Thursday, March 10, 2016


UKWELI JUU YA SEMINA ZA MTANDAONI

Natumaini wewe ni mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli zako za kila siku. Ni jambo jema sana la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kukupatia siku nyingine tena ukiwa na nguvu tele, una ndugu, una marafiki wazuri, umekula umeshiba, shughuli zako za kila siku zinafanikiwa, familia yako inaamani n.k.

Kumekuwa na mitazamo tofauti tofauti katika jamii kuhusiana na Semina zinazotolewa Mitandaoni; kwa njia ya Telegram, Wasap, Facebook n.k. Wengi wakiona tu tangazo linalotaarifu umma juu ya kuwepo kwa Semina fulani kupitia Whatsapp au Telegram, kichefuchefu kinawaingia na mara hiyo wanaondoka mitandaoni…ni nini tatizo!! Wengine wameshachukulia kama ni Utapeli mtupu, semina gani inayofanyikia mtandaoni tena kwenye Whatsapp? Tena, ingawa hiyo Semina inagusa moja kwa moja tatizo linalomsumbua lakini hawezi kuchukua hatua ya kufuatilia au kulipia gharama zilizowekwa ili kupata semina hiyo kwasababu Akilini mwake ameshaamini ya kwamba ni Utapeli.

Hii ni karne ya kisasa yenye maendeleo ya sayansi na teknolojia, majukumu yamekuwa ni mengi sana na watu wako bize. Wanandoa nao wako bize wakitafuta fedha ili familia isonge mbele, watu wanawahi kuamka asubuhi kuwahi katika shughuli zao na kuchelewa kurudi majumbani mwao, njiani pia foleni ya kutosha kwa wale waliopo kwenye miji mikubwa kama Dar, Mwanza, Arusha na hivyo kufika nyumbani wakiwa wamechoka sana na kupitiliza kulala, siku ya wikendi nayo mtu anapenda awe japo karibu na familia yake au atembelee miradi yake mbalimbali. Muda wa kuhudhuria kwenye Ukumbi wa Semina, anaupata wapi? Muda wa kutoka mkoa mmoja hadi mkoa mwingine ili akapate Semina labda ya Ndoa au biashara unapatikanaje? Hivyo ni baadhi tu ambao wanaweza kupangilia mambo yao vizuri na wakaudhuria Semina kwa wakati. Sasa hao wengine ambao hawapati muda wa kuhudhuria hizo Semina, elimu itawafikiaje?

Katika hali kama hiyo ndipo Umuhimu wa Semina za Mitandaoni zinahitajika ili mtu aweze kupata elimu stahiki kwa wakati sahihi bila kuathiri shughuli zake au muda wake wa kazi. Je! Kuna faida gani za kuhudhuria hizo semina za Mitandaoni, mfano kupitia Whatsap? Zifuatazo ni faida ambazo utazipata;

1.     Unapata Elimu stahiki ukiwa popote pale (Elimu Kiganjani Mwako)
Elimu hiyo unaipata ukiwa nyumbani, ofisini, kazini, safarini au sehemu yoyote ile ukiwa na simu yako au kompyuta inayokubali Intaneti na kuwa na Wasap ndani yake. Karne hii ya kisasa, mafunzo ya mtandaoni yameshika kasi sana kwa kiasi kikubwa. Kuna vyuo mbalimbali vinatoa mafunzo mtandaoni na kumwezesha mtu kupata Stashahada, Shahada, au Masters. Hii itakusaidia kupata masomo kwa uhuru, kwa wakati ambao uko free na sehemu yoyote ile uliyopo bila usumbufu wowote. Unaweza ukatoka ofisini kwako na ukachukua Simu au Kompyuta yako na kuanza kujifunza wakati umepumzika au wakati unakula bila kuathiri muda wako wa kazi.
Miaka ya sasa watu wamekuwa bize sana katika kutafuta maisha bora kutokana na kupanda kwa gharama za maisha, na hivyo inakuwa vigumu kwa watu kuacha shughuli zao na kwenda kwenye ukumbi fulani kuhudhuria Semina kutokana na ufinyu wa muda walionao. Kupitia Semina za mitandaoni, unapata Elimu stahiki kiganjani mwako kama elimu ya biashara na Ndoa mahali popote pale ulipo pasipo kuathiri shughuli zako.

2.     Gharama Nafuu~Low Cost
Badala ya kwenda sehemu na kukaa katika nyumba za wageni (guest house) au kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa gharama kubwa, unaweza kupata hii Semina hapo hapo nyumbani kwako kwa kutozwa kiwango kidogo cha fedha. Ni wewe tu kuwa na Simu au Kompyuta inayokubali intaneti

3.     Unaokoa Muda~Saving Time
Badala ya kusafiri na kutumia muda mwingi njiani, kwenda na kurudi. Lakini pia kuacha shughuli zako za siku na kwenda kwenye kumbi mbalimbali za Semina, sasa utaokoa muda wako kwa kupitia Online Seminars na ukawa unaendelea na kazi yako ya Ualimu, Udaktari, Ujasiriamali n.k.

          “TIME IS MONEY, HOW DO YOU INVEST YOUR TIME?”


Karibu sasa katika Semina yangu itakayoanza tarehe 21/3/2016, naamini ya kwamba hautojutia kabisa. Kuna mambo mengi sana utajifunza kupitia Simu au Kompyuta yako ukiwa hapo hapo kazini, safarini au nyumbani bila kuathiri shughuli zako. Jiandikishe sasa mapema, kwa Ushauri na Maswali binafsi nipo Wasap kwa nambari 0764793105. Tangazo hili limeelezea vizuri;




0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI