Sunday, May 1, 2016


 
USIJIOGOPE... WEWE MWENYEWE NDIYE MSHINDANI.
Watu wengi sana katika maisha tunapenda kufanikiwa... Kuishi maisha ya kifahari, jamii kufahamu ya kwamba tupo, kupewa pongezi na watu mbali mbali. Mbona sasa hatufikii hiyo hatua!! Nini tatizo jamani?

🏃 Unashindana na nani katika maisha yako? Je! Ni rafiki yako au ndugu yako au jirani au mfanyakazi mwenzako? Ikiwa upo katika mojawapo ya hayo makundi ya watu ambao wanashindana na wengne, basi ndiyo maana hadi sasa bado maisha yako hayabadiliki. Unajitahidi sana kufanya kila jambo na bado hufanikiwi... Ni kwasababu unashindana na wengne... Compete with your own self.

🏃🏃Acha kushindana na watu wengne katika maisha ya kupata mafanikio. Kila mtu ananjia yake ya kufikia mafanikio... Njia aliyopitia Jack Ma tajiri wa China anayemiliki Alibaba ni tofauti na njia aliyopitia Bill Gates mmiliki wa kampuni ya Microsoft na njia tofauti na aliyoipitia Barack Obama.. Njia aliyoipitia Reginald Mengi ni tofauti na ya Erick Shigongo au Barhesa na watu wengne wengi. Hivyo ni vyema ukatambua njia yako ambayo ni Kushindana Na Unayemeona kwenye Kioo Unapojiangalia.

🔎Anza Leo kujichunguza vyema sana, kila mtu anaNafasi yake katika dunia hii. Nafasi ya Nabii Eliya ilikuwa ni kudhihirisha ya kwamba yupo Mungu mwingne mwenye uweza mkuu kuliko wa baali, Nyerere na Mandera Madiba walileta Uhuru na Ukombozi wa Afrika... Nafasi yako ni ipi?
 
KILA MMOJA WETU ANANAFASI SAWA YA KULETA MAENDELEO KWA KUSIMAMIA KUSUDI LA YEYE KUWEPO HAPA DUNIANI. JIULIZE NI KWA JINSI GANI KAMA KIJANA UTAIHUDUMIA JAMII YAKO.
📚Kila mtu anamaono na ndoto zake...hvyo hata mbinu na Mipango atakayotumia kufika kule anapokwenda ni tofauti na wewe... Unakuta kaweka Mipango ya kufungua salon, hoteli, kununua gari halafu nawe unaiga na kufanya hvyo ili kumuonesha ya kwamba nawe unaweza... Hapo unapoteza muda wako bure... Fanya kwako kwa ustadi mkubwa na utafanikiwa.

Mwambie huyo unayemwona kwenye Kioo ya kwamba utamshinda katika masomo, biashara n.k..
COMPETE WITH YOURSELF NOT OTHERS.

Nakutakia Mafanikio mema.

©Lackson Tungaraza
0764793105 whatsApp group.

Related Posts:

  • UNAKIMBIA KWA STAILI GANI? Moja ya tafsiri za Maisha nilizowahi kuzisoma na kuzisikia ni kwamba Maisha ni Mbio. Cha kujiuliza, “Unakimbizana na nani?” Nimegundua ya kwamba Maisha ni Mbio ambayo Mshindani ni wewe mwenyewe… unajipulizia mwenyewe kipen… Read More
  • PATA MAARIFA KWA KUWA MKIMYA ~ Wanadamu hata siku moja haitawahi kutokea tukawa sawa kimtazamo, kimienendo..never. Unaweza ukajiulza mbona Mimi ninajiheshima, mpole, mvumilivu lakini huyu ndugu yangu ni mkorofi sana, mlevi, mbeya, mzinzi n.k. Hyo … Read More
  • JE KIJANA UNAHAMU YA KUWA NA MAISHA YENYE FURAHA NA MAFANIKIO? Ni haki yako Kijana Mwenzangu kuwa na Maisha yenye furaha na Mafanikio. Tumia ushauri ufuatao ili uweze kufikia lengo hilo; … Read More
  • LIFE IS A PROCESS [Maisha Ni Mlolongo Wa Mambo] Ni nini maana ya neno ‘Maisha?’ Kila mtu anaweza kutoa maana ya neno Maisha kwa yale aliyoyapitia, anayoyapitia au anayotarajia kukutana nayo mbeleni. Maisha yanamaana nyingi sana na kulingana na mtazamo wa kila mtu, ja… Read More
  • UMUHIMU WA RATIBA KATIKA MAISHA YAKO Maisha ya Mwanadamu yana mwanzo na mwisho, ikiwa na maana ya kwamba kuna kuzaliwa na kufariki. Lakini katikati ya kuzaliwa na kufariki kuna mambo ambayo Mwanadamu anatakiwa afanye ili aweze kustahimili hali ya kimwili na… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI