Saturday, May 7, 2016


Ni nini maana ya neno ‘Maisha?’
Kila mtu anaweza kutoa maana ya neno Maisha kwa yale aliyoyapitia, anayoyapitia au anayotarajia kukutana nayo mbeleni. Maisha yanamaana nyingi sana na kulingana na mtazamo wa kila mtu, jaribu kujiuliza wewe binafsi, maisha yanamaana gani kwako. Je, kuwa na Mke Mrembo ndiyo maisha? Kuwa na Magari na Majumba ya Kifahari ndiyo Maisha? Nimesikia watu wengi sana wa Vijijini wakisema ya kwamba wanaenda Mijini kutafuta Maisha, sijui maana ya Maisha kwao ni nini hadi wanaenda kuyatafuta Mijini na siyo Vijijini.

Hiyo yote ni mitazamo kama nilivyosema hapo awali, naomba leo Lackson Tungaraza nizungumzie Maisha kwa namna ambayo mtu anakuwa Kimwili na Kiakili. Ukujitazama hapo ulipo sasa na jinsi ulivyokuwa Miaka miwili au mitatu huko nyuma ni tofauti kabisa; Aidha ni kiumbile au kiakili. Kama vile ambavyo imekuchukua muda mrefu kufikia kimo cha urefu ulionao leo na uwezo wako wa kuchukulia mambo kwa upana zaidi, ndivyo ambavyo nasema MAISHA NI HATUA… Mlolongo wa Mambo. Mafanikio pia katika maisha ni hatua, hakuna Mafanikio ya kulala Maskini na kuamka Tajiri hata kama ni kwa kutumia nguvu za giza au kuwa mwanachama wa Freemasons kama wengine wanavyodhani… bado kuna mambo kadha wa kadha yanakuhitaji kutenda kwanza ili kufika kule unakotaka. Mambo mazuri hayapatikani haraka au kwa uwepesi, dhahabu ni ya thamani sana na ndiyo maana hata upatikanaji na uchimbaji wake ni mgumu.

Kuna watu ambao wamekata tamaa kwa sababu yay ale waliyoyapitia au wanayoyapitia sasa… Rafiki na ndugu wamewatenga kwa sababu ya umaskini wao, waume wao wamewaacha kwa sababu wanaonekana ni kama Magoli kipa… Ni waambie tu ya Kwamba Life Is A Process as long as you want to grow.

Chukua maamuzi leo ya kuwa dereva wa maisha yako na uangalie ni barabara gani nzuri utakayotumia ili safari yako iwe salama. Najua kuna mambo mengi ambayo unatamani uwe nayo kwenye maisha, hayatakuja hadi uyatafute… Atafutaye huona, abishaye hufunguliwa, aombaye hupewa. Anza kufanya hatua kwa hatua bila kuogopa changamoto ukiamini ya kwamba siku moja mambo yatakuwa sawa maana unamtumaini Mungu… One day YES, by doing not saying. Mtoto mdogo anapotaka kutembea, hata akianguka mara ngapi na kuumia bado anaendelea tu kujaribu tena na tena hadi atembee. Wakati mwingine Mama yake anamnunulia kigari kidogo cha kujifunzia kutembea, nawe ikiwezekana tafuta mtu au watu ambao watakusaidia kusonga mbele.

Siku moja waliokuwa wanakucheka na kudharau juhudi zako, watakusalimia kwa heshima na kuomba Siri ya Mafanikio yako. Chukulia mfano wa mti unapokuwa mdogo (Mche) watu huwa wanaudharau na hata kuupiga piga mateke na kutegea katika kuupatia maji ya kutosha. Lakini pindi unapokuwa mkubwa, wale wale watu hutafuta kivuli kwenye huo Mti, kupata Mbao kwaajili ya Ujenzi na wengine kupata dawa pamoja na vitamin C kwa maa ya Matunda. You Present Situation is not final destination, the Best is yet to come.
MAISHA NI MFANO WA MCHE UNAOKUA


Tazama Changamoto kama ni daraja la kukuvusha kwenda ng’ambo ya pili… ANegative Thinker sees a Difficulty in every Opportunity while a Positive Thinker sees an Opportunity in every Difficulty… The word NO means Next Opportunity. Bila Changamoto nilizopitia katika maisha, nisingekuwa na uwezo wa kuandika haya unayoyasoma hivi leo wala kugundua ya kwamba Kalamu ya Uandishi ndiyo Silaha yangu ya kuifikia jamii. Ndiyo maana sahivi nachukulia Changamoto kama Ngazi ya kunipandisha juu… huwezi kuwa mtu mkubwa maishani bila kupitia mambo makubwa, angalia maisha ya Mfalme Daudi au Mwl. Nyerere ndipo utaelewa ninachokiandika hapa… I have Never met a great person with an Easy past.



Natumaini ya kwamba utakuwa umepata Maarifa ya kukusaidia kusonga mbele zaidi kwa sababu Life Is A Process… Hutaogopa tena Changamoto wala kuwa na hofu ya kuonesha thamani yako katika jamii… Wasambazie na rafiki zako ujumbe huu WhatsApp, Facebook, Twiiter na katika mitandao mbali mbali ya kijamii ili nao waweze kuwa sambamba na maisha…. Karibu pia katika kundi langu la Whatsapp [0764793105]. Uwe na wakati mwema, tukutane tena katika mada nyingine….toa maoni yako kwa mada yoyote ile ambayo unatamani niigusie zaidi ambayo nimekwisha kuifundisha lakini haikuelewa au bado sijaifundisha na unaipenda, karibu sana usisite kwasababu ndiyo mwanzo wa Life Is a Process.

Related Posts:

  • WHAT DO YOU HAVE? UNA NINI? Do you Need Success? Do you want a Life of Prosperity? Do you Love walking with God at Higher Standards? Are you Passionate of having a Job or a Business? WHAT DO YOU HAVE? UNA NINI? Every Now and Then, People Seek New th… Read More
  • "I DON'T STOP WHEN I'M TIRED, I STOP WHEN I'M DONE"*Akasema, YOTE IMEKWISHA. LIFE is PERFORMANCE. Na Mara unapoanza Kuperfom ndipo unaanza kutambua aina ya wasikilizaji na watazamaji ulionao. Aidha wako pamoja nawe, au la. That's how life is in this world. Bahati Bukuku a… Read More
  • DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO.Ukubali, Ukatae.. Ukweli unabaki pale pale ya kwamba DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO. Karibu tupeane Maarifa kidogo hapa, Kujifunza Kitu Kipya Kila Mara ni sifa kubwa ya watu wenye Mafanikio Makubwa maishani. -Binafsi napen… Read More
  • ANDIKA JINA LAKO VIZURI Heri Kuchagua Jina jema kuliko Mali nyingi [smart phones, kompyuta, iPhone, iPad, gari, nyumba, nguo, shamba, ng'ombe]; Na Neema kuliko fedha na dhahabu.. Mith 22:1 Watu wengi sana hawajali juu ya majina wanayojiita au … Read More
  • JE UNAJIKUBALI...! #KUJIKUBALI NI HATUA KUBWA SANA NA YA KWANZA KATIKA MAISHA ILI MTU AWEZE KUFURAHIA UUMBAJI WA MUNGU. #Hivi unamkubali kwa asilimia ngapi huyo unayemwona kwenye Kioo unapojiangalia? #Kuna waliojikatia tamaa kabisa, hawata… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI