Friday, January 8, 2016

ZAWADI YANGU KWAKO MFANYABIASHARA NA MJASIRIAMALI WA KWELI


Habari yako Mfanyabiashara na Mjasiriamali?
Namrudishia Mungu sifa, utukufu na heshima kwa kunilinda hadi siku hii ya leo na pia kukulinda wewe Mjasiriamali na Mfanyabiashara. Kwa hakika tusingeliweza kufika mahali hapa tulipo kama isingelikuwa ni rehema zake kwetu, tumepitia visa na mikasa mbali mbali ya kukatisha tamaa, kuchoa machozi, kufiwa, kufilisiwa, vitisho. Lakini katika yote hayo, tumeibuka washindi na sasa bado tunasonga mbele tena huu mwaka. Inawezekana unapitia maisha magumu ya kukatisha tamaa na hata huoni msaada mwingine. Ndugu, jamaa na rafiki wamekukimbia, nakuomba usikate tamaa na umwamini yeye aliyekuweka hai hadi hii siku ya leo. Kuna jambo ambalo Mungu atatenda muda siyo mrefu katika maisha yako ikiwa hutokata tamaa na ukiendelea kumwamini.

Katika mwaka huu mpya tuliyouanza siku kadhaa zilizopita, kila mmoja wetu kajiwekea Malengo ya kufikia kabla ya mwaka kuisha. Inawezekana mipango uliyonayo umeiga au ni kwa tamaa tu, usihofu mwaka huu ni Mwaka wa Mabadiliko ukichukua hatua ya imani ya kutaka kubadilisha maisha yako kuanzia muda huu. Ili kuleta Mabadiliko hayo chanya katika maisha yako, inakubidi kuwa mtu wa vitendo na siyo maneno. Katika kukusaidia kuleta Mabadiliko katika maisha yako, ikiwemo suala ya kiuchumi, nimekuandalia kitabu cha biashara kilichopewa jina la “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA” Kikiwa ni sehemu ya kwanza ya Mada ya “SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA.”

Hii Ofa ni kwa wale wote ambao watajiunga na Semina ya biashara itakayoanza kesho tarehe 8 January. Nafasi hii ni yako wewe Mfanyabiashara na Mjasiriamali makini, fanya maamuzi sahihi ya kuleta mabadiliko katika maisha yako ndani ya mwaka huu. Isiishi maisha ya kubahatisha kila mwaka, biashara pia inahitaji kuwa na elimu yake na maarifa. Usipochukua hatua nzuri mwanzoni mwa mwaka, utapata shida huko mbeleni. NYOTA NJEMA HUONEKANA ASUBUHI.

Nakukumbusha juu ya semina ya mwaka wa mafaniko wa 2016, itakayoanza tarehe 8 Januari kesho kwenye makundi ya wasap na Email(barua pepe). Hivyo ni vyema ukalipia mapema gharama za semina kabla ya muda kufika ili kuleta mafanikio ya kiuchumi, kimtazamo na kiroho mwaka 2016. Mada zilizopo ni;

1.      Jinsi ya kupata Wazo bora la Biashara
Kuna watu wengi ambao wana Mitaji lakini hawajui wafanye biashara gani itakayowapa mafanikio

2.     Siri itakayo badilisha maisha yako mwaka 2016
Hii Siri itakupa ushindi wa kiuchumi na katika mfumo wako wa maisha

3.     Jinsi ya kuweka Malengo na njia za kufanikisha Malengo yako mwaka 2016
Utapata Mbinu zilizofupi na za Uhakika

4.     Mambo ya kuepuka ili ufanikiwe kiuchumi mwaka 2016
Kuna mambo  mengi ambayo yamekuwa  yakiwazuia watu kufanikiwa kiuchumi, yamechambuliwa vizuri. Pia baada ya Semina utapata Bure copy ya kitabu kiitwacho “SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA” sehemu ya kwanza iliyopewa jina la “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA.”

PATA COPY YA KITABU HIKI BURE KABISA
BAADA YA SEMINA
0764793105
Lackson Tungaraza


Gharama ni Tsh. 10,000/- tu na Semina itafanyika wiki nzima kuanzia tarehe 8 Januari. Hivyo wahi mapema nafasi hii muhimu kwa kutuma pesa yako kwenda namba 0764793105, utaona jina limeandikwa Lackson Tungaraza . Usisahau kutuma Jina lako kwa ajili ya uhakiki na barua pepe(Email Address) kwa njia ya SMS. Ikiwa hauna Wasap au Barua pepe, nijulishe ili upate masomo kwa njia ya Inbox yako ya Facebook. FANYA UWAMUZI SAHIHI. Usisite kuSHARE na kuCOMMENT hapa.

FURAHIA FURSA AMBAZO MUNGU ANAKUPATIA
HUWEZI KUFANIKIWA KWA UBINAFSI
Karibu  Nikupe Semina Ya Ujasiriamali
2016, Mwaka Wa Mabadiliko



1 comment:

  1. Kama wewe ni mfanyabiashara au mjasiriamali makini, sidhani kama utapanga kukosa semina hii kwa njia ya whatsapp na Email
    Unasemaje juu ya hili?
    Toa maoni yako hapa

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI