Tuesday, February 16, 2016


By Lackson Tungaraza
0764793105 whatsapp

Hapo ulipo sahivi unaangaika kwasababu unataka Mafanikio, jiulize kwanza Mafanikio yana maana gani kwa upande wako!! Kila mmoja wetu anahitaji mafanikio katika mambo anayoyafanya; Mwanafunzi, mwalimu, mwajiri, mwajiriwa, viongozi mbali mbali wa kiserikali na wa kidini, vijana, wazee , wote wanahitaji mafanikio kwa viwango tofauti tofauti kulingana na msukumo uliomo ndani ya mtu juu kile anachokihitaji. Mimi mwenyewe Lackson Tungaraza ninayeandika haya, ninahitaji mafanikio na ndiyo maana ninapenda na wewe uwe pamoja nami katika kupata mafanikio stahiki. Mafanikio hayaji bila kufahamu njia ya kupitia, leo nitakupa Mambo Matatu Muhimu ili uweze Kufanikiwa;

    §     Watu;
Watu ni rasilimali kubwa sana katika jamii yoyote ile ili iweze kuendelea. Bila watu kusingekuwa na haja ya kufanya mapinduzi ya kisiasa au kibiashara. Ili ujue umuhimu wa watu katika kuleta mabadiliko yoyoye yale katika jamii, fikiria ambavyo vyama mbali mbali vya kisiasa vinatumia gharama kubwa kutafuta wafuasi kabla na baada ya Chaguzi mbali mbali. Watu mbali mbali pia wamepata nguvu za Ushawishi katika jamii kwa sababu ya kuwa na watu ambao ni wafuasi wake, nawe pia unahitajika kuwa na watu ili uweze kufanikiwa katika hiyo biashara, dhehebu, shule, kampuni yako n.k. Hivyo tengeneza urafiki na watu mbali mbali katika jamii ili uweze kuyafikia mafanikio yako

    §  Watu sahihi
Baada ya kuwa umepata watu mbali mbali katika jamii, ni wakati sasa wa kufuata hatua hii ya pili ya kuwa na watu sahihi. 75% ya yale ambayo watu wanayo na wanayoyafanya, yanatokana na ushawishi wa watu ambao wanaambatana nao. Kuwa watu walioingia vyuo vikuu wakiwa na tabia njema lakini bada ya kuanza kuambatana na watu wasio sahihi, tabia zao zikabadilika na kuwa hatarishi zaidi. Wengine pia walizaliwa katika familia ya watu maskini lakini wakapata bahati ya kuwa karibu na watu wanaotoka katika familia zenye maendeleo ya kiuchumi, nao wakaanza kubadilika mitazamo yao na baadaye kufanikiwa. Vivyo hivyo inakubidi nawe uchague watu ambao ni sahihi kati ya hao ulionao, siyo kila rafiki ni sahihi. Ambatana na watu ambao watakuwezesha kuyafikia mafanikio, kuanzia hapo ulipo na hata katika mitandao ya kijamii. Usipokuwa na watu sahihi, utachelewa kufikia mafanikio au usifanikiwe kabisa.

    §  Taarifa Sahihi
Taarifa pia unazopata kutoka kwa watu hao, inabidi iwe sahihi. Watu wengi wamekimbia ndoa zao, biashara zao, wokovu, shule kwa sababu ya kupokea taarifa zisizo sahihi kutoka kwa watu waliokuwa karibu nao. Unapopata taarifa fulani, jaribu kuichunguza kama ni sahihi kwasababu inaweza kukuinua au kukuangamiza kabisa. Siyo kila taarifa ni ya kuiweka moyoni au katika utekelezaji, chambua zinazokufaa katika eneo lako unalotaka kufanikiwa. Tafuta taarifa za kibiashara kama unafanya biashara au unataka kuwa mfanyabiashara, taarifa za wokovu wa kweli kama unataka kumtumikia Mungu, taarifa za udaktari kama unataka kuja kuwa daktari au kama wewe ni daktari n.k. Kuwa makini sana katika mambo haya Matatu ili uweze kuyafikia mafanikio stahiki.


Natumaini utakuwa umejifunza jambo fulani ambalo litakupa hatua zaidi kuelekea katika ulimwengu wa mafanikio, sambaza somo hili kwa rafiki zako mbali mbali ili nao pia wapate kujifunza (share). Ubarikiwe sana na uwe na siku njema.  

Related Posts:

  • FIKIRIA NJE YA BOX All the so-called 'Secrets of Success' will not work unless you do--Unknown. Siri za mafanikio ni nyingi sana na utaendelea kuzisikia na kuzisoma sehemu mbali mbali.. Mtandaoni, magazetini, vitabuni nk..... Sidhani kama k… Read More
  • DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO.Ukubali, Ukatae.. Ukweli unabaki pale pale ya kwamba DUNIA NI UWANJA WA MAPAMBANO. Karibu tupeane Maarifa kidogo hapa, Kujifunza Kitu Kipya Kila Mara ni sifa kubwa ya watu wenye Mafanikio Makubwa maishani. -Binafsi napen… Read More
  • NJIA MPYA YA KUTENGENEZA KIPATO CHA ZIADAHaijalishi una Kazi ama hauna Kazi, kikubwa ni UTAYARI wako pamoja na Kiasi kidogo cha #PESA kuanzia Tsh.4000/= Sasa Unaweza Kutengeneza Kipato cha Ziada (PESA) kupitia Kitabu changu "SITARUDI NYUMA TENA" - Sitaki KUFANIKI… Read More
  • FACEBOOK VS BLOG KIPI NI BORA KWA BIASHARA YAKO? Kumekuwa na sitofahamu juu ya namna ya kutumia mitandao hii katika kukuza biashara. Ndiyo maana nimekuuliza; Kati ya Facebook na Blog, ni kipi bora kwa Biashara yako? Jibu lako litaash… Read More
  • "SIRI ZA MAFANIKIO!" (Lackson Tungaraza) ▪Zipo Siri nyingi sana za Mafanikio zilizokuwepo, zilizopo, na zitakazoendelea Kuwepo Siku zote maadam Watu Wanaendeleo kufanya Tafiti na kufanikiwà. ▪Kufanikiwa Kimaisha hakukuhitaji Kujua kwanza Siri zote za Mafaniki… Read More

0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI