Tuesday, May 24, 2016

Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tele, una ndugu, una marafiki wazuri, umekula umeshiba, shughuli zako za kila siku zinafanikiwa, familia yako inaamani n.k.

Kumekuwa na mitazamo tofauti tofauti katika jamii kuhusiana na Semina zinazotolewa Mitandaoni; kwa njia ya Telegram, Wasap, Facebook n.k. Wengi wakiona tu tangazo linalotaarifu umma juu ya kuwepo kwa Semina fulani kupitia Whatsapp au Telegram, kichefuchefu kinawaingia na mara hiyo wanaondoka mitandaoni…ni nini tatizo!! Wengine wameshachukulia kama ni Utapeli mtupu, semina gani inayofanyikia mtandaoni tena kwenye Whatsapp? Tena, ingawa hiyo Semina inagusa moja kwa moja tatizo linalomsumbua lakini hawezi kuchukua hatua ya kufuatilia au kulipia gharama zilizowekwa ili kupata semina hiyo kwasababu Akilini mwake ameshaamini ya kwamba ni Utapeli.

Hii ni karne ya kisasa yenye maendeleo ya sayansi na teknolojia, majukumu yamekuwa ni mengi sana na watu wako bize. Wanandoa nao wako bize wakitafuta fedha ili familia isonge mbele, watu wanawahi kuamka asubuhi kuwahi katika shughuli zao na kuchelewa kurudi majumbani mwao, njiani pia foleni ya kutosha kwa wale waliopo kwenye miji mikubwa kama Dar, Mwanza, Arusha na hivyo kufika nyumbani wakiwa wamechoka sana na kupitiliza kulala, siku ya wikendi nayo mtu anapenda awe japo karibu na familia yake au atembelee miradi yake mbalimbali. Muda wa kuhudhuria kwenye Ukumbi wa Semina, anaupata wapi? Muda wa kutoka mkoa mmoja hadi mkoa mwingine ili akapate Semina labda ya Ndoa au biashara unapatikanaje? Hivyo ni baadhi tu ambao wanaweza kupangilia mambo yao vizuri na wakaudhuria Semina kwa wakati. Sasa hao wengine ambao hawapati muda wa kuhudhuria hizo Semina, elimu itawafikiaje?

Katika hali kama hiyo ndipo Umuhimu wa Semina za Mitandaoni zinahitajika ili mtu aweze kupata elimu stahiki kwa wakati sahihi bila kuathiri shughuli zake au muda wake wa kazi. Je! Kuna faida gani za kuhudhuria hizo semina za Mitandaoni, mfano kupitia Whatsap? Zifuatazo ni faida ambazo utazipata;

1.     Unapata Elimu stahiki ukiwa popote pale (Elimu Kiganjani Mwako)
Elimu hiyo unaipata ukiwa nyumbani, ofisini, kazini, safarini au sehemu yoyote ile ukiwa na simu yako au kompyuta inayokubali Intaneti na kuwa na Wasap ndani yake. Karne hii ya kisasa, mafunzo ya mtandaoni yameshika kasi sana kwa kiasi kikubwa. Kuna vyuo mbalimbali vinatoa mafunzo mtandaoni na kumwezesha mtu kupata Stashahada, Shahada, au Masters. Hii itakusaidia kupata masomo kwa uhuru, kwa wakati ambao uko free na sehemu yoyote ile uliyopo bila usumbufu wowote. Unaweza ukatoka ofisini kwako na ukachukua Simu au Kompyuta yako na kuanza kujifunza wakati umepumzika au wakati unakula bila kuathiri muda wako wa kazi.
Miaka ya sasa watu wamekuwa bize sana katika kutafuta maisha bora kutokana na kupanda kwa gharama za maisha, na hivyo inakuwa vigumu kwa watu kuacha shughuli zao na kwenda kwenye ukumbi fulani kuhudhuria Semina kutokana na ufinyu wa muda walionao. Kupitia Semina za mitandaoni, unapata Elimu stahiki kiganjani mwako kama elimu ya biashara na Ndoa mahali popote pale ulipo pasipo kuathiri shughuli zako.

2.     Gharama Nafuu~Low Cost
Badala ya kwenda sehemu na kukaa katika nyumba za wageni (guest house) au kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa gharama kubwa, unaweza kupata hii Semina hapo hapo nyumbani kwako kwa kutozwa kiwango kidogo cha fedha. Ni wewe tu kuwa na Simu au Kompyuta inayokubali intaneti

3.     Unaokoa Muda~Saving Time
Badala ya kusafiri na kutumia muda mwingi njiani, kwenda na kurudi. Lakini pia kuacha shughuli zako za siku na kwenda kwenye kumbi mbalimbali za Semina, sasa utaokoa muda wako kwa kupitia Online Seminars na ukawa unaendelea na kazi yako ya Ualimu, Udaktari, Ujasiriamali n.k.
          “TIME IS MONEY, HOW DO YOU INVEST YOUR TIME?”
Karibu sasa katika Semina yangu itakayoanza tarehe 07/06/2016, naamini ya kwamba hautojutia kabisa. Kuna mambo mengi sana utajifunza kupitia Simu au Kompyuta yako ukiwa hapo hapo kazini, safarini au nyumbani bila kuathiri shughuli zako. Jiandikishe sasa mapema, kwa Ushauri na Maswali binafsi tumia Wasap/sms kwa nambari 0764793105… Utapata elimu stahiki katika maeneo yafuatayo kwa njia ya Whatsapp na Email;

1. Jinsi Ya Kufanikiwa Maishani ikiwa hauna mtaji.

Mtaji ni kilio kwa wengi nawe ukiwa mmoja wao. Kwanini usichukue uwamuzi wa kuyaokoa maisha yako sasa ili upate kujua jinsi ya kuwa na maisha bora na kuzifikia ndoto zako hata kama hauna Mtaji.

2. Jinsi Ya Kupata Wazo Bora la Biashara.

Najua unataka kuanzisha biashara ya kukuinua kiuchumi katika viwango vikubwa lakini hujui ni biashara gani ufanye na kwa njia zipi. Pia unamawazo mengi ya biashara lakini hauna Mtaji na pia hujui lipi ulipe kupaumbele..Sogelea Semina sasa upate kujua

3. Umuhimu wa Maono Kwa Kijana.

Kijana mwenzangu acha kuishi maisha ya kubahatisha. IT'S BETTER TO BE BORN BLIND THAN TO LIVE A LIFE WITHOUT VISION. Ni afadhali ungezaliwa ukiwa kipofu wa macho kuliko kuishi pasipo kuwa na Maono. Maono yatakupa nidhamu nini ufanye na nini usifanye na kwa wakati gani. Ni dira yako ya maisha. Nikuulize, UNAJIONA UKO KATIKA MAISHA GANI BAADA YA MIAKA MITANO? Karibu sasa katika Semina hii ujue zaidi juu Ya Maono kwa kijana

4. Jinsi Ya Kuongeza Mauzo katika Biashara Yako

Mbinu utakazozipata hapa ni nzuri na kwa uhakika zitakusaidia sana..nimekuwa nikizitumia sehemu mbalmbal hata katika mitandao ya kijamii na zmezaa matunda. Usiwe mnyonge kwa sababu biashara yako haina faida ya kutosha, ni siri tu Fulani ambazo hujazipata...karibu sana uchote Maarifa

5. Kutengeneza Kipato cha ziada ukiwa kazini kwako

Hivi unatambua ya kwamba unaweza ukawa unaendesha biashara yako ukiwa hapo hapo kazini? Hamna ya kusubiri hadi upewe likizo au hadi wikendi Ifike...kupitia simu yako, kompyuta yako, mazingira yako ya kazi sasa unakwenda kutengeneza mfereji wa pesa
...usikae maskini kwa sababu ya mshahara mdogo na unatumia nguvu kubwa.

Hata wewe mama wa nyumbani hii siri itakusaidia kutengeneza pesa ukiwa hapo Hapo nyumbani kwako.

Jiandikishe mapema sasa kupitia Wasap kwa namba niliyoitoa hapo juu..semina ni Tsh. 10,000/- tu bila senti. Utaituma kwa nambari 0764793105[M-Pesa] na utaona jina langu Lackson Tungaraza. Ukishatuma utanijulsha kwa Meseji maana wanaotuma ni wengi. Pia Utapata Kitabu cha Biashara Bure.


CHOTA MAARIFA NA LACKSON TUNGARAZA.

www.lacksontungaraza.blogspot.com



0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI