Monday, August 6, 2018

Tangu Uanze kuvunja Laana za UMASKINI, huu ni Mwaka wa ngapi, na Je Umeshaanza kuwa TAJIRI?

Kabla ya Kuanza au Kuendelea tena na Uvunjaji Wako wa Laana za UMASKINI, Tathimini Kwanza ni kwa Jinsi Umejitoa Kulipa Gharama za kuwa TAJIRI; Muda, Nguvu, Fursa, Maarifa, Pesa N.k
... Je Umeshahudhuria Semina ngapi za Kiuchumi-za bure na za Kulipia,?
... Umeshasoma VITABU vingapi vya Kukusaidia Katika eneo Unalotaka Kufanikiwa Kiuchumi,?
... Umeshajifunza kwa Watu gani Waliyokutangulia,?
... Umeshaanza Kufanya mangapi tangu Umalize Kusoma Vitabu na Kuhudhuria Semina Za Kiuchumi,?
... Matumizi Yako  ya Kifedha Yakoje -Nidhamu ya Mapato na Matumizi,?
... Matumizi Yako ya Muda Yakoje - Tangu Unapoamka hadi Unaporudi Kulala,?
... Umetumiaje FURSA ya Kifedha zinazokuzunguka,? Mfano Kutatua Matatizo na Changamoto zilizopo kwenye Jamii Yako; Maji, Chakula, Usafiri, Elimu N.K.
... Umejitoa Kwa Kiasi gani Kujifùnza kwenye Makosa Yako ya Awali,? - Kulalamika na Kuwalaumu Wengine hakuleti Msaada wo Wote.
... Unatumiaje Teknolojia ya Sasa katika Mambo Yako ya KIUCHUMI,?
- "Ukiendelea Kuishi Wakati huu Sasa kama zamani, Utapata Shida sana Kufanikiwa Kiuchumi. Kila Msimu Mpya Unapoingia, Jaribu Kubadilika kiMalengo na Kimkakati, lakini ubaki kwenye MAONO Yako."
- Lamax.

... Je, Una MAONO Yaliyoandikwa,?
- Maono Ni dira ya Maisha Yako... ni Wapi Uelekee na namna gani Uelekee huko.
- "Pasipo Maono WATU HUACHA KUJIZUIA"

... Je, Una Mipango na Mikakati gani ya Kujikomboa Kiuchumi,? - Hii inafuata baada ya Kuwa na Maono Yaliyoandikwa.

Baada ya hapo, ndipo Uendelee au Uache Mambo Yako ya KUVUNJA LAANA ZA UMASKINI. Inawezekana UJINGA Wako ndio Unaowapatia UTAJIRI na UMAARUFU Wale Mitume na Manabii wa Uongo.

. Life Is a Choice
   You Live What you Decide.
  . LACKSON TUNGARAZA

Related Posts:

  • ICEFM_KWANINI WATU HAWAFANIKIWI KWENYE MAISHA YA KILA SIKU_Part2 (made with Spreaker) ICEFM_KWANINI WATU HAWAFANIKIWI KWENYE MAISHA YA KILA SIKU_Part2 (made with Spreaker) Source: http://ift.tt/2zpTKIG kuna mambo kadha wa kadha ambayo huwa kwa namna moja ama nyingine huwafanya watu wasifanikiwe katika maisha … Read More
  • #JIULIZE Hivi hicho Unachokifanya Sasa Ukiwa peke Yako au ukiwa na mtu mwingine, kama Kesho utakikuta kwenye magazeti Yote ya Mitaani na Mitandaoni, JE UTAKIFURAHIA? JE NDUGU ZAKO WATAENDELEA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUWA DAMU MOJA NAWE… Read More
  • BADO UNAENDELEA KUVUNJA LAANA ZA UMASKINI? Tangu Uanze kuvunja Laana za UMASKINI, huu ni Mwaka wa ngapi, na Je Umeshaanza kuwa TAJIRI? Kabla ya Kuanza au Kuendelea tena na Uvunjaji Wako wa Laana za UMASKINI, Tathimini Kwanza ni kwa Jinsi Umejitoa Kulipa Gharama … Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI