Wednesday, April 17, 2019

KWA MAHITAJI YA;

(1) KUANDIKIWA #VITABU.

- Yawezakuwa Una wazo Zuri la kuwa na KITABU Chako kama Wengine lakini Hujui namna ya Kukiandika hadi kikamilike. Kumbuka ya kwamba Sio Kila aliye na kitabu alikiandika Yeye Mwenyewe. Wapo Watu Wengi wanaoandikiwa Vitabu na Watu Wengine Wenye UJUZI mzuri wa Uandishi. Kwa hiyo siyo Lazima uende leo Kujifunza Namna ya Kuandika Vitabu Ikiwa umebanwa na Shughuli zingine nyingi, au hauna hiyo Shauku ya kuketi chini kwa masaa Mengi Ukiwa unaandika Kitabu. Sasa Usiwe na Shaka, NJOO Kwetu UHUDUMIWE Vizuri.
.

(2) KUPANGILIWA KITABU ILI KIWE NA MWONEKANO MZURI WA NDANI.

- Inawezekana Umekwisha Kuandika Kitabu chako kwenye soft copy  (nakala tete), lakini unawaza bila kupata majibu ya namna ya kukipangilia ili kiwe na Ubora mkubwa kama Vitabu vingine vya Watu mashuhuri Duniani. Usiwe na Shaka, njoo Kwetu Upate hiyo huduma. Kumbuka; Mpangilio mzuri wa Kitabu ni Jambo la Msingi sana ili kiweze kuwavutia Wasomaji wakubwa wa Vitabu.
.

(3) KUTENGENEZEWA JALADA ZURI LA KITABU.

- Wazungu wa zamani walikuwa wanasema ya kwamba DON'T JUDGE A BOOK BY ITS COVER (Usikihukumu Kitabu kwa Mwonekano wa Jalada lake). Jambo ambalo Kwetu tunalipinga sana. Mwonekano wa Kitabu ni wa thamani sana kama ulivyo Mwonekano Wako mbele ya Watu Wengine unaokutana nao kwa Mara ya kwanza. Watu bora huwa na vitu bora, na Mojawapo ni kuwa na Majalada ya Vitabu Yenye kuvutia MACHO ya Mtazamaji. Kwa hiyo unapaswa kuwa na "Cover" la Kitabu ambalo mtu akiliona Mtandaoni au maktaba, Basi anavutiwa kusogea karibu ili ajue Yaliyomo ndani Yake.
.

(4) KUFUNDISHWA MBINU NA NAMNA YA KUANDIKA VITABU.

- Hakuna Mtu anayezaliwa akiwa anajua Kila kitu. Kila Mtu anatakiwa Kujifunza ili aweze kufanikiwa na Kustawi Kimaisha. Na Mojawapo ya mambo ya muhimu sana ni kuwa na UJUZI. Sasa ujuzi/kipawa cha Uandishi wa Vitabu nacho Unaweza ukajifunza na kuwa mahiri. Uandishi wa Vitabu una mambo Yake ya Kipekee kama ilivyo kwa idara zingine. Njoo ujifunze Kwetu.
.

(5) KUFANYIWA MAREKEBISHO YA KITABU (Proof-Reading).

- Kitabu kikiwa na Makosa Mengi ya kiuandishi ni ISHARA ya kwamba aliyekiandika hakuwa makini (serious) na kazi Yake. Sasa Kuandika Kitabu ni Jambo moja, na Kukipitia ni Jambo jingine kabisa ambalo linahitaji Umakini na Nguvu ya ziada.  Sasa Ikiwa hauna muda wa kufanya hivyo au kwa Sababu yo yote Ile, karibu sana Kwetu UHUDUMIWE Vizuri sana.

#KUMBUKA:
LAMAX DESIGNS Inakupatia unachostahili  - Lamax Designs "providing you what you deserve."

KARIBU SANA LAMAX DESIGNS UPATE UNACHOSTAHILI KWA GHARAMA INAYOKUFAA.

#Mawasiliano: +255 (0) 764 793 105
#Email: lamaxdesigns@gmail.com
HUDUMA ZA LD-LAMAX DESIGNS 


0 comments:

Post a Comment

MAKUNDI YA MASOMO YETU

CHAGUA MASOMO HAPA

Powered by Blogger.

ZILIZOSOMWA ZAIDI