Saturday, January 2, 2016

JITAMBUE KUANZIA LEO


Heshima na Shukrani za dhati zikufikie wewe msomaji wa Makala zangu za Uelimishaji kupitia Mitandao ya Kijamii ya Facebook, Twitter, Linkedln, Instagram pamoja na blog yangu (lacksontungaraza.blogspot.com) kwani umekuwa msaada wangu kusonga mbele ndani ya mwaka 2015 na sasa tena uko pamoja nami mwaka 2016. Nimejipanga  huu mwaka kukupa Masomo na Semina mbali mbali ambazo zitakuwezesha kujitambua na kufanikiwa ndani ya huu mwaka ili itakapofika tarehe 31 Disemba ziwepo shuhuda nyingi za mafanikio kwa kila mmoja wetu, hivyo usiache kufuatilia masomo yangu na pia kuwa rafiki yangu facebook ( www.facebook.com/ltungaraza ).
Leo nitazungumzia suala la mtu kujitambua ana tabia ya aina gani maishani ili afanye mabadiliko na kusonga mbele. Nimezitenga hizo tabia katika makundi matatu ambayo kwa uhakika na wewe umo kama ukijitathimini baada ya kusoma. Makundi hayo ni;

Ø MTU WA KUIGA
Kama wewe ulikuwa msomaji mzuri wa hadithi zaSungura na Fisi, utagundua ya kwaamba fisi alikuwa anaiga mambo mengi kutoka kwa Sungura; njia alizokuwa akitumia Sungura kupata chakula wakati wa njaa, Ujanja n.k. Na hivyo kupelekea Sungura kuonekana ni Mjanja zaidi ya Fisi. Fisi alijikuta yuko matatani kwa kuwa na tabia ya kuiga.
Katika mfumo wa maisha ya mwanadamu, kuna watu ambao wao wapo kwa ajili ya kuiga ya wengine, hawana ya kwao. Inawezekana na wewe upo katika kundi hili lakini endelea kusoma, utagundua cha kufanya.

Unamkuta mtu katulia kama vile hana jambo la kufanya, kumbe anasubiri mtu fulani afanye na ndipo na yeye afanye. Inawezekana biashara unayoifanya  uliiga kutoka kwa jirani au rafiki yako, Masomo unayosoma shuleni uliiga sehemu baada ya kusikia kuna soko la ajira ukiyafaulu vizuri n.k.
Unapokuwa unamuiga mtu mwingine, unakuwa umedharau kipaji  au ujuzi wako ambao Mungu kakupatia. Biashara yako ingekuwa katika kiwango kikubwa sana kama ungetumia Ujuzi wako binafsi au mfumo wako wa maisha ungekuwa bora kwa kufuata yaliyo yako bila kuiga. ACHA KUIGA, FANYA AMBAYO MUNGU KAWEKA NDANI YAKO.

Ø MTU WA KUSHINDANA
Kuna watu ambao wapo hadi sasa duniani kwa ajili ya kushindana na ndoto za watu wengine. Kila mtu kaumbiwa jambo la kipekee ndani yake, linalomtofautisha na wengine na ndiyo maana ukitazama “finger print” au alama ya kidole chako ni ya kipekee duniani kote. Hata mapacha  wakifanana kwa kiwango gani lakini “finger print” zao ni tofauti.
Unapokuwa unashindana na Malengo na Ndoto za watu wengine, utaumia wewe mwenyewe. Muulize Farao ni yapi yalimtokea na majeshi yake ya Misri kwa kushindana na ndoto ya Musa ya  kuwatoa wana wa Israeli Misri na kuwapeleka Kaanani.
Wanasema, “Adhabu ya kaburi aijuaye ni maiti.” Mtu anapopanga malengo yake ya kutimiza, anakuwa ameshajitolea wakfu kwa changamoto yoyote ile itakayokuja mbele yake pasipo kukata tamaa. Wewe unaposhindana naye, utajihumiza na kukata tamaa. Usishindane na ndoto wa mtu mwingine, wala mfumo wake wa maisha.

Ø MTU WA UPEKEE
Ninaposema “Mtu wa Upekee” ni mtu ambaye anatenda yale ambayo yanatoka moyoni mwake na kuyaamini, yanaweza kuwa ni ya kiroho au ya kimwili.
Watu wa tabia hii huwa wanafika mbali kimafanikio kwa sababu wanatenda yale ambayo wanayaamini kutoka moyoni, maana akili hudanganya na pia kukatisha tama lakini moyo ndiyo umebeba uhalisia.
Ninakushauri sana ndugu yangu utoroke huko uliko, uje katika kundi hili la tabia la “Mtu wa Upekee.” Biashara yako na mfumo wako wa maisha ndani ya huu mwaka utabadilika na kuwa bora ukiwa “Mtu wa Upekee”. LIVE YOUR REALITY.

Napenda nikukumbushe juu ya Semina yetu kwa njia ya Mtandao (Online Seminar) itakayoanza tarehe 8 Januari kwenye makundi ya Wasap na kupitia barua pepe(Email). Masomo yatakayofundishwa ili kuleta mafanikio ya uhakika katika maisha yako mwaka 2016 ni;

1.      Jinsi ya kupata Wazo bora la Biashara
Kuna watu wengi ambao wana Mitaji lakini hawajui wafanye biashara gani itakayowapa mafanikio

2.     Siri itakayo badilisha maisha yako mwaka 2016
Hii Siri itakupa ushindi wa kiuchumi na katika mfumo wako wa maisha

3.     Jinsi ya kuweka Malengo na njia za kufanikisha Malengo yako mwaka 2016
Utapata Mbinu zilizofupi na za Uhakika

4.     Mambo ya kuepuka ili ufanikiwe kiuchumi mwaka 2016

Kuna mambo  mengi ambayo yamekuwa  yakiwazuia watu kufanikiwa kiuchumi, yamechambuliwa vizuri. Pia baada ya Semina utapata Bure copy ya kitabu kiitwacho “SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA” sehemu ya kwanza iliyopewa jina la “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA.”
PATA KITABU HIKI BURE KABISA BAADA YA SEMINA
2016, MWAKA WA MABADILIKO
Usipange Kukosa Semina Hii


·        Gharama ni Tsh. 10,000/- tu na Semina itafanyika wiki nzima kuanzia tarehe 8 Januari. Hivyo wahi mapema nafasi hii muhimu kwa kutuma pesa yako kwenda namba 0764793105, utaona jina limeandikwa Lackson Tungaraza . Usisahau kutuma Jina lako kwa ajili ya uhakiki na barua pepe(Email Address) kwa njia ya SMS. Ikiwa hauna Wasap au Barua pepe, nijulishe ili upate masomo kwa njia ya Inbox yako ya Facebook. KAZI NI KWAKO.

SHARE(shirikisha) na ndugu,jirani na rafiki zako juu ya hii Semina . Kwa lolote , 0764793105 (SMS/Piga/Wasap) 


5 comments:

  1. Je unapenda kujiunga na hii semina lakini bado una mashaka?.. Unaweza ukaandika tatizo lako hapa au ukanitafuta kwenye namba yangu 0764793105
    Kuwa muwazi

    ReplyDelete
  2. helo mr Habar za kaz
    tunashukuru kwa semina za kujikwamua kimaisha hasa hasa kwa ss vijana
    ndugu mwandishi, kwa sasa kuna tatizo kubwa la ajira hasa kwa vijana wanao tokaa ma vyuoni sasa tunafanyaje ili kujiajiri wenyewe??
    Na hii ni kwa sababu ya wasomi wengi ofici kuwa chache
    Ndugu mwandishi swal kwangu bado linanipa utataa ni kwa namna gan vijana wanaweza kujiajiri wenyewe ili tujikwamue kimaishaa?

    ReplyDelete
    Replies
    1. John Fidelis Mbuya, ahsante sana kwa kutoa ya moyoni ili kuleta ukombozi kwa vijana wengi nchini. Nakushauri sana ujiunge na hii semina itakayoanza tarehe 8 Januari kama nilivyoelezea hapo juu. Mtu yeyote yule ambaye anataka kujikwamua kiuchumi akaribie kwenye hii semina, naamini baada ya semina maisha yako yatakuwa tofauti.
      kutakuwepo muda wa maswali na majibu pia.
      kumbuka semina ni wiki nzima

      Delete
  3. Vijana wengi wanadanganyana vyuoni, kwamba wakimaliza tu masomo watapata ajira tena ya mishahara minono. Wanasahau ya kwamba kuna wenzao wa mwaka juzi, mwaka jana wapo bado mitaani wanazunguka na vyeti. Ni vyema kijana, mama, baba ukajiunga na semina hii ya kuleta ukombozi 2016....HUTOJUTA

    ReplyDelete
  4. Vijana wengi wanadanganyana vyuoni, kwamba wakimaliza tu masomo watapata ajira tena ya mishahara minono. Wanasahau ya kwamba kuna wenzao wa mwaka juzi, mwaka jana wapo bado mitaani wanazunguka na vyeti. Ni vyema kijana, mama, baba ukajiunga na semina hii ya kuleta ukombozi 2016....HUTOJUTA

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI