Sunday, September 27, 2015

Hili ni miongoni kwa maswali ambayo nilikuwa najiuliza sana hivi kwanini watu wanafanyabiashara ya mtandao kwanini wasifanye biashara za kawaida haya ndio majibu kamili.tunafanyabiashara ya mtandao kwasababu zifuatazo.

1.UKOSEFU WA MUDA WA KUTOSHA
Watu wengi wanataka kuanzisha biashara lakini tatizo ni muda, hakuna ukiangalia mfumo wa biashara wa kizamani ambao tumezoea ili kuanzisha biashara lazima muda mwingi uwepo lakini mfumo huu wa biashara ya karne ya 21, Mult level marketing hauhitaji muda mwingi uwepo.

2.UKOSEFU WA MITAJI
Kama tunavyojua kwenye mfumo wa biashara wa kizamani ili uanze kufanyabiashara lazima uwe na mtaji mkubwa sana ndio uweze kufanikiwa lakini kwenye mfumo huu wa biashara unaanza kufanya biashara hata kama unamtaji mdogo cha msingi uwe serious nanuwe tayali kupambana.

3.KUEPUSHA UTEGEMEZI
Unapoanza hii biashara wengi huanza wakiwa wafanyakazi, hata mimi nakumbuka nilikuwa mwanafunzi, na nilikuwa nategemea sana fedha ya mikopo, hii ilinifanya kutokuwa na uhuru wa fedha na hata uhuru wa muda, hivyo mikopo haukai hata wiki tatu unapitia kwenye madeni.sasa nikaona ni bora nitafute biashara ili kuepuka utegemezi.hivyo tunafanya hii biashara kuepuka utegemezi, kutegemea mishahara, au kutegemea kuomba kwa ndugu, mme au mke.

4.KUPATA ELIMU YA BIASHARA
Katika vitu muhimu ambavyo naweza kusema vimebadilisha maisha yangu kwenye huu mfumo wa biashara ni kupata elimu ya biashara, nilianza kufanya hii biashara nikiwa sijui chochote kuhusu biashara lakini kupitia Mfumo huu wa biashara ya mtandao nikapata elimu ya biashara na sasa nafanya biashara zaidi ya moja.hata wewe kama uko serious na ukawa unafata mafunzo serious siku moja maisha yako yatabadilika sana.

6.KUWA MUWEKEZAJI HATA KAMA HUNA KIPATO
Ili awe na uhuru mzuri na wakweli wa fedha na muda ni lazima atoke kwenye kiwango cha mfanyabiashara wa kujiajiri na kuwa muwekezaji, kuwaajiri wengine.sasa kwa kupitia mfumo wa biashara wa kizamani ili uwe muwekezaji lazima uwe na pesa nyingi, maana uweze kuwekeza kwa kununua mashamba, kujenga majengo, kufubgua viwanda, au kuwa na vyombo vya usafiri.lakini sasa kupitia biashara hii ya mtandao, utaweza kuwa muwekezaji ambae utawekeza kwenye rasilimali watu ambayo ni rasilimali inayolipa sana.

SOMA: http://lacksontungaraza.blogspot.com/2015/10/ siri-ya-mafanikio-ndani-ya-biashara-ya.html

0764793105 kupata maelekezo ya kujiunga na mfumo huu wa biashara kwa Tsh.26000/- na kuanza safari yako kama mimi
Email:lacksontungaraza@gmail.com

Related Posts:

  • UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tele, una ndugu, una marafiki wazuri, umekul… Read More
  • SIRI INAYOVUTA MAFANIKIO SIRI INAYOVUTA MAFANIKIO  Nitakuwa muongo sana kama nikisema ya kwamba hamna mtu anayependa Mafanikio, hata wewe umechukua muda wako kusoma makala hii kwa sababu unapenda kufanikiwa kupitia hii Siri Inayovuta Mafa… Read More
  • IFANYE BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA LACKSON TUNGARAZA KATIKA HARAKATI ZAKE ZA KUTOA HUDUMA YA VIATU Tunashindwa kuongeza vipato vyetu kwa sababu  biashara zetu hazina mvuto Tunapoendelea kufungua vyanzo vingine vya vipato kwa kutumia mbinu zile zi… Read More
  • JE KIJANA UNAHAMU YA KUWA NA MAISHA YENYE FURAHA NA MAFANIKIO? Ni haki yako Kijana Mwenzangu kuwa na Maisha yenye furaha na Mafanikio. Tumia ushauri ufuatao ili uweze kufikia lengo hilo; … Read More
  • KWANINI BIASHARA YA MTANDAO Hili ni miongoni kwa maswali ambayo nilikuwa najiuliza sana hivi kwanini watu wanafanyabiashara ya mtandao kwanini wasifanye biashara za kawaida haya ndio majibu kamili.tunafanyabiashara ya mtandao kwasababu zifuatazo. 1.UK… Read More

1 comment:

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI