Wednesday, July 6, 2016


Kuna siku niliandika hapa juu ya mada inayoitwa LIFE IS A PROCESS… Katika hiyo mada nilitoa mfano wa Mti ambao huanza kama mche baada ya mbegu kuwekwa ardhini. Hakuna mti ambao umetokea tu kuwepo hapo ulipo, ulianzia katika udogo sana… wengine wakaumwagilizia Maji kwa kutegea lakini baadae ukafikia hatua hiyo licha ya kupigwa na upepo na mvua nyingi.

Mada ya leo inawezekana ikawa ni mwendelezo wa mada iliyopita kwa mtazamo wako au ikawa mpya kulingana na nitakavyoelezea.  Inawezekana hapo ulipo umekata tamaa kwa hali ya maisha unayopitia kama kukoswa ajira, kutengwa na ndugu zako, maombi uliyomwomba Mungu hujajibiwa, magonjwa kila siku ni yako, pesa unazisikia tu katika matangazo ya M-Pesa, kila wazo la biashara unalopata halifanikiwi… MAISHA NI SAFARI NDEFU!
Lackson Tungaraza. Maisha Ni Safari ndefu.

I have Never met a great person with an easy past… Sijawahi kukutana na mtu aliyefanikiwa katika maisha ambaye anahistoria ya kawaida isiyokuwa na changamoto. Hiyo yote ni Safari na katika safari kunachombo cha Usafiri ambacho unatumia; Yaweza kuwa ni miguu, pikipiki, baiskeli, gari, ndege au mabawa… kulingana na hivyo vyombo vya usafiri vilivyo, ni vigumu kuwa na matokeo sawa. Mtu awezaye kuwa na nidhamu kubwa ya maisha ni yule ambaye anafuata kila hatua ya kwenda mbele, na siyo kuruka hatua ili awahi kufika. Nadhani umeshasikia habari za watu wanaojiunga na FREEMASON ili watajirike, ni mfano wa watu ambao wanataka njia za mkato… KULALA MASKINI NA KUAMKA TAJIRI! SITARAJII NAWE UWE MMOJA WAO

Nakumbuka kuna kipindi nilikuwa nafanya NETWORK MARKETING, nilikutana na changamoto sana. Nilikuwa nauza pedi za wanawake chuoni, stendi kuu ya Dodoma na kwa watu mbali mbali katika maeneo yao ya kazi. Moja ya changamoto ilikuwa ni MALALAMIKO YA BEI ya kwamba iko juu sana.. nikawa nawaza *Itawezekanaje bidhaa yenye ubora mkubwa ilingane na bidhaa ya kawaida!!* Nikawapotezea na kutafuta watu wengine. Baada ya changamoto kama hizo, ikaja akili mpya na kuandaa VIPEPERUSHI na kupita navyo kwenye SUPERMARKET na PHARMACY. Hii njia ilinisaidia sana hadi Pedi zikaisha, nikawa nimejuana na watu mbali mbali na kukuza kipato changu [ushuhuda mfupi wa Lackson Tungaraza]

Kwanini nakuambia MAISHA NI SAFARI!! Nataka ujue ya kwamba hiyo hatua uliyofikia ni katikati ya safari, je utarudi nyuma uanze upya tena au utaendelea ili ufike malengo uliyojiwekea kwenye maisha? Inawezekana safari ya kufikia mafanikio yako ni 100KM na sasa umefikisha 50KM. Ukirudi nyuma, ni sawa na umemaliza 100KM lakini haujafikia ulikotaka kwenda… ni sawa na kutoka Dodoma kwenda Dar halafu unaghairi safari yako Morogoro na kurudi tena Dodoma kisa umeona ya kwamba haufiki unakokwenda. SONGA MBELE, MAZURI ZAIDI YANAKUJA.
 
NI BORA UENDELEE MBELE KULIKO KURUDI NYUMA. UTAKUWA UMEJISUMBUA BURE


 Mmiliki wa kampuni ya soda ya PEPSI alifilisika mara tatu lakini alisonga mbele akiamini ipo siku atafika, na sasa unakunywa soda yake. Bill Gates aliambiwa ya kwamba dunia inahitaji Kompyuta 5 tu, lakini yeye aliamini ya kwamba atatengeneza Kompyuta ambazo kila mtu atakuwa na yake… Leo hii karibia kila mtu ana Kompyuta yake. MAISHA NI SAFARI NDEFU, ENDELEA MBELE KWA SABABU UNAKARIBIA KUFIKA.  

Whatsapp Group: 0764793105 [Lackson Tungaraza]
Instagram: LACKSONTUNGARAZA
Twitter: @lacksonthecoach

Lackson Tungaraza katika safari ya Ushindi.

2 comments:

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI