Wednesday, March 16, 2016



~Nilipokuwa mtoto nilipendelea sana kutazama muvi za ngumi ( action movies), katika kuangalia kwangu nilishangaa kuona ya kwamba muhusika mkuu wa Muvi ambaye ndiye anaitwa STARRING alikuwa hafi hata kama amekutana na majanga kiasi gani.

~ Wanajeshi wengi walikuwa wanaagizwa kwenda kukomboa mateka Vietnam, wengi walikuwa wanauawa sana tena kinyama lakini STARRING alibaki kuwa hai. Japokuwa alikuwa anapigwa kisawa sawa hata kulko wanajeshi wenzake lakini bado alibaki kuwa hai na kushinda vita.

~KWANINI UWE STARRING WA MAISHA YAKO? Inawezekana umesoma kichwa cha somo na hukuelewa au ulitafsiri kivingne. Starring siku zote ndiye Muhusika mkuu wa fedha na ndiye mwamuzi wa mwisho wa hatima ya Adui zake ambao ndiyo huitwa Majambazi au Mamluki.

~Ili ufanikiwe maishani mwako kwa jambo lolote lile kuanzia sasa unaposoma ujumbe huu wa Lackson Tungaraza, jaribu nafasi ya kuwa STARRING wa maisha yako. Acha nafasi zingne zote za uigizaji kama Ulinzi, Ubaba au Umama..kuwa Starring. Changamoto zisikukatishe tamaa ya kuendelea mbele. Majungu ya watu yasikurudishe nyuma kabisa. Wewe ni Starring na mwisho wa picha wewe ndye Mshindi.

~Sijawahi ona jambazi ndiye anakuwa mshindi wa Muvi..ikiwa hivyo basi ujue kuna mwendelezo wa hiyo Picha(new episode). Ni maamuzi yako juu ya hatima ya Yale yanayokukumba katika maisha ya kila siku. Kama movie ambavyo jambazi akibaki hai hadi mwisho wa picha wanatengeneza mwendelezo wake...hunabudi na wewe kusimama tena na kurudi kupambana hata kama mwanzoni ulikuwa umekata tamaa katika biashara, masomo au ndoa yako. Katika episode inayofuata jihakikishie wewe Starring kuwa Mshindi bila kufa.

~ Mimi nimeshachagua kuwa STARRING wa maisha yangu. Ndiye mwamuzi wa hatima ya changamoto zinazonikabili(jambazi katika muvi)... Simlaumu mwingne ila ninapambana nazo kwa kutumia maarifa mbalmbal ya kiuStarring. WEWE JE? Hujachelewa, amua sasa . THE DOOR TO SUCCESS IS OPEN, WAITING FOR YOU TO ENTER. Make a move.

~ Natumaini umejifunza jambo litakalokusaidia maishani. Sambaza kwa wengne pia wapate maarifa bila kuedit chochote na utabarikiwa sana. Usisite pia kutoa maoni yako.


 By Lackson Tungaraza
0764793105 wasap.

CHOTA MAARIFA.

www.lacksontungaraza.blogspot.com

Related Posts:

  • MAMBO MATATU MUHIMU YA KUFANYA KIJANA KABLA YA KUANZA KUTAFUTA PESA YA KUFANYA BIASHARA Kijana mwenzangu kabla hujaanza kusumbuka kutafuta pesa kila mahala kwaajili ya biashara.  Kwanza Fanya maamuzi ni biashara gani unayohitaji kufanya, hiyo ni hatua ya kwanza kabisa. Kwanini ufanye uwamuzi kwanza? Ili k… Read More
  • FACEBOOK VS BLOG KIPI NI BORA KWA BIASHARA YAKO? Kumekuwa na sitofahamu juu ya namna ya kutumia mitandao hii katika kukuza biashara. Ndiyo maana nimekuuliza; Kati ya Facebook na Blog, ni kipi bora kwa Biashara yako? Jibu lako litaash… Read More
  • HABARI NJEMA KWAKO MTANZANIA * Uhusiano wa Binadamu na Panga* Ukitaka kujua ukali wa Wembe, sugua kidole chako kwenye upande wa Makali yake. Vivyo hivyo na kwa binadamu, huwezi ona makali yake kwa sasa hadi pale Makali yake yatakapoonekana. Binadamu… Read More
  • WHY ONLINE SEMINARS? UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tel… Read More
  • SIRI AMBAZO MFANYA BIASHARA HUJAZIJUA  “JINSI YA KUFANYA BIASHARA YAKO KUWA YA TOFAUTI NA YENYE MVUTO MKUBWA”  Tunashindwa kuongeza vipato vyetu kwa sababu biashara zetu hazina mvuto. Tunapoendelea kufungua vyanzo vingine vya vipato kwa kut… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI