Wednesday, January 13, 2016

KWANINI SOKO LA AJIRA LIMEPUNGUA SANA KWA KASI KARNE HII?


Habari yako rafiki yangu mpendwa?
Napenda nikupe pongezi kwa kufuatilia masomo yetu mbali mbali katika mitandao ya jamii na kuhudhuria semina zetu za Ujasiriamali kwa njia ya Whatsapp na barua pepe. Leo tutajifunza mada uliyoisoma hapo juu katika kichwa cha habari.


KILA SIKU WATU WANAKESHA MITANDAONI NA KATIKA BAO ZA MATANGAZO
KUTAFUTA NAFASI ZA AJIRA

NAFASI ZA AJIRA KILA SIKU ZINAPUNGUA KWA KASI YA AJABU
NINI TATIZO?


WANAVYUO WANA PRESHA YA INTERVIEW ILI WAWEZE KUPATA AJIRA
JE, SULUHISHO NI SERIKALI?


Kila mara utawasikia wagombea Ubunge, udiwani, uraisi wakisema, “Mkituchagua sisi kwa hakika soko la ajira kwa vijana litapanda kutoka asilimia fulani hadi asilimia fulani.” Pia vijana wa kike na wa kiume masikioni mwao hupenda kusikia maneno kama hayo, lakini mambo hubadilika kuwa ndivyo sivyo pindi viongozi hao wanapoingia madarakani na kumaliza vipindi vyao vya uongozi bila kutimiza ahadi yao hiyo kwa vijana ambao ndiyo walio wengi nchini. Nini tatizo?
Lackson Tungaraza, baada ya utafiti wake ameweza kubaini kuwa tatizo siyo viongozi wala mfumo wa elimu nchini kama wengi wanavyolalamika, wakiwemo watu mashuhuri na maarufu nchini.

Tatizo ni “Sayansi na teknolojia”. Unaweza  shangaa au kukataa ni kwanini iwe Sayansi na teknolojia na siyo Serikali!!?
Ukuaji wa Sayansi na teknolojia nchihi na duniani kote unaathiri sana soko la ajira hata kwa wasomi kila siku, ndiyo maana wenye vyeti ni wengi kuliko wenye ajira.
Jiulize mambo yafuatayo;

1.     Wako wapi waliokuwa wanavusha watu ziwani kwa mitumbwi na mashua?
2.     Idadi kubwa ya vijana waliokuwa wanaishi kwa kuwarushia watu nyimbo kwenye simu zao kutoka kwenye Kompyuta,imeenda wapi?
3.     Idadi kubwa ya vijana waliokuwa wanasafisha mchanga migodini na kuchimba madini, imekimbilia wapi?
4.     Idadi kubwa ya watu waliokuwa wanalima mashamba yaw engine kwa jembe la mkono, imeenda wapi?

Utagundua kuwa  baada ya ugunduzi wa meli/boti, smartphones, bulldozers, tractors, robot n.k. Idadi kubwa ya watu wameondolewa katika sehemu zao za ajira za mwanzo. Mfano, kazi ambazo wangeliajiri watu 200 kiwandani kubeba vyuma na bidhaa zingine, hufanywa na Roboti mmoja au idadi kubwa ya watu ambao wangeliajiriwa na serikali kubeba moramu, mchanga, kuponda kokoto, hufanywa kwa mashine ambayo inaendeshwa na watu wachache sana. Na mambo mengine mengi kama hayo.
Ni wakati wako dada, kaka, mjomba, shangazi, baba, mama kufanya biashara inayoendana na ukuaji wa Sayansi na teknolojia. Wakati unasumbuka kutafuta fremu/pango kwa ajili ya kufungua biashara, wateja wengine wanafikishiwa bidhaa zilizo bora zaidi hadi milangoni mwao, atakuja saa ngapi kwako?
NI WAKATI WA KUCHUKUA MAAMUZI YA KUTAFUTA SULUHISHO LA
TATIZO LA AJIRA KATIKA MAISHA YAKO
USITEGEMEE SERIKALI
MUNGU KAWEKA KITU CHA THAMANI NDANI YAKO

Biashara ya Mtandao au Network Marketing ni biashara inayoweza kuleta mapinduzi ya kimtazamo na kiuchumi kwako kama ilivyofanya kwa wengine, bila kujali kiwango cha elimu, uzoefu bali ni msukumo uliyomo ndani yako kuyafikia malengo yako ya kifedha. Wasiliana nasi kupitia Whatsapp kwa nambari 0764793105 kuifahamu biashara hii na uendeshwaji wake.

Kama tayari una biashara na unapenda kuifanya kuwa ya tofauti na yenye mvuto mkubwa, kuna kitabu ambacho tunakitoa bure kabisa ili uweze kukuza biashara yako. Kimeandikwa “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA.” Ili kupata Nakala ya kitabu hicho, tuma Jina lako na Anuani ya barua pepe (Email address) kwenda namba 0764793105 au kwenye Email ya lacksontungaraza@gmail.com


Usisite kuuliza jambo lolote lile pale unapopata utata, wewe ni mtu wa maana sana kwetu. Pia unaweza kuwatumia na wengine taarifa hii au kutoa maoni yako hapa .Ahsante sana na ubarikiwe na Bwana.

1 comment:

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI