Thursday, September 8, 2016


Heri Kuchagua Jina jema kuliko Mali nyingi [smart phones, kompyuta, iPhone, iPad, gari, nyumba, nguo, shamba, ng'ombe]; Na Neema kuliko fedha na dhahabu.. Mith 22:1

Watu wengi sana hawajali juu ya majina wanayojiita au wanayoitwa [mwendokasi, msiba, playboy, muuza sura, kikaango, taabu, huzuni] .. Badala yake wanajali Mali nyingi(magari, nyumba, mashamba) pamoja na fedha na dhahabu.

Wako tayari kucheza uchi mbele ya Kamera[mfano video ya chura, diamond] na hata kuvaa mavazi ya kuonesha maungo ya ndani ili tu wapate Mali nyingi pamoja na fedha.
Wako tayari kutembea wa waalimu wao, wazazi wao, waajiri wao, wachungaji wao ili watengeneze Mali nyingi. Wanasahau ya kwamba HERI KUCHAGUA JINA JEMA KULIKO MALI NYINGI.



Kunamuunganiko kati ya historia ya Mtu na Jina lake. Unaitwa Malaya, shoga, playboy, mzinzi, kahaba, changudoa... Unadhani historia yako itakuwaje? Kuna watu ambao hata kufariki kwao jamii ilisema *Afadhari Mtoto wa fulani kaondoka duniani maana alikuwa kero hapa mtaani.. Kila binti ni mimba, wake za watu kuwaonga* Historia hujengwa kuanzia katika Jina ulilochagua.

Neema kuliko fedha na dhahabu. Neema inayoongelewa hapo ni neno la Kristo. Neno la Mungu ni zaidi ya fedha na dhahabu... Ukipokea neno umepokea vyote. Uko tayari kuandikiwa Historia njema? Chagua Neema pamoja na Jina jema... Mungu Vs Kusudi.

Jina linabeba maana na Kusudi.
Yesu maana yake ni Mkombozi, Kusudi ni Kukomboa watu wake na dhambi zao #Mathayo 1;21.
Jina lako linamaana na Kusudi gani?

Acha kutembea na wanawake wanaokuzidi umri almaarufu kama mashugamami ili upate Mali nyingi au fedha. Acha kuchanganya wanaume ili upate fedha... CHAGUA NEEMA KULIKO FEDHA NA DHAHABU. JINA JEMA KULIKO MALI NYINGI.
Now Is Your Time to Choose a better name and Grace. Mwl. Emmanuel Makwaya Godfrey anasema To Be Is To Do, Shemeji Melayeki anasema From Reading to Leading, Pastor Raphael Joachim Lyela anasema Kama unabisha Ogelea kwenye Gundi.

Proudly sponsored by
N.Y.I MOVEMENT
*Join today and Be part of the Change*
©Lackson Tungaràza
0764793105 whatsapp/call°

Related Posts:

  • "I DON'T STOP WHEN I'M TIRED, I STOP WHEN I'M DONE"*Akasema, YOTE IMEKWISHA. LIFE is PERFORMANCE. Na Mara unapoanza Kuperfom ndipo unaanza kutambua aina ya wasikilizaji na watazamaji ulionao. Aidha wako pamoja nawe, au la. That's how life is in this world. Bahati Bukuku a… Read More
  • FACEBOOK VS BLOG KIPI NI BORA KWA BIASHARA YAKO? Kumekuwa na sitofahamu juu ya namna ya kutumia mitandao hii katika kukuza biashara. Ndiyo maana nimekuuliza; Kati ya Facebook na Blog, ni kipi bora kwa Biashara yako? Jibu lako litaash… Read More
  • WHAT DO YOU HAVE? UNA NINI? Do you Need Success? Do you want a Life of Prosperity? Do you Love walking with God at Higher Standards? Are you Passionate of having a Job or a Business? WHAT DO YOU HAVE? UNA NINI? Every Now and Then, People Seek New th… Read More
  • UNAMALIZAJE HUU MWAKA WA 2017?? Kati ya maeneo ambayo huwa yanawatia watu Joto Kubwa ni eneo la Umalizaji. Umalizaji huu huenda mbali zaidi katika mchezo wa Mpira, katika Utumishi, kwenye Chumba cha Mitihani, kwenye Ndoa, Uchaguzi Mkuu n.k... Eneo hili hu… Read More
  • JE UNAJIKUBALI...! #KUJIKUBALI NI HATUA KUBWA SANA NA YA KWANZA KATIKA MAISHA ILI MTU AWEZE KUFURAHIA UUMBAJI WA MUNGU. #Hivi unamkubali kwa asilimia ngapi huyo unayemwona kwenye Kioo unapojiangalia? #Kuna waliojikatia tamaa kabisa, hawata… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI