Thursday, January 18, 2018

All the so-called 'Secrets of Success' will not work unless you do--Unknown.

Siri za mafanikio ni nyingi sana na utaendelea kuzisikia na kuzisoma sehemu mbali mbali.. Mtandaoni, magazetini, vitabuni nk..... Sidhani kama kuna mtu humu ambaye hajawahi kutamani Mafanikio na kufikia kiwango cha kutafuta Siri yake kwenye vyanzo mbali mbali.
Nimekutana na Vijana wengi sana, wengine ni ndugu zangu... Wamesoma vitabu kadhaa vya mafanikio. Mfano WHY WE WANT YOU TO BE RICH, RICH DAD POOR DAD, THINK BIG, THINK AND GROW RICH, MIDAS TOUCH n.k....

~~~Wengne wameenda mbali zaidi hadi kuhudhuria Semina za waandishi wa Vitabu hivyo ili waipate ladha halisi... Kama kunywa Togwa ambayo haijachacha. Why are they not Successful!!!!!"



Lackson Tungaraza nimejifunza vingi kwenye vitabu mbali mbali nilivyosoma, awali nilikuwa siyo msomaji wa Vitabu kama baadhi ya wapuuzi wanavyosema ya kwamba WATANZANIA HAWAWEZI KUSOMA VITABU HATA UFANYAJE. Baada ya kusota na maisha kwa muda, siku moja nilikwenda kwa rafiki yangu kuongea naye mambo fulani ... Kipindi ananionesha baadhi ya nondo alizonazo kwenye Kompyuta, ghafla nikakiona kitabu cha THE BUSINESS OF 21st CENTURY cha Robert Kiyosaki. Nilikichukua na kuanza kukisoma ukurasa kwa ukurasa pamoja na kunakili vitu vya Muhimu.

~~Aissseh! Macho yangu yalitiwa Nuru kuanzia siku hiyo.. Cha kwanza ilikuwa ni juu ya MAPATO NA MATUMIZI. Namna ambavyo wengne wanakuwa matajiri zaidi na wengne maskini zaidi... Assets vs Liabilities.

~Success Secret brings results to those working on it. Bila kufanyia kazi ulichosoma utabaki tu vivyo hvyo kama anayejitazama ktk kioo akaondoka na baadae kusahau alivyo na kurudi tena kujitazama. JIFUNZE KUENDESHA GARI BARABARANI SIYO KWENYE KOMPYUTA KWA KUCHEZA GEMU. Umenipata hapo?

~~Kuwa Mtendaji wa yapo Mema unayoyaona na kuyasikia.. Hamna tofauti ya mtu aliyesomea Kilimo na hajui hata kushika jembe na yule ambaye hakusomea hicho... Tunahitaji kuona kitu kimetokea siyo kimetabiriwa.

---Kwa Leo tuishie hapa, Maoni yako yanakaribishwa kabisa.
TENDA, USISEME TU.
Lackson Tungaraza.
( www.facebook.com/ltungaraza )
0764793105 Whatsapp, sms.


Related Posts:

  • ROLE MODEL WETU WA LEO 16/1/2016 WILLIAM H GATES III    WILLIAM H GATES III William H Gates III , anajulikana kama Bill Gates. Alizaliwa tarehe 28 Oktoba 1955 na kulelewa katika kijiji cha Seattle pamoja na dada zake wawili. Baba yake ni At… Read More
  • JE UNATAKA KUKINYWEA KIKOMBE CHAKE?Asomae na asome kwa Umakini na Kuelewa Lengo la Makala hii. Kabla ya Hadithi kuanza kusimuliwa, huanza Hadithi! Hadithi! Hapo zamani za Kale… Nami katika Kutafakari jambo hili, nikakumbuka hapo zamani za kale za Mama yao Wa… Read More
  • HAKIKA, ANASTAHILI KUPEWA SIFA.Haikuwa jambo jepesi kuacha shughuli zake, Umaarufu wake, Ulinzi, Utajiri na kuja kututembelea huku kwetu. Sidhani kama wewe msomaji ungeweza kufanya hivyo. Yeye aliweza, pasipo manung'uniko wala hamu ya kutamani kurudi huk… Read More
  • FIKIRIA NJE YA BOX All the so-called 'Secrets of Success' will not work unless you do--Unknown. Siri za mafanikio ni nyingi sana na utaendelea kuzisikia na kuzisoma sehemu mbali mbali.. Mtandaoni, magazetini, vitabuni nk..... Sidhani kama k… Read More
  • "JIFUNZE KWA MWANAMKE MCHAPAKAZI MAZNAT"Jina lake kamili ni Maza Sinare Mchome.    Alipokuwa anaongea katika Kipindi cha Ndoano ndani ya Wanawake live tv ya JOYCE KIRIA, alisema ya kwamba alipokuwa Mdogo alikuwa anaweka 2000 juu ya meza na kuisemeza ya… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI