Monday, May 6, 2019


A- Kwenye biashara kuna kukuru kakara nyingi sana. Unaweza Ukapoteza pesa zako zote ulizoanzishia.

B- Fursa yo yote Ile ina Hatari ya kupata HASARA kabla ya FAIDA, tofauti Ipo kwenye Asilimia.

C- Mradi/BIASHARA yenye FAIDA kubwa sana ina hatari/vikwazo Vikubwa pia. Na kama FAIDA ni Ndogo, basi na hatari zake ni za kawaida. UNAWEZA UKAFUGA KUKU NA WAKAFA WOTE AU KUIBIWA

Ndivyo BIASHARA zilivyo.Matajiri wakubwa kama Donald Trump nao Walishakumbwa na hiyo mikasa - kuna Kipindi aliwekeza na kufilisika kabisa.

Kwa hiyo: "kabla ya kujiingiza kwenye biashara au FURSA, tathimini kama una Uwezo wa kustahimili hasara yo yote Ile utakayoipata huko mbeleni." - Lamax.


"USHUHUDA WANGU."

- Nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dodoma mwaka wa Pili, nilipata WAZO la kuanza kuuza viatu vya Kiume. Kwa hiyo nikachukua pea kadhaa za viatu Dar na kwenda navyo chuoni, nikiamini ya kwamba Vitapendwa na kuuzika Fasta. Nilipofika nikaandaa Tangazo na kubandika sehemu mbali mbali chuoni, na Pia Kusambaza kwenye Makundi ya WhatsApp.

Baada ya hapo nikaanza kusubiria Wateja. Mungu Sio Athumani, Wakaanza kuja, lakini Kila kiatu wanachopima wanasema Hawapendi Rangi, Hawapendi Muundo, au Hakuna vya Kuwatosha (Kwa maana ya size). Jambo hilo likawa linaniuma sana. Lakini nikaendelea kuwa na Uvumilivu. Baada ya Muda vikanunuliwa viatu kadhaa na vingine kubaki vikiwa vinanikodolea tu macho.

Baada ya Kuona ya kwamba Vinanijazia tu nafasi Chumbani kwangu na haviuziki, nikamtafuta jamaa niliyekuwa najuana naye, nikampatia hivyo viatu aviuze. Wakati wa Likizo, Jamaa akavichukua viatu vyote na kwenda navyo nyumbani kwao kijijini. Nilipomwuliza Baada ya Muda fulani, jamaa akaniambia Wadogo zake walivichukua na kuvivaa. Hilo Jambo lilinikera sana ajabu. Lakini nikamwacha nilipoona ya kwamba shida ilikuwa kwangu kwa kumwamini mtu asiyejua kuwa makini na biashara. Kwahiyo nikapoteza zaidi ya laki moja.

"WATU WENGI WANASHINDWA KUNUFAIKA KWENYE FURSA NA BIASHARA WANAZOZICHAGUA kwa Sababu ya MIHEMUKO MINGI YA KUONA YA KWAMBA WATAFANIKIWA HARAKA HARAKA. Na hiyo yote inatokana na MAHESABU YA KWENYE MAKARATASI."

Naamini Kuna Jambo Zuri sana ulilojifunza hapa, basi Litendee Kazi. Na kama Unahitaji Vitabu vyangu LACKSON TUNGARAZA usisite kuwasiliana nami moja kwa moja WhatsApp kwa kubofya hii LINK: https://wa.me/255764793105 . UNAWEZA KUPATA VITABU VYA HARD COPY (Nakala Ngumu) na SOFT COPY (Nakala Laini ya kusomea kwenye Simu au Kompyuta yako.




By Lackson Tungaraza.
@LACKSONTUNGARAZA.
AMUA LEO KUWA WA TOFAUTI.

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI