita au wanayoitwa [mwendokasi, msiba, playboy, muuza sura, kikaango, taabu, huzuni] .. Badala yake wanajali Mali nyingi(magari, nyumba, mashamba) pamoja na fedha na dhahabu.

Wako tayari kucheza uchi mbele ya Kamera[mfano video ya chura, diamond] na hata kuvaa mavazi ya kuonesha maungo ya ndani ili tu wapate Mali nyingi pamoja na fedha.
Wako tayari kutembea wa waalimu wao, wazazi wao, waajiri wao, wachungaji wao ili watengeneze Mali nyingi. Wanasahau ya kwamba HERI KUCHAGUA JINA JEMA KULIKO MALI NYINGI.



Kunamuunganiko kati ya historia ya Mtu na Jina lake. Unaitwa Malaya, shoga, playboy, mzinzi, kahaba, changudoa... Unadhani historia yako itakuwaje? Kuna watu ambao hata kufariki kwao jamii ilisema *Afadhari Mtoto wa fulani kaondoka duniani maana alikuwa kero hapa mtaani.. Kila binti ni mimba, wake za watu kuwaonga* Historia hujengwa kuanzia katika Jina ulilochagua.

Neema kuliko fedha na dhahabu. Neema inayoongelewa hapo ni neno la Kristo. Neno la Mungu ni zaidi ya fedha na dhahabu... Ukipokea neno umepokea vyote. Uko tayari kuandikiwa Historia njema? Chagua Neema pamoja na Jina jema... Mungu Vs Kusudi.

Jina linabeba maana na Kusudi.
Yesu maana yake ni Mkombozi, Kusudi ni Kukomboa watu wake na dhambi zao #Mathayo 1;21.
Jina lako linamaana na Kusudi gani?

Acha kutembea na wanawake wanaokuzidi umri almaarufu kama mashugamami ili upate Mali nyingi au fedha. Acha kuchanganya wanaume ili upate fedha... CHAGUA NEEMA KULIKO FEDHA NA DHAHABU. JINA JEMA KULIKO MALI NYINGI.
Now Is Your Time to Choose a better name and Grace. Mwl. Emmanuel Makwaya Godfrey anasema To Be Is To Do, Shemeji Melayeki anasema From Reading to Leading, Pastor Raphael Joachim Lyela anasema Kama unabisha Ogelea kwenye Gundi.

Proudly sponsored by
N.Y.I MOVEMENT
*Join today and Be part of the Change*
©Lackson Tungaràza
0764793105 whatsapp/call°

Related Posts:

  • SIRI ILIYOPO KATIKA UTENDAJI -------------------------------------------------------------------------------------------------------------- -------------------------------------------------------------------------------------------------------------- … Read More
  • UJASIRIAMALI NI NINI? Kuna tafsiri mbali mbali katika vichwa vya watu na katika mitandao ya kijamii juu ya dhana ya UJASIRIAMALI. Wengi wamepata tafsiri zilizowapa presha na kuamua kuacha kuwa WAJASIRIAMALI, na baadhi hawatambua ni kwa namna gan… Read More
  • MAONGEZI YENYE MAANA NI YAPI HAYO... Tungaraza na Kijana Joseph katika Mjadala. Kila mara watu tunajikuta tupo au tunaingia wenyewe katika Mazungumzo, na hayo mazungumzo yanaweza yakawa yenye kuleta Matokeo chanya au hasi. Hivyo uhalali wa matokeo ya mazungumzo unategemeana na wahusika binafsi. Leo… Read More
  • UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tele, una ndugu, una marafiki wazuri, umekul… Read More
  • JINSI YA KUWEKA MALENGO NA NAMNA YA KUFANIKISHA MALENGO YAKO  By Lackson Tungaraza 0764793105 whatsapp. Habari yako rafiki yangu mpendwa? Baada ya kuwa tumejifunza mada mbalimbali za ukombozi wa fikra na mafanikio ya kiuchumi. Napenda kukushukuru kwa ufuatiliaji wako katik… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI