Tuesday, January 5, 2016

NGUVU YA MANENO YATOKAYO KATIKA VINYWA VYETU


Walisema manabii na mitume, “Atakaye kupenda maisha na kuona siku njema auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isinene hila” (1 Petro 3:10). Wengine wakaongezea”Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake” (Mith 13:2). Hayo yote yalitokea ili sisi tupate kujifunza namna gani tunaweza kuwa sehemu salama kwa kuwa makini nay ale tunayoyatamka kutoka katika vinywa vyetu.
Walisema, nimeamini na mimi nakwambia leo “MANENO NI SILAA” tena silaa yenye nguvu zaidi ya bunduki, mabomu au wanyama wakali wa mwituni. Wananchi wameingia katika balaa la kupigwa na Askari ovyo kwa sababu ya maneno mabaya ambayo viongozi fulani waliyatamka. Ndoa zimevunjika, zimetengana, yote sababu ya maneno waliyoyatamka wana ndoa hao.

Wanafunzi shuleni wanaendelea kufeli mitihani yao, afya za wagonjwa kuzidi kuwa mbaya kila siku kisa maneno waliyojitamkia. Wanasema, “Mimi ni wa kufeli tu”, “hatuna historia ya kudumu kwenye ndoa”, “umasikini tumeumbiwa”, “huu ugonjwa ni wa kwangu” n.k.

Tukibadili aina ya maneno yanayotoka vinywani mwetu, tutakuwa na amani, umoja, furaha na maendeleo katika jamii na kwetu pia kwa sababu hapatakuwepo na kauli mbaya za kuleta misuguano
Tofauti iliyopo kati ya waliofanikiwa na ambao hawajafanikiwa au tajiri na masikini, ni aina ya maneno yanayotoka katika vinywa vyao. Matajiri wanatamka maneno ya ushindi hata kama wako katika hali ngumu, wanajiamini hata kama mazingira waliyopo yanaleta hofu, waamini katika kutimiza malengo hata kama wengine wanakata tamaa, na maneno yao yanaashiria hivyo.

Baada ya kusoma juu ya nguvu iliyopo katika maneno tunayoyatamka kutoka  vinywani mwetu, mithiri ya kuleta umasikini, magonjwa, vifo katika maisha yetu. Kuanzia leo chukua hatua ya kuchunguza yale unayoyatamka juu ya maisha yako na juu ya watu wanaokuzunguka, kwa kufanya hivyo utapata mabadiliko ambayo hukutegemea hata katika biashara yako.
Hili somo limewasaidia wengi na kubadili aina ya maisha waliyokuwa nayo hapo awali, akiwemo Bwn. Lackson Tungaraza, blogger wa makala za kuikimboa jamii na Motivator, pia wanafunzi wa vyuo vikuu nchini. Wasiliana nae kujua zaidi, yale anayoyajua hadi sasa..Elimu haina Mwisho.

Nakukumbusha juu ya semina ya mwaka wa mafaniko wa 2016, itakayoanza tarehe 8 Januari kwenye makundi ya wasap na Email(barua pepe). Hivyo ni vyema ukalipia mapema gharama za semina kabla ya muda kufika ili kuleta mafanikio ya kiuchumi, kimtazamo na kiroho mwaka 2016. Mada zilizopo ni;

1.      Jinsi ya kupata Wazo bora la Biashara
Kuna watu wengi ambao wana Mitaji lakini hawajui wafanye biashara gani itakayowapa mafanikio

2.     Siri itakayo badilisha maisha yako mwaka 2016
Hii Siri itakupa ushindi wa kiuchumi na katika mfumo wako wa maisha

3.     Jinsi ya kuweka Malengo na njia za kufanikisha Malengo yako mwaka 2016
Utapata Mbinu zilizofupi na za Uhakika

4.     Mambo ya kuepuka ili ufanikiwe kiuchumi mwaka 2016
Kuna mambo  mengi ambayo yamekuwa  yakiwazuia watu kufanikiwa kiuchumi, yamechambuliwa vizuri. Pia baada ya Semina utapata Bure copy ya kitabu kiitwacho “SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA” sehemu ya kwanza iliyopewa jina la “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA.”


Gharama ni Tsh. 10,000/- tu na Semina itafanyika wiki nzima kuanzia tarehe 8 Januari. Hivyo wahi mapema nafasi hii muhimu kwa kutuma pesa yako kwenda namba 0764793105, utaona jina limeandikwa Lackson Tungaraza . Usisahau kutuma Jina lako kwa ajili ya uhakiki na barua pepe(Email Address) kwa njia ya SMS. Ikiwa hauna Wasap au Barua pepe, nijulishe ili upate masomo kwa njia ya Inbox yako ya Facebook. FANYA UWAMUZI SAHIHI. Usisite kuSHARE na kuCOMMENT hapa.


JIFUNZE KUJIAJIRI NA KUJITENGENEZEA KIPATO CHA ZIADA
Lackson Tungaraza
Blogger & Motivator
0764793105
USIPITWE NA SEMINA HII MUHIMU
2016, MWAKA WA MABADILIKO

1 comment:

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI