Sunday, May 1, 2016


 
USIJIOGOPE... WEWE MWENYEWE NDIYE MSHINDANI.
Watu wengi sana katika maisha tunapenda kufanikiwa... Kuishi maisha ya kifahari, jamii kufahamu ya kwamba tupo, kupewa pongezi na watu mbali mbali. Mbona sasa hatufikii hiyo hatua!! Nini tatizo jamani?

🏃 Unashindana na nani katika maisha yako? Je! Ni rafiki yako au ndugu yako au jirani au mfanyakazi mwenzako? Ikiwa upo katika mojawapo ya hayo makundi ya watu ambao wanashindana na wengne, basi ndiyo maana hadi sasa bado maisha yako hayabadiliki. Unajitahidi sana kufanya kila jambo na bado hufanikiwi... Ni kwasababu unashindana na wengne... Compete with your own self.

🏃🏃Acha kushindana na watu wengne katika maisha ya kupata mafanikio. Kila mtu ananjia yake ya kufikia mafanikio... Njia aliyopitia Jack Ma tajiri wa China anayemiliki Alibaba ni tofauti na njia aliyopitia Bill Gates mmiliki wa kampuni ya Microsoft na njia tofauti na aliyoipitia Barack Obama.. Njia aliyoipitia Reginald Mengi ni tofauti na ya Erick Shigongo au Barhesa na watu wengne wengi. Hivyo ni vyema ukatambua njia yako ambayo ni Kushindana Na Unayemeona kwenye Kioo Unapojiangalia.

🔎Anza Leo kujichunguza vyema sana, kila mtu anaNafasi yake katika dunia hii. Nafasi ya Nabii Eliya ilikuwa ni kudhihirisha ya kwamba yupo Mungu mwingne mwenye uweza mkuu kuliko wa baali, Nyerere na Mandera Madiba walileta Uhuru na Ukombozi wa Afrika... Nafasi yako ni ipi?
 
KILA MMOJA WETU ANANAFASI SAWA YA KULETA MAENDELEO KWA KUSIMAMIA KUSUDI LA YEYE KUWEPO HAPA DUNIANI. JIULIZE NI KWA JINSI GANI KAMA KIJANA UTAIHUDUMIA JAMII YAKO.
📚Kila mtu anamaono na ndoto zake...hvyo hata mbinu na Mipango atakayotumia kufika kule anapokwenda ni tofauti na wewe... Unakuta kaweka Mipango ya kufungua salon, hoteli, kununua gari halafu nawe unaiga na kufanya hvyo ili kumuonesha ya kwamba nawe unaweza... Hapo unapoteza muda wako bure... Fanya kwako kwa ustadi mkubwa na utafanikiwa.

Mwambie huyo unayemwona kwenye Kioo ya kwamba utamshinda katika masomo, biashara n.k..
COMPETE WITH YOURSELF NOT OTHERS.

Nakutakia Mafanikio mema.

©Lackson Tungaraza
0764793105 whatsApp group.

Related Posts:

  • UJASIRIAMALI NI NINI? Kuna tafsiri mbali mbali katika vichwa vya watu na katika mitandao ya kijamii juu ya dhana ya UJASIRIAMALI. Wengi wamepata tafsiri zilizowapa presha na kuamua kuacha kuwa WAJASIRIAMALI, na baadhi hawatambua ni kwa namna gan… Read More
  • MAONGEZI YENYE MAANA NI YAPI HAYO... Tungaraza na Kijana Joseph katika Mjadala. Kila mara watu tunajikuta tupo au tunaingia wenyewe katika Mazungumzo, na hayo mazungumzo yanaweza yakawa yenye kuleta Matokeo chanya au hasi. Hivyo uhalali wa matokeo ya mazungumzo unategemeana na wahusika binafsi. Leo… Read More
  • JINSI YA KUWEKA MALENGO NA NAMNA YA KUFANIKISHA MALENGO YAKO  By Lackson Tungaraza 0764793105 whatsapp. Habari yako rafiki yangu mpendwa? Baada ya kuwa tumejifunza mada mbalimbali za ukombozi wa fikra na mafanikio ya kiuchumi. Napenda kukushukuru kwa ufuatiliaji wako katik… Read More
  • SIRI ILIYOPO KATIKA UTENDAJI -------------------------------------------------------------------------------------------------------------- -------------------------------------------------------------------------------------------------------------- … Read More
  • UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tele, una ndugu, una marafiki wazuri, umekul… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI