Saturday, January 16, 2016


WILLIAM H GATES III 

 
WILLIAM H GATES III
William H Gates III , anajulikana kama Bill Gates. Alizaliwa tarehe 28 Oktoba 1955 na kulelewa katika kijiji cha Seattle pamoja na dada zake wawili. Baba yake ni Attoney na marehemu mama yake alikuwa mwalimu tu wa kawaida wa shule. Katika umri wake mdogo Bill Gates alivutiwa na utengenezaji wa programu akiwa katika mojawapo wa shule kijijini Seattle. Akiwa huko shuleni Seattle, Bill Gates alikutana na Paul Allen , mwanafunzi mwenzake wakawa marafiki.Hapo ndipo wakaanza kutumia tarakilishi ndogo ya shule kuendeleza ujuzi wao, kama ambavyo pia wanafunzi mbalmbal duniani wanavyotumia elimu ya darasan na elimu ya kijamii kuvumbua mitandao mbalmbal ya kijamii n.k.

Baadaye Bill Gates akaenda kujiunga na  Chuo Kikuu cha Harvard kwa masomo ya elimu ya juu. Kwa mara nyingine tena akajiunga pamoja na Paulo kuandika toleo jipya la programu ya Msingi wa lugha ya kwanza ya kompyuta ya kibinafsi, iitwayo Altair 8800. Kampuni iliyotumia program hiyo iliridhishwa na kazi ambayo Bill Gates na Paul Allen waliofanya na programu hiyo ikapewa leseni.
Jambo hili liliwachangia Gates na Allen Kuanzisha kampuni ya Microsoft, iliyokuwa ikitengenezea kampuni zingine programu. Bill Gates aliacha masomo yake katika chuo kikuu cha Harvard na kujishughulisha muda wake wote katika biashara.
MICROSOFT COMPANY YA BWANA BILL GATES NA PAUL ALLEN

Funzo: Fanya lile jambo unalolipenda maishan kwa juhudi kubwa, usiige ya engine kwa sababu umeona wamefanya jambo Fulani. Mungu kakupatia jambo la kipekee ndani yako, usijidharau. YOU ARE GENIOUS, INVEST ON YOUR TALENTS.
Mafanikio yao yalikuja walipotengeneza mfumo wa kuendesha kompyuta uitwao MS-DOS uliotumika katika kompyuta ya kwanza ya kibinafsi ya IBM. Baadaye waliweza kuzishawishi kampuni zingine zinazotengeneza kompyuta kutumia mfumo huo wa MS-DOS. Mfumo huu mpya wa MS-DOS ulipata umaarufu katika soko miaka ya 1980.

Kipindi cha miaka mitano baadaye Microsoft ilitoa mifumo mipya ya Windows 2.0 iliyokuwa bora zaidi kuliko mifumo ya hapo awali. Kampuni ya Microsoft iliweza kupata umaarufu zaidi katika soko la hisa, na akiwa umri wa miaka 31, Bill Gates aliweza kuwa bilionea mchanga zaidi katika historia ya Marekani.
MAGARI YAKE YALIYOPO NYUMBANI

BAADHI YA MAENEO ANAYOMILIKI BWN. BILL GATES

Bill Gates alifunga ndoa na Melinda French Gates mwaka wa 1994 na wakabarikiwa na watoto watatu, Jennifer, Rory na  Fibi. Wote wawili Bill na Melinda ni waanzilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali. Waliweza kulianzisha shirika la Bill na Melinda Gates Foundation ambalo limesaidia kutoa michango mbalmbal ya kuiendeleza jamii pamoja na watu wasiojiweza. Ubunifu wa Bill Gates wa kutengeneza programu umekuwa mchango wake katika mapinduzi ya kompyuta na sayansi ya kompyuta.
Tangu Mwaka 1995 amekua namba moja katika orodha ya matajiri wakuu (forbes) duniani isipokua mwaka 2008 ambapo alikua namba 3 akiwa na utajiri wa takribani dola bilioni 58 za kimarekani. Mwaka huo Bw. Warren Buffet ndio alikua mtu namba mmoja akiwa na utajiri takribani dola za kimarekani bilioni 62 akifuatiwa na Bw.Carlos Slim akiwa na utajiri wa takribani dola bilioni 60 za kimarekani. Unaweza usijue lakini kila sekunde Bill Gates anaingiza takribani dola 250 za kimarekani, Na kwa dakika nzima anaingiza takribani dola 15000. Unashangaa?? . Bill Gates anaweza akagawa Dola 15 za kimarekani kwa kila mtu duniani na bado akabakiwa na dola milioni 5 za kimarekani mfukoni. Kama akiangusha dola 1000 za kimarekani hana haja ya kuziokota kwa sababu ndani ya sekunde 4 ambazo angeweza kuziokota angekuwa tayari amesha zirudisha . Ukiachana na kompyuta, pia Bill Gates ni muandishi. Mpaka sasa ana vitabu viwili amabavyo ni ”The Road Ahead'” na ‘Business at the Speed of Thought’.
BAADHI YA PESA ZA JAMAA, SIYO UCHAWI, 
NI REAL



Kwa Leo, hayo yanatosha kujifunza kutoka kwa Role Model wetu, Bwn. Bill Gates. Unalipi la kuongezea juu ya huyu jamaa, Mr. Bill Gates?.. Unaweza changia hapa na pia kuwashirikisha na wengine wajifunze (share)

MORAL OF THIS:
1: Kuna wakati ambapo sisi kama wanadamu tunatenda mambo ambayo hatuyapendi kutoka moyoni; bali kwa sababu ya tamaa zetu binafsi. Watu wanafanya kazi ambazo hawazipendi kutoka mioyoni ila kwa sababu mishahara ya hizo kazi ni minono.

2. Ukitenda jambo ambalo hulipendi kutoka moyoni, tambua ya kwamba hutopata mafanikio ambayo ulipaswa kupata katika maisha yako na pia hayo mafanikio hayatakuwa ya kudumu. Bwana Bill Gates na wengine wengi wamekuwa na mafanikio makubwa sana hadi hii leo kwa sababu waliweza kutenda yale ambazo waliyapenda kutoka mioyoni mwao. Anza leo kuwekeza nguvu kubwa katika fani, kipaji na ujuzi ulionao. Elimu ya shuleni ni daraja tu la kukutanisha na vitu fulani ambavyo Mungu anataka uvijue kabla ya kufika kule unakotaka  kwenda. Usiitegemee sana kuliko kipaji chako.

3. Watu waliowekeza katika fani, ujuzi na vipaji vyao wamefika mbali sana kimafanikio. Mfano Lionel Messi, Christian Ronaldo, Samatta, Diamond, Ambwene, Rose Muhando n.k. Japo kuwa elimu zao za darasani siyo kubwa kivile

4. Naamini kabisa ya kwamba 2016, Mwaka Wa Mabadiliko na kuinuliwa na Bwana katika maisha yako. Wekeza pia katika kutafuta elimu ya kiMungu katika maisha yako. Hvyo unaweza kuungana name katika kampeni ya kuleta ukombozi katika maisha yao kuanzia mwaka huu. Kampeni yangu inaitwa 2016, MWAKA WA MABADILIKO NA KUINULIWA kama ambavyo picha hii ya chini inavyoelezea;
USIPITWE NA MAONO HAYA JUU YA MAISHA YAKO, 2016, YEAR OF VICTORY.



1 comment:

  1. HUYU JAMAA KAFANYA MAISHA KUWA RAHISI KWA NAFASI KUBWA SANA, WEWE KAMA MPENDA MAENDELEO, UNALIPI LA KUSEMA JUU YA HUYU BILL GATES?
    Toa maoni yako hapa.

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI