Wednesday, June 15, 2016

--------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Ukiangalia kwa Umakini, kuingia katika jambo lolote lile katika maisha yako kuna ugumu wake kuliko kutoka;

i.                   Ukitaka kuingia katika ukumbi wa kuonesha mpira, itakubidi ukate tiketi ambayo utaipata baada ya kutoa kiasi fulani cha pesa, lakini wakati wa kutoka hakuna anayekwambia ulipie

ii.                 Ili upate nafasi ya kuingia Bungeni, itakuhitaji uwe na mtu atakayekualika ambaye anajulikana humo bungeni au uwe ni mfanyakazi wa bungeni au kiongozi wa serikali ambaye unahitajika bungeni. Pia utafanyiwa ukaguzi wa hali ya juu sana wakati wa kuingia kuliko wakati wa kutoka

iii.              Ili uweze kuingia katika maisha ya Uanandoa; Itakubidi upate mwenzi sahihi, umchunguze vyema, ujitambulishe kwao na katika nyumba ya ibada, utoe mahari, sherehe ya harusi kama hali inaruhusu nk. Lakini wakati wa kutoka nje ya ndoa inaweza ikawa ni Talaka tu au bila taarifa wala gharama yoyote ile

Ingia katika Utendaji. Kama kuingia huwa kunaugumu wake kuliko kutoka, basi ujue ya kwamba ni wachache sana wanaoingia katika Utendaji…. Ingia ili utende, siyo kuwa mtazamaji.

Chukulia mfano wa mbegu ya mahindi, isipoingia katika utendaji baada ya kuwekwa ardhini hatuwezi kupita mmea wa Mhindi ambao utatupatia mahindi mengi.
--------------------------------------------------------------------------------
Je unapenda Kuchora, Kuimba, Uandishi, Uigizaji, Kufundisha? Ingia katika Utendaji. Kumbuka ya kwamba Punje isipofanya kazi iliyokusudiwa ardhini, hatutopata mmea wa mhindi.
---------------------------------------------------------------------------------
Thamini eneo ambalo Mungu amekuweka… shuleni, ofisini, mtaani. Usisubiri hadi uwe na shahada au stashahada ya sanaa ndipo uanze kuigiza au kuchora… Ingia katika Utendaji.

Mwanzo huwa mgumu, anza kidogo kidogo… Haba nah aba hujaza kibaba. Kila aliyekiongozi leo, jana alikuwa anaongozwa. Aliyemaarufu leo kuna wakati alikuwa hafaamiki… Ingia katika utendaji.


Kuwa na Baiskeli halafu hujui kuendesha, ni bora usiwenayo kwasababu utafanana na yule ambaye hajui kabisa kuendesha. Haujifunzi kuendesha baiskeli kwa kucheza mchezo wa mashindano ya baiskeli kwenye Kompyuta au kwa kusoma shuleni; Bali kwa kuingia katika utendaji. Kama punje ya mhindi iinavyohitaji udongo, maji, mwanga wa Jua, mbolea ili kukua vyema… Vivyo hivyo nawe pia utafanikiwa ikiwa utakuwa karibu na watu sahihi ambao mnaendana, kusoma vitabu sahihi ili kupata maarifa stahiki na pia kuwa na msukumo wa ndani wa kutenda (Burning desire).

Ingia katika utendaji, anza na ulichonacho siyo vile ulivyopoteza au unavyotamani kuja kupata. Value what you have Now, you’ll get what you don’t have Next.

ACTIONS SPEAK LOUDER THAN WORDS
Natumaini ya kwamba utakuwa umepata maarifa ya kukusaidia kufikia ile ndoto kubwa  unayotamani kuitimiza katika maisha yako.. aidha kuwa mwanasoka bora Afrika, kuwa Mwigizaji mkubwa duniani, kuwa Mwimbaji wa nyimbo za Injili au kuwa T.O [Tanzania One].

================================================
Kwa sasa Nimekwisha kuandika Kitabu kingine kiitwacho KIJANA TAMBUA NAFASI YAKO. Inawezekana kabisa Mungu amekupangia kuwa Mwanasiasa ili uikomboe nchi yako katika masuala ya siasa safi na hadi sahivi haupendi siasa na unang’ang’ania kuwa Rubani au Mwalimu yaani unachengana na NAFASI YAKO… Nafasi Yako inasifa mbili kuu, kujenga ufalme wa Mungu na kuleta maendeleo katika jamii yako siyo kwako tu. Utaijuaje Nafasi Yako? Kitabu hiki kitakupa Njia mbali mbali za kufuata katika kutambua Nafasi Yako… YOU WERE BORN TO WIN NOT TO LOSE. Unaweza ukashiriki katika Uchapishaji wa Kitabu hiki ili kiwahi kutoka kwa kutoa kiasi chochote cha fedha kama ambavyo Mungu atasema nawe. Utautuma katika Namba yangu ya Vodacom 0764793105 [Lackson Tungaraza] na kisha utanipatia na jina lako kamili ili nikuweke katika kumbu kumbu ya watu waliyofanikisha zoezi hilo.
=============================**=================

Ubarikiwe sana na Mungu, uwe na siku njema.
Kwa Maoni na Ushauri: 0764793105 [WhatsApp/sms].

                                   www.facebook.com/ltungaraza

1 comment:

  1. Nini maoni Yako juu ya hii mada ukilinganisha na ulivyokuwa ukichukulia mambo katika maisha yako?
    karibu sana katika uchangiaji wa mada

    ReplyDelete

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI